Fredrick Sanga
JF-Expert Member
- Jan 27, 2011
- 3,153
- 697
Friday, 22 April 2011
Fidelis Butahe
MWASISI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edwin Mtei amesema siku za CCM kukaa madarakani zinahesabika kwa kuwa chama hicho kimekosa usimamizi bora na hivyo kuiyumbisha nchi.
Akijibu maswali mbalimbali ya Mwananchi jana, Mtei alisema chama hicho kimeshindwa kutatua matatizo yanayowakabili Watanzania, suala ambalo litaifanya kupotea katika ramani ya utawala wa nchi.
"Siku za CCM kukaa madarakani zinahesabika, yaani natamani hata uchaguzi ufanyike kabla ya 2015,"alisema Mtei.
Mtei ametoa kauli hiyo ikiwa ni siku moja baada ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye kukaririwa akisema kwamba, hatua inayofuata katika vita ya ufisadi ndani ya CCM, ni kwa viongozi wa Serikali wa ngazi zote ambao wamekuwa wakikisaliti chama hicho kwa kujifanya miungu watu.
Kwa mujibu wa Mtei, Chadema ndio chama kitakachochukua nchi baada ya CCM, kwani chama hicho tawala, kinakosa viongozi waadilifu na wanaojali matatizo ya Watanzania.
Mtei ambaye aliwahi kuwa gavana wa kwanza mzalendo wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) nchini, alisema chama imara ni kile chenye sera za kutatua matatizo ya nchi na watu wake na sio "kujivua gamba".
Alisema kuwa Chadema ni chama imara kwa kuwa kina viongozi waadilifu ambao wako tayari kubuni mikakati mbalimbali kwa ajili ya kuwaletea wananchi maendeleo.
Mtei alisema kitendo cha CCM kuwachukulia hatua watuhumiwa wa ufisadi ikiwa ni pamoja na kuwapa siku 90 wanaweza kutimkia vyama vya siasa huku akisisitiza kuwa Chadema haitakuwa tayari kuwapokea.
"Chadema hakiwezi kukubali watuhumiwa wa ufisadi, yaani Watanzania wanataka wahukumiwe kwa ufisadi wao leo hii Chadema tuwapokee, hakuna kitu kama hicho, Watanzania wako wengi sana na wanaoingia Chadema wapo pia ila kwa watuhumiwa wa ufisadi hapana, haiwezekani,"alisisitiza
Fidelis Butahe
MWASISI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edwin Mtei amesema siku za CCM kukaa madarakani zinahesabika kwa kuwa chama hicho kimekosa usimamizi bora na hivyo kuiyumbisha nchi.
Akijibu maswali mbalimbali ya Mwananchi jana, Mtei alisema chama hicho kimeshindwa kutatua matatizo yanayowakabili Watanzania, suala ambalo litaifanya kupotea katika ramani ya utawala wa nchi.
"Siku za CCM kukaa madarakani zinahesabika, yaani natamani hata uchaguzi ufanyike kabla ya 2015,"alisema Mtei.
Mtei ametoa kauli hiyo ikiwa ni siku moja baada ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye kukaririwa akisema kwamba, hatua inayofuata katika vita ya ufisadi ndani ya CCM, ni kwa viongozi wa Serikali wa ngazi zote ambao wamekuwa wakikisaliti chama hicho kwa kujifanya miungu watu.
Kwa mujibu wa Mtei, Chadema ndio chama kitakachochukua nchi baada ya CCM, kwani chama hicho tawala, kinakosa viongozi waadilifu na wanaojali matatizo ya Watanzania.
Mtei ambaye aliwahi kuwa gavana wa kwanza mzalendo wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) nchini, alisema chama imara ni kile chenye sera za kutatua matatizo ya nchi na watu wake na sio "kujivua gamba".
Alisema kuwa Chadema ni chama imara kwa kuwa kina viongozi waadilifu ambao wako tayari kubuni mikakati mbalimbali kwa ajili ya kuwaletea wananchi maendeleo.
Mtei alisema kitendo cha CCM kuwachukulia hatua watuhumiwa wa ufisadi ikiwa ni pamoja na kuwapa siku 90 wanaweza kutimkia vyama vya siasa huku akisisitiza kuwa Chadema haitakuwa tayari kuwapokea.
"Chadema hakiwezi kukubali watuhumiwa wa ufisadi, yaani Watanzania wanataka wahukumiwe kwa ufisadi wao leo hii Chadema tuwapokee, hakuna kitu kama hicho, Watanzania wako wengi sana na wanaoingia Chadema wapo pia ila kwa watuhumiwa wa ufisadi hapana, haiwezekani,"alisisitiza