Elections 2010 CCM ifungue kesi ya Kikatiba dhidi ya CHADEMA kuwalazimisha kutambua matokeo!

subutuuuu, CCM hawawezi kwenda mahakamani, waende wajikaange kwa mafuta yao wenyewe? subutu
 
Kwa ufupi naamini CCM wanaweza kutoa mfano wa utawala wa sheria kwa kwenda mahakamani kufungua kesi hizo za Kikatiba.[/QUOTE]

Mwanakijiji umechoka hata fikra za kisheria na maadili
 
Thubutu! Waende mahakamani wakaumbuke?

Wataendelea kupiga kelele kwa propaganda na au kupitia bunge ambako wako wengi, wanaweza hata kubadirisha kanuni ili kulitekeleza hili.

Hawawezi kamwe kwenda mahakamani kwani mahakamani hakuna porojo, kule wanataka facts na CCM wanajua ukweli wataumbuka kwani CHADEMA watatoa facts
 
Nilikuwa nafikiria namna nyingine ya kutatua mgogoro uliopo sasa hivi kati ya CCM na CHADEMA kuhusu suala la matokeo ya Urais. Nimefikiria kuna kesi mbili ambazo nikiwasikiliza CCM na wale wenye kulaani kitendo cha "kutoka nje" kilichofanywa na CHADEMA wanaweza kuja nazo.


1. Kesi ya Kikatiba ya kuwalazimisha CHADEMA kumtambua Rais Kikwete kwa vile waliamua kutoka wakati Rais ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu na Mkuu wa serikali ya JMT alipokuwa anazungumza. Kwa vile kitendo kile kimeelezewa na Kapt. Chiligati kuwa kilikuwa kinavunja Katiba basi mantiki inataka wale wanaotetea Katiba wachukue hatua za kuitetea Katiba hiyo kwa kufungua kesi ya Kikatiba dhidi ya CHADEMA.

2. Kesi ya pili nayo ni ya Kikatiba vile vile nayo iwe ni ya kulazimisha CHADEMA WATAMBUE matokeo ya Uchaguzi wa Rais kwani kutokutambua matokeo ya kura za Urais yanatuleta kwenye tatizo la kwanza hapo juu. Kwa vile CCM na wengine wanaamini kuwa kura zilizopigwa na kutangazwa zilikuwa ni halali na hakuna mashaka yoyote basi jawabu pekee ni kuwalazimisha CHADEMA KUKUBALI matokeo hayo. Katiba inazuia kuhoji kutangazwa kwa Rais lakini HAKUZUII kutetea kutangazwa huko mahakamani! Hivyo, CCM na wanasheria wake wafikirie namna ya kuthibitisha au kuutetea ushindi mahakamani. Hapa napendekeza wao CCM waitishe kura zote za Urais kutoka majimbo yote ili kuonesha kiasi cha kura alizoshinda. Watakapofanya hivyo watafunga kelele zote za Chadema na kuwaridhisha Watanzania kuwa hakuna kura zilizochakachuliwa. Hapa itakuwa ni goli kama la Maradona au lile goli la elfu moja la Pele.

Kwa ufupi naamini CCM wanaweza kutoa mfano wa utawala wa sheria kwa kwenda mahakamani kufungua kesi hizo za Kikatiba.

CCM hawawezi kufanya hivyo kwa sababu that is a scientific evidance. Evidance zilizopo zikiwasilishwa hazitasupport matakeo yaliyotangazwa na tume. So hawawezi.

na kuhusu kesi hizo ulizosema, ingekuwa inawezekana wangeanza na kesi namba 2 ili namba moja iweze kufanywa. ki ukweli, Demkkrasia ilibakwa na CCM. wao wataishia kulalamika lakini suala ambalo linahiyaji evidance, CCM hawalitaki.

Cheers CHADEMA. Evidance based political party...
 
Naomba nieleweke kwa yafuatayo:
1.CHADEMA KUTOMTAMBUA RAIS KIKWETE
Kwa hili naona halijaeleweka sawia,kwanza hoja ya msingi ya CHADEMA siyo kutomtambua rais
Bali ni kutokubali matokeo yaliyomuweka rais huyo madarakani.Ikumbukwe kuwa hoja hii ililetwa siku ya tatu ya kutangaza matokeo ambapo mgombea urais Kupitia CHADEMA mh.Slaa aliitaka tume kusitisha utangazaji wa matokeo hayo,kama kweli NEC ingekuwa tume ya haki kwa vyama vyote ingekubali kupitia kwa makini hoja ya mh.Slaa Kabla ya kumtangaza mshindi wa urais.Hapo ndipo ugomvi wa kikatiba unapoibuka.Kwa katiba ya sasa Mshindi wa urais hawezi kutenguliwa baada ya kuapishwa.Swali ni je kwanini hoja ya Slaa ilipuuzwa ilhali vielelezo muhimu alikuwa navyo kabla?

