"CCM imevaa nepi halafu inajisifia"- Mzee wa Upako-Lusekelo

Sijui ugumu wa kuelewa unatoka wapi?
Mch. Lusekelo amesema kuwa CCM imevaa NEPI halafu inajisifia. Sasa humu ndani watu badala ya kujadili hiyo hoja wanamshambulia Mchungaji.

Ni matarajio ya wafikirifu makini kuona kuwa baada ya pastor kusema hayo yangetokea makundi mawili: Moja likiwa linaona kuwa maneno hayo ni ya KWELI na hapo wangeyatumia hata kufukia kutoa maoni namna ya kuikomboa Tanzania dhidi ya mfubao huo. Kundi la pili lingekuwa lile linaloona kuwa maneno hayo ni UONGO. Hawa wangeleta hoja za kuthibitisha kuwa kwa miaka 50 ya uhuru Tanzania imepiga hatua kubwa kama ilivyotarajiwa na au zaidi.

Kimenishangaza tu kwamba hapa katika jukwaa la wafikirifu makini badala ya hoja kujadiliwa wametokea wachangiaji ambao hawataki kujadili hoja hizi bali wanaanza kumshambulia mtoa hoja.

Nitoe tu taarifa kidogo kuhusu WACHUNGAJI WANAOTUMIA MUDA MWINGI KUPAMBANA NA SHETANI. Wachungaji hawa wana utamaduni wa kutangaza ukuu wa MUNGU na ubaya wa SHETANI.

Wanapomwelezea MUNGU wanajaa TABASAMU na UKARIMU mkubwa. Lakini wanapomkemea SHETANI wanakuwa wakali sana na hutoa sauti kubwa. Ni imani ya wengi kwamba huwezi kumhubiri MUNGU usimkemee SHETANI. Na huwezi kumkemea shetani kistaarabu au kiupole. Lazima utumie MAMLAKA.
 
Ni kweli CCM wamevaa nepi na serikali yao. Miaka ya 1970-74 trekta la kilimo liliuzwa TSh. laki moja leo ni TSh. Milioni 38.
 
Mzee wa upako aache kutumia lugha ya uchochezi,maana waumini wake wanaweza kugawanyika ndani ya kanisa.hata kama viongozi wa dini watakiwa kuikosoa serikali yetu wanapaswa kutumia lugha ya staha ingawa itakuwa ina uma kwa viongozi walioko madarakani.

Kwa uhalisia Mzee wa Upako ametumia lugha ya staha na kiungwana mno, kwani kuna dhambi gani kusema ukweli? Kama mtu mzima "anatembea uchi" hakuna haja ya kusema "hajavaa nguo" ni kusema wazi ili message ifike ajirekebishe. Mzee wa Upako rusha kombola jingine labda watasikia!
 
Mzee wa upako aache kutumia lugha ya uchochezi,maana waumini wake wanaweza kugawanyika ndani ya kanisa.hata kama viongozi wa dini watakiwa kuikosoa serikali yetu wanapaswa kutumia lugha ya staha ingawa itakuwa ina uma kwa viongozi walioko madarakani.

Acha woga mgawanyiko umeanza siku nyingi magamba wenyewe wamegawanyika sembuse waumini
 
Siwezi kushangaa kwa hawa wachungaji wa sasa ambao dini leo imekua pazia ili nyuma yake warahisishe maslah yao kwa siri,leo wachungaji ndio wauza unga wakubwa,wachungaji leo wanawania nyazifa mbalimbali ktk siasa,kiukweli jamaa hana jipya!

....Hizi zote ni dalili za massage sent and delivered. mfano murua ambao hata mtoto mdogo anauelewa, I am sure Roho mtakatifu alimuongoza kutoa message hii, maana imanikumbusha mifano ya Nyerere.
 
Akihojiwa huhusu mafanikio ya CCM katika miaka 50 iliyopita Mchungaji Lusekelo Mzee wa Upako amesema:"Yaani ni sawa na mtu mzima kuvaa nepi; ndiyo nepi ni nguo lakini mtu mzima akivaa nepi anakuwa kichekesho. Haya wanayodai kwamba ni maendeleo ni sawa na mtu mzima kuvaa nepi halafu akaanza kujisifia" mwisho wa nukuu Gazeti la NYAKATI jumapili Octoba 30- Novemba 5 -2011. Pamoja na kwamba mimi si mshabiki au mojawapo wa kondoo wa Mzee wa Upako naona angalizo lake hili kuhusu miaka 50 ya CCM ni chakula cha vichwa(food for thought?) vya wachambuzi hapa JF. Karibuni!

Yupo sasa mia kwa mia, tena nep yenye mav
 
Hapa hoja ni ulinganifu wa umri wa nchi na maendeleo! Nepi si vazi baya! tatizo ni kwa mvaaji! Je maendeleo yetu yanafanana na huo umri wa miaka 50? Ni aibu hata kufanya ulinganifu!
 
Dubu miaka 50 ni toka TANU baba yake CCM ni aibu Kwa muda wote huo wananchi wako in masikini
 
Back
Top Bottom