Nimemesoma kwa masikitiko makubwa kuwa wananchi wa monduli wataendelea kumchagua lowasa kwa sababu amewaletea maendeleo makubwa katika jimbo lake. Kwa mtazamo wangu naona hii inaonyesha jinsi watanzania tusivyojali umoja na uzalendo wetu wa kuipenda tanzania. Pia niliwahi kusema katika moja ya post zangu kuwa tatizo kubwa ninaloliona tanzania ni 'ubinafsi(umimi)'. wamasai wameshindwa kuona hasara aliyoleta lowasa kwa taifa? wao wanachoona amewafanyia nini watu wa jimbo lake, Basil mramba ufisadi uko wazi kabisa lakini watu wa Rombo wameshindwa kuona hasara aliyoileta kwa taifa bali wanachojali ni nini amekifanya Rombo. Kwa rostam aziz hasara aliyoleta kwa taifa letu iko wazi kabisa, lakini watu wa jimbo lake hiyo hasara ya taifa haiwahusu? ,kinachowahusu ni amefanya nini katika jimbo lake! TABIA HII YA WATANZANIA NDO INAWAPA OPPORTUNITY VIONGOZI KUFUJA MALI YA UMMA NA KUFANYA WATAKAVYO (katiba pia ina changia) kwa sababu wanajua udhaifu wetu. na wakirundi majimboni mwao wanaweka mambo sawa. WATANZANIA HIKI NI KIPINDI CHA KULIKOMBOA TAIFA