nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Wednesday, 01 June 2011 12:45 newsroom
NA MWANDISHI WETU
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeelezea kusikitishwa kwakwe na tuhuma zinazotolewa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Tundu Lissu kwamba imehusika katika mauaji ya wananchi katika mgodi wa Nyamongo, Tarime. Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana, ilisema kuwa CCM haihusiki kwa namna yoyote na mauaji hayo na kwamba habari zilizoandikwa na gazeti la Tanzania Daima la Mei 30, mwaka huu, ni uzushi. "Tuhuma hizi ni nzito na za kusikitisha, lakini zinastahili kupuuzwa na wananchi wenye akili timamu, kwani mtoa habari hizo siku zote amekuwa ni mwongo," ilisema taarifa hiyo iliyotiwa saini na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Propaganda cha CCM, Richard Tambwe.
Tambwe alisema CCM kwa muda mrefu imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha nchi inakuwa na amani na imekuwa ikifanya hivyo kabla CHADEMA haijaanzishwa, lakini ni mambo ya kusikitisha kuona kuwa chama hicho ndicho kimekuwa kikichangia kubomoa hali ya amani na utulivu uliopo.
Alisema Lissu amekuwa akitumia maneno ya uchochezi kwa sababu za kisiasa kwa nia ya kutaka kuungwa mkono na wananchi.
Aliliomba Jeshi la Polisi nchini kuendelea kuwatafuta wote walioshiriki kwa njia moja au nyingine katika tukio la Tarime, wakiwemo viongozi ambao wamekuwa wachochezi.
Tambwe aliwakumbusha wananchi kuwa serikali iliyopo madarakani imetokana na CCM, ambayo ilishinda baada ya wananchi kuonyesha imani kwa Chama.
NA MWANDISHI WETU
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeelezea kusikitishwa kwakwe na tuhuma zinazotolewa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Tundu Lissu kwamba imehusika katika mauaji ya wananchi katika mgodi wa Nyamongo, Tarime. Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana, ilisema kuwa CCM haihusiki kwa namna yoyote na mauaji hayo na kwamba habari zilizoandikwa na gazeti la Tanzania Daima la Mei 30, mwaka huu, ni uzushi. "Tuhuma hizi ni nzito na za kusikitisha, lakini zinastahili kupuuzwa na wananchi wenye akili timamu, kwani mtoa habari hizo siku zote amekuwa ni mwongo," ilisema taarifa hiyo iliyotiwa saini na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Propaganda cha CCM, Richard Tambwe.
Tambwe alisema CCM kwa muda mrefu imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha nchi inakuwa na amani na imekuwa ikifanya hivyo kabla CHADEMA haijaanzishwa, lakini ni mambo ya kusikitisha kuona kuwa chama hicho ndicho kimekuwa kikichangia kubomoa hali ya amani na utulivu uliopo.
Alisema Lissu amekuwa akitumia maneno ya uchochezi kwa sababu za kisiasa kwa nia ya kutaka kuungwa mkono na wananchi.
Aliliomba Jeshi la Polisi nchini kuendelea kuwatafuta wote walioshiriki kwa njia moja au nyingine katika tukio la Tarime, wakiwemo viongozi ambao wamekuwa wachochezi.
Tambwe aliwakumbusha wananchi kuwa serikali iliyopo madarakani imetokana na CCM, ambayo ilishinda baada ya wananchi kuonyesha imani kwa Chama.