2.KUTOKA NJE YA BUNGE
Hili vyombo vingi vya habari vimeandika kuwa CHADEMA imemsusa rais kwa tafsiri ya kuwa haimtambui.Mwenyekiti wa taifa wa CHADEMA ambaye ndiye kiongozi mkuu wa upinzani mh.Freeman Mbowe amelitolea maelezo kuwa ni shinikizo la kuvunja tume ya sasa ya uchaguzi na kuundwa kwa tume mpya ambayo itakuwa inajiendesha kwa uhuru na kwa haki kwa chaguzi zijazo na katiba mpya,tume ya sasa chini ya Lewis Makame iliundwa kwa parliamentary act ya mwaka 1971 ambayo inafuata mfumo wa chama kimoja cha siasa ndo maana tumeyaona yaliyotokea kwenye uchaguzi wa oct 31

CHADEMA ni chama kinachopigania maslahi ya wengi na ikiwa mapendekezo yake yatazingatiwa yatakuwa na faida si tu kwake bali kwa vyama vingine vya upinzani ambavyo kweli vipo kwa ajili ya upinzani na kwa maslahi ya wananchi na si kwa maslahi ya chama tawala.:target:
 
Hiyo kesi itakuwa based kwenye vifungu vipi kwenye katiba? au ni kwa vile tukiandika kuvunja katiba inaleta mvuto?
 
Tatizo Mzee Mwanakijiji.................Mahakama hazina mamlaka ya kisheria kuingilia majukumu ya NEC yakiwemo kumtangaza Raisi aliyeshinda.........hivyo kwa mantiki hiyo mahakama haiwezi kupokea migogoro itokanayo na maamuzi ya NEC yawe ni kutambua au hata kutotambua maamuzi ya NEC kuhusiana na uraisi............................kwa hiyo hayo yote uliyoyandika hapo juu hayatekelezeki kwa maana ya kisheria...................................

lakini ipo sababu nyingine kwa nini CCM haina sababu ya kuumiza kichwa na kelele za Chadema...........................ni kuwa Chadema wamkubali au wamkatae JK bila ya kwenda mahakamani ni sawsawa kabisa na kutwanga maji kwenye kinu.............................CCM wao watakaa kimya na kuvuta pumzi tu hawana jingine la kufanya................................

Chadema kama wana ushahidi wa kuwa NEC ilikiuka taratibu za kisheria katika kumtangaza JK na ushahidi wanao basi itabidi watinge mahakamani na vinginevyo hizo purukshani nyingine ni ubabaishaji tu...mwaka 1995 mahakama hiyo hiyo ilikwisha sema pamoja na Ibara ya katiba inayokataza kuchunguza matokeo yaliyotangazwa na NEC lakini mahakama yaweza kuichunguza NEC kama ilifuata sheria katika kumtangaza aliyeshinda Uraisi................
Umelewa pingu!!!!
 
Mzee Mwanakijiji,

Sidhani hatua kama hiyo, itasaidia kulimaliza tatizo la uchakachuaji wa kura unaodaiwa kufanyika wakati wa uchaguzi mkuu uliopita. Kama unavyofahamu, kisheria, 'he who asserts must prove' (tuseme anaye hakikisha, athibitishe).

Kwa hiyo, chini ya principle hii, utakuta kwamba CHADEMA (na wale wote wanaoamini uchakachuaji wa kura ulifanyika), wanaweza kutakiwa na Mahakama kuthibitisha kwamba, kweli CCM ilifanya hivyo i.e. ilichakachua kura; lakini hailekei CCM yenyewe, inaweza kutakiwa na Mahakama ithibitishe 'ushindi' wake, kwa kuwa haiupingi.

Lakini pamoja na hayo, ukweli ni kwamba kura zilihesabiwa na Tume ya Uchaguzi ambayo iliteuliwa na CCM, na wala hakuna hata mjumbe yeyote kutoka kambi ya upinzani (achilia mbali CHADEMA), aliyekuwepo wakati wa zoezi hilo.

Hii ina maana kwamba ni CCM, pamoja na taasisi zake, zinazohifadhi kumbukumbu muhimu ambazo CHADEMA ingelizihitaji kuthibitisha Mahakamani, uchakachuaji wa kura unaodaiwa.

Aidha, itakuwa ni juu ya CHADEMA kuiomba Mahakama iilazimishe serikali ya CCM kuzitoa takwimu hizo, ili CHADEMA iweze kuthibitisha kesi yake mbele ya Mahakama.

CHADEMA inaweza kuiomba Mahakama kuitaka serikali kufanya hivyo, kwa kuonyesha kwamba, swala zima, ni muhimu kufahamika vyema na kupata suluhu, kwa manufaa ya Taifa (public interest).

Vinginevyo, CCM inaweza kwenda mahakamani kudai CHADEMA, na wafuasi wake, wamtambue Rais aliyetangazwa na Tume ya Uchaguzi kuwa ni mshindi halali.

Lakini, amri kama hiyo, haiwezi peke yake kubadili hisia zilizokwisha jengeka katika mioyo ya baadhi ya wananchi kwamba kweli uchakachuaji wa kura ulitokea.

Kwa kukazia, hazipo nguvu za dola zinazoweza kubadili kilichomo mioyoni mwa baadhi ya wananchi wake, bali kujenga misingi mizuri, ya pande-husika kuaminiana.

Ni dhahiri kwamba msingi wa tatizo lenyewe, ni katiba ya Jamhuri ya Muungano. Katiba hii, haiwahami vya kutosha wanasiasa kutoka kambi ya upinzani. Isitoshe, ilitungwa muda mrefu, enzi za chama kimoja; na ina viraka vingi mno, vinavyokipa Chama-tawala upendeleo, kwa gharama za siasa za wakati huu i.e. za ushindani.

Nje ya hayo, katiba hii haitilii maanani mabadiliko ya kisiasa, na ya kijamii, yaliyotokea (na yanayoendelea kutokea) katika jamii yetu. La zaidi, ni katiba isiyotilia maanani kutokuwepo usawa (kikatiba) kati ya wananchi na Taifa lao (unequal power relationship between the State and its citizens). Bila ya kulishughulikia tatizo la katiba hii, serikali itaendelea kukumbana na matatizo (au malalamiko) ya namna hii, kila wakati.

Kwa upande mwingine, kama serikali itaendelea kupuuza malalamiko ya wananchi; malalamiko ambayo yanayotokona na dosari za katiba hii; inaweza kutafsiriwa na baadhi ya wananchi kwamba, serikali inafanya hivyo, maksudi, ili iendelee kuyahami maslahi ya wateule wachache, miongoni mwake.

Pamoja na kuwepo ushahidi unaoonyesha kwamba serikali ya Rais Kikwete, huko nyuma, ilishindwa kuzichukulia hatua nguvu zilizolihujumu, kiuchumi, Taifa analoliongoza, sidhani kwamba (Rais Kikwete) angelipenda kujenga, kuimarisha, na, au kuendeleza hisia hizi, miongoni mwa wananchi wake.
 
Naomba tuungane kutaka CCM ifungue kesi ya kuwalazimisha CHADEMA kutambua matokeo.. na kumtambua Kikwete.. lets join hands wale wote tunaotaka utawala wa sheria na ambao tunaamini kitendo cha Chadema kutoka Bungeni hakikuwa sahihi..

hawatakubali kujitia kitanzi ..
 
Mkuu ccm hawawezi, we fikiria badala ya kufikiria kuanza mchakato wa kubadili katiba na kuleta uwezekano wa kuhesabiwa upya kura za urais, wao wanataka chadema wafukuzwe mjengoni na wanasahau kuwa wabunge wa chadema kama wao waliochaguliwa kihalali wamepekekwa na wananchi na kuwafukuza mjengoni ni kuwafukuza vilevile wananchi wao. Bongo haiwezi kuendelea as long as ccm wanabaki madarakani!
 
Nilikuwa nafikiria namna nyingine ya kutatua mgogoro uliopo sasa hivi kati ya CCM na CHADEMA kuhusu suala la matokeo ya Urais. Nimefikiria kuna kesi mbili ambazo nikiwasikiliza CCM na wale wenye kulaani kitendo cha "kutoka nje" kilichofanywa na CHADEMA wanaweza kuja nazo.


1. Kesi ya Kikatiba ya kuwalazimisha CHADEMA kumtambua Rais Kikwete kwa vile waliamua kutoka wakati Rais ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu na Mkuu wa serikali ya JMT alipokuwa anazungumza. Kwa vile kitendo kile kimeelezewa na Kapt. Chiligati kuwa kilikuwa kinavunja Katiba basi mantiki inataka wale wanaotetea Katiba wachukue hatua za kuitetea Katiba hiyo kwa kufungua kesi ya Kikatiba dhidi ya CHADEMA.

2. Kesi ya pili nayo ni ya Kikatiba vile vile nayo iwe ni ya kulazimisha CHADEMA WATAMBUE matokeo ya Uchaguzi wa Rais kwani kutokutambua matokeo ya kura za Urais yanatuleta kwenye tatizo la kwanza hapo juu. Kwa vile CCM na wengine wanaamini kuwa kura zilizopigwa na kutangazwa zilikuwa ni halali na hakuna mashaka yoyote basi jawabu pekee ni kuwalazimisha CHADEMA KUKUBALI matokeo hayo. Katiba inazuia kuhoji kutangazwa kwa Rais lakini HAKUZUII kutetea kutangazwa huko mahakamani! Hivyo, CCM na wanasheria wake wafikirie namna ya kuthibitisha au kuutetea ushindi mahakamani. Hapa napendekeza wao CCM waitishe kura zote za Urais kutoka majimbo yote ili kuonesha kiasi cha kura alizoshinda. Watakapofanya hivyo watafunga kelele zote za Chadema na kuwaridhisha Watanzania kuwa hakuna kura zilizochakachuliwa. Hapa itakuwa ni goli kama la Maradona au lile goli la elfu moja la Pele.

Kwa ufupi naamini CCM wanaweza kutoa mfano wa utawala wa sheria kwa kwenda mahakamani kufungua kesi hizo za Kikatiba.


Viongozi wa Chama Cha Majambazi wakiongozwa na Mwizi mkuu pamoja na huyo Chiligati si waliapa kuitetea katiba ya JMT hebu tuone sasa kama kweli wanaweza kuitetea hii katiba si wamesema Chadema wameivunja?
 
Tuungane kutaka CCM ambao wanaona kitendo cha CHadema kimevunja Katiba (kama alivyosema Chiligati) na kuwa kina makosa makubwa ya kustahili kuwafukuza Bungeni wabunge wa Chadema waende mahakamani kuwalazimisha Chadema kutambua matokeo na Rais. Mbona wote mnasema "haiwezekani"? grrrrrrrrrrrrr tuwasihi CCM waende mahakamani kuonesha utawala wa Sheria na Katiba.. Remember hawaendi "kuhoji" matokeo (kama Katiba inavyokataza) bali kulazimisha Chadema watambue matokeo na kumtambua Rais. Huu si mtego jamani.
 
Naomba tuungane kutaka CCM ifungue kesi ya kuwalazimisha CHADEMA kutambua matokeo.. na kumtambua Kikwete.. lets join hands wale wote tunaotaka utawala wa sheria na ambao tunaamini kitendo cha Chadema kutoka Bungeni hakikuwa sahihi..
Hakuna Kesi Hapo na Hata hao CCM wanajua na wala vichwa haviwagongi.Kwani hii ni nusu mchezo CUF Waliweka full nondo na mwisho wa yote walisalimu amri.Kama CDM Wanafikiri katiba mpya italetwa kwa Drama za unaharakati wanapoteza wakati wakae chini na wazumgumze kwa kuwakilisha hoja na kufanya ushawishi wa kihoja ili hoja zao zikubalike iwe kitaifa kwa kutumia vyombo husika au kimataifa kwa kutumia jumuiya za kimataifa.Vinginevyo CCM Wanawalia timing tu....................!
 
KNKU.. hii timing ni kwa sababu Chadema wamefanya makosa ya Kikatiba aliyosema Chiligati? au alichosema Chiligati hakikuwa ni msimamo wa Chama?
 
CCM wakifanikiwa kunishawishi kwamba Baba Ridhiwani alishinda kihalali nitawalaumu sana wabunge wa CHADEMA kwa kumdharau Rais
 
Back
Top Bottom