Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
CCM ILIVYO SASA HAIOKOLEKI (MwanaHalisi)
Na. M. M. Mwanakijiji
Kuna watu ambao kwa makosa ya fikra zao na kiburi cha utamu wa madaraka na hasa wale waliopigwa ganzi ya ufisadi wanaamini katika mioyo yao kuwa CCM itadumu milele. Hawa pamoja na vikaragosi wengine wa ufisadi wamejiaminisha katika upotofu wao kuwa Chama hiki cha Mapinduzi kitatawala milele, kitadumu milele na kitaendelea kuwa kama kilivyo sasa milele. Hawa ni wa kuwekewa mikono na ikibidi kupepewa huku wanavutwa masikio.
Leo niendelee kuwa mjumbe wa habari mbaya. CCM ni mazao ya binadamu; ni chombo kilichoundwa na wanadamu, kimeongozwa na kinaongozwa na binadamu na kutokana hilo tu peke yake CCM inakuwa ni chombo kinachoweza kuharibika, kuvunjika, kuporomoka na kwa hakika kabisa chaweza kuzama. Hakuna ustadi wa mwanadamu unaoweza kufanya kazi zake zisiwe na makosa milele. Katika uelewa wetu huu mdogo wa kibinadamu ni kazi za Mungu tu ambazo hazina makosa.
Hivyo ninaposikia mtu anasema kwamba hakuna ufisadi ndani ya CCM ninamshangaa. Nikimsikia mtu anasema CCM ni safi ninamtumbulia macho kama mjusi aliyekoswakoswa na mlango. Na pale ninaposikia kuna wana propaganda wa CCM ambao wanaitetea CCM kuwa ni chama safi na kina mafisadi wanne tu ninafumba macho yangu kwa mshtuko na kama ningekuwa karibu ningemtundika konzi mtu huyo kumgutusha kutoka katika usingizi wake uliochanganyika na ulevi wa madaraka.
Malumbano tunayoyasikia sasa na kugongana kunakoendelea hivi sasa ndani ya CCM na tutashuhudia zaidi miezi michache ijayo kunatoa ushahidi wa jambo moja kubwa kuwa CCM iko matatani na hakuna mtu wa kuiokoa. CCM haiokoleki.
Jipatie nakala yako hapa chini na isambazwe!!!
Baadhi ya maoni niliyoyapokea tangu makala itoke leo:
Na. M. M. Mwanakijiji
Kuna watu ambao kwa makosa ya fikra zao na kiburi cha utamu wa madaraka na hasa wale waliopigwa ganzi ya ufisadi wanaamini katika mioyo yao kuwa CCM itadumu milele. Hawa pamoja na vikaragosi wengine wa ufisadi wamejiaminisha katika upotofu wao kuwa Chama hiki cha Mapinduzi kitatawala milele, kitadumu milele na kitaendelea kuwa kama kilivyo sasa milele. Hawa ni wa kuwekewa mikono na ikibidi kupepewa huku wanavutwa masikio.
Leo niendelee kuwa mjumbe wa habari mbaya. CCM ni mazao ya binadamu; ni chombo kilichoundwa na wanadamu, kimeongozwa na kinaongozwa na binadamu na kutokana hilo tu peke yake CCM inakuwa ni chombo kinachoweza kuharibika, kuvunjika, kuporomoka na kwa hakika kabisa chaweza kuzama. Hakuna ustadi wa mwanadamu unaoweza kufanya kazi zake zisiwe na makosa milele. Katika uelewa wetu huu mdogo wa kibinadamu ni kazi za Mungu tu ambazo hazina makosa.
Hivyo ninaposikia mtu anasema kwamba hakuna ufisadi ndani ya CCM ninamshangaa. Nikimsikia mtu anasema CCM ni safi ninamtumbulia macho kama mjusi aliyekoswakoswa na mlango. Na pale ninaposikia kuna wana propaganda wa CCM ambao wanaitetea CCM kuwa ni chama safi na kina mafisadi wanne tu ninafumba macho yangu kwa mshtuko na kama ningekuwa karibu ningemtundika konzi mtu huyo kumgutusha kutoka katika usingizi wake uliochanganyika na ulevi wa madaraka.
Malumbano tunayoyasikia sasa na kugongana kunakoendelea hivi sasa ndani ya CCM na tutashuhudia zaidi miezi michache ijayo kunatoa ushahidi wa jambo moja kubwa kuwa CCM iko matatani na hakuna mtu wa kuiokoa. CCM haiokoleki.
Jipatie nakala yako hapa chini na isambazwe!!!
Baadhi ya maoni niliyoyapokea tangu makala itoke leo:
Kwanza naomba nikujulishe kuwa nimekuwa sio mpenzi sana wa makala zako hadi pale ulipotoa taarifa hivi karibuni kwenye mtandao kuhusu MEREMETA. Sasa ninajisikia kutaka kusoma kila unachokiandika, na ikiwa utaanzisha namna nzuri ya kukuwezesha huenda nikafikiria kukuchangia japo kwa kiwango cha dola moja kama alivyofanyiwa Rais wa Marekani Barak Hussein Obama.
Kwa nini? Kwa sababu katika hoja ya MEREMETA umejipambanua kwangu haswa wewe ni nani na unasimamia nini. Nilidhani wewe una dira, dhamira na falsafa katika maisha, na inayojishikiza na Chama kimojawapo cha siasa hapa Tanzania, kumbe hapana. Wewe ni sawa na wengine wanaofanya kazi ya kulitumikia Taifa hili changa linalohitaji mchango wa kila mmoja wetu katika kufikia ile Tanzania yenye asali tele inayotosha kwa kila mmoja wetu kuilamba. BRAVO! - Ngonyani
Nimesoma makala yako leo kuhusu CCM haiwezi kuokoleka,
Umewataja wanasiasa wengi wote wa ngazi za juu ila nashangaa
hukumtaja Dr. Shein Makamu wa Rais huyu ni muhimu kwa Bara na
Muungano. Sijui kwa nini labda una makusudi yako.
Bado nakuunga mkono kwenye harakati za Ukombozi wa nchi yetu na
Bara letu kwa Ujumla. Tunakuombe Mungu akutie Nguvu kwenye hii
vita ya Ufisadi tuweze kusonga mbele na kizazi kijacho. - Mage