Ehud
JF-Expert Member
- Feb 12, 2008
- 2,685
- 337
Baada ya kutafakari sana yanayojiri nchini nimegundua matatizo mengi yanayoikumba nchi yetu ya Tanzania kwa sasa kwa namna moja ama nyingine yametokana na CCM. Hii ni kutokana na ukweli kuwa viongozi wote waliolifisidi/wanaolifisidi taifa kama vile JK,EL,RA,Mramba,Mkapa,Karamagi, n.k ama wametokana na CCM au ni watu waliotufikisha hapa tulipo kwa kupitia mgongo wa CCM.
Ikumbukwe kuwa CCM ilikuwa na ahadi zake nzuri tu kama vile "rushwa kwangu ni mwiko sitapokea wala kutoa rushwa" na pia chama hicho hapo kale kilijikita kwenye kusaidia wananchi lakini kwa sasa kipo zaidi kusaidia wezi wa mali ya umma na wawekezaji wa kigeni hivyo kwa mtaji huu chama hiki kimepoteza sifa zote za kuiongoza nchi yetu ya Tanzania na hivyo wakati umefika wa kukifuta ili tuanze upya kabisa bila chembe chembe za u-ccm. Nawakilisha
Ikumbukwe kuwa CCM ilikuwa na ahadi zake nzuri tu kama vile "rushwa kwangu ni mwiko sitapokea wala kutoa rushwa" na pia chama hicho hapo kale kilijikita kwenye kusaidia wananchi lakini kwa sasa kipo zaidi kusaidia wezi wa mali ya umma na wawekezaji wa kigeni hivyo kwa mtaji huu chama hiki kimepoteza sifa zote za kuiongoza nchi yetu ya Tanzania na hivyo wakati umefika wa kukifuta ili tuanze upya kabisa bila chembe chembe za u-ccm. Nawakilisha