CCM: Dharura Kamati Kuu & NEC, Kuna Nini Huko?

Watu hatutakuwa wapumbavu milele,taratibu mambo tutayabadilisha then CCM nje kabisa. Kwani KANU walitegemea kwamba wangepigwa chini Kenya?!
 
Wildcard mkuu heshima mbele.

Kutawaliwa na CCM si kitu cha kushangilia hata kidogo, Hawa jamaa wote isipokuwa mmoja wanaangalia masilah yao na watoto wao tu na hawana kazi nyingine. Nchi yetu hali ni mbaya ukiangalia kwenye viashiria vyote vya Taifa Imara. Inflation 12% Ndullu yupo tu, Ada za shule za watoto wetu tunatakiwa kulipa kwa dola ( kama vile tuko marekani) wakati mishahara yetu ni kwa Shilingi. Malalamiko kila kona, ujambazi umeongezeka mwingine unawahusisha mapolisi (mfano ukerewe), ajali za barabarani zinaongezeka kila kukicha, wizi wa mali ya umma, Raisi kudanganywa hadharani kila siku (mfano Ufunguzi wa hoteli-Arusha, Kukabidhi Gari Ikulu, Uzinduzi wa malaria basi-THT na sasa Udanganyifu kwenye sheria iliyopitishwa na bunge). Raisi anatokea hadharani kwa mbwembwe kwa issue ambayo baadae inaonekana ni usanii mtupu.

Wildcard haya yote hayana wa kuyaongoza, kuelekeza, au kusimamia sheria. CCM ni kiama chetu sote Tunaoipenda na Tunaoichukia. usishangilie hata kidogo.
 
Mkuu amefadhaishwa sana na vijana na baadhi yetu hapa jf kujitafutia uongozi kwa gharama ya jina na mgongo wake. Acha ashughulike na wanachama wake, awaweke kwenye line, makatibu wa wilaya wengi wako kwenye mifuko ya wenye mapesa hivyo ni tishio kwa wagombea wengine ambao wana cha mboga tena cha familia tu.
 
- The dataz ni kwamba wiki nzima hii Muungwana amekuwa akifanyia kazi Lumumba na bila kusema na mtu, ndio maana tunasema kuna jambo huko linakuja, au?

Respect.

FMEs!

Ni kweli ikifika jioni ile barabara ya Lumumba inafungwa Muungwana yupo ndani busy anakula mzigo ndani.
Siasa za bongo maana zinachekesha sana.
 
teh! hivi, unapokuwa na washauri ambao baba zao wanadiriki kusema kwamba wakiachia ngazi watoto wao ambao ni washauri wa mkuu watashika hatamu, pamoja na mambo ya kuacha kazi walizopangiwa na mkuu na kuanza kufanya kazi za tenda, je, kuna usalama hapo? hata mkuu anaona jinsi anavyohujumiwa. ila cha kushangaza sasa ni jinsi anavyo lalamika utafikiri hana madaraka ya kuwaachisha kazi!!! urafiki huo!
labda hivi vikao ni sakata aliloibua dr. slaa la kuongezwa kwa vipengele kwenye dokumenti alizosaini bw. mkubwa (bila wasaidizi wake kuzipitia kwanza) na na lile la uzinduzi wa malaria haikubaliki!!!
kazi kwetu!
 
Kule serikalini kidogo amepamudu. Ana "watiifu" wake wengi kule. Huku CCM ndio bado. Wazee wale wawili, Msekwa na Makamba wamechoka. Aangalie tu afya yake kama inaruhusu mizunguko yote hii.
 
Sijakata tamaa na JK ingawa hali ya uongozi wake inakatisha tamaa kila mtanzania mwenye matagemeo. I believe JK atafanya maamuzi ambayo hayajawahi kutokea tangu tupate uhuru. I believe mafisadi wamemshika pabaya sana na sasa yuko tayari kukubali fedheha kuliko kuendelea kujipakulia lawama za wananchi juu ya mafisadi.

JK sasa anafahamu fika kwamba mafisadi sasa wanafanikiwa kuteka JWT kwenye kambi yao.....patamu, tusubiri. JK will act...very soon.

Hivi unaweza kukata tamaa na uongozi wa mtu wakati unaendelea kuwa na imani naye kama kiongozi? Am confused.

Nafananisha kauli hii na ile ya REDET kuwa wananchi wana imani na utendaji wa Rais lakini hawana imani na utendaji wa Baraza la Mawaziri na wanasahau kuwa Rais ndiye mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri na ndiye anayesimamia utendaji wa baraza lake.

Ni wakati muafaka sasa kuhusianisha mtu na uongozi wake ili tuwawajibishe hawa pretenders.
 
mtashangaa siku hiyo inafika wanakutana na wanajadili mambo ya kawaiiiiiida, wanakunywa kahawa, wanalipana posho, halafu wanachapa mwendo
 
Hivi unaweza kukata tamaa na uongozi wa mtu wakati unaendelea kuwa na imani naye kama kiongozi? Am confused.

Nafananisha kauli hii na ile ya REDET kuwa wananchi wana imani na utendaji wa Rais lakini hawana imani na utendaji wa Baraza la Mawaziri na wanasahau kuwa Rais ndiye mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri na ndiye anayesimamia utendaji wa baraza lake.

Ni wakati muafaka sasa kuhusianisha mtu na uongozi wake ili tuwawajibishe hawa pretenders.

Na kuliteua pia..........
 
Lakini jambo la muhimu ni... Je, tutalalamika bila kuchukua hatua hadi lini? Kurasa kama hizi ndo za kuhamasishana na kuchukua hatua za kuleta mabadiliko. Oktoba inakuja, je, tumejiandaaje na tunaelimishaje umma wa Kitanzania kwamba miaka ya wanaotutawala imekwisha????

Wildcard mkuu heshima mbele.

Kutawaliwa na CCM si kitu cha kushangilia hata kidogo, Hawa jamaa wote isipokuwa mmoja wanaangalia masilah yao na watoto wao tu na hawana kazi nyingine. Nchi yetu hali ni mbaya ukiangalia kwenye viashiria vyote vya Taifa Imara. Inflation 12% Ndullu yupo tu, Ada za shule za watoto wetu tunatakiwa kulipa kwa dola ( kama vile tuko marekani) wakati mishahara yetu ni kwa Shilingi. Malalamiko kila kona, ujambazi umeongezeka mwingine unawahusisha mapolisi (mfano ukerewe), ajali za barabarani zinaongezeka kila kukicha, wizi wa mali ya umma, Raisi kudanganywa hadharani kila siku (mfano Ufunguzi wa hoteli-Arusha, Kukabidhi Gari Ikulu, Uzinduzi wa malaria basi-THT na sasa Udanganyifu kwenye sheria iliyopitishwa na bunge). Raisi anatokea hadharani kwa mbwembwe kwa issue ambayo baadae inaonekana ni usanii mtupu.

Wildcard haya yote hayana wa kuyaongoza, kuelekeza, au kusimamia sheria. CCM ni kiama chetu sote Tunaoipenda na Tunaoichukia. usishangilie hