Bado naikumbuka ccm ya Mwl. Nyerere; wakati ule chama kilikuwa na maadili na miiko ya uongozi. Chama hakikuwa sahihi 100% lakini angalau kilikuwa kikimjali kila mtanzania. Wengi tulitegemea ccm kingemuendeleza mtanzania hasa kwenye kipindi hiki cha vyama vingi, leo hii chama kimegeuka kama club ya wahuni watupu, viongozi tulio nao wapo mstari wa mbele kwenye kuliangamiza taifa letu, kila kukicha kashfa, sijui ni kiongozi yupi kumuamini; cha ajabu viongozi hao wamekuwa mstari wa mbele kukanusha hata mambo ambayo ni dhahiri, hebu wana ccm tuliangalie hili jipya la Bw. Kinana, maishani mwangu sijasikia hata siku moja mchaga wala muhaya wakawinda tembo, siku zote wawindaji haramu ni wasomali haya unganisha hesabu hapo, wawindaji haramu wasomali, Kinana msomali halafu mtu Kinana leo hii anakataa kwamba hajui mzigo aliokuwa anasafirisha? Kweli watanzania tumekuwa mbumbu lakini haya mengine hebu tuyaangalie kwa makini nadhani wakati ccm tumekuwa mstari wa mbele kuwa wapinzani yupi ni raia au si raia hebu tujichunguze wenyewe kwa maslahi ya taifa letu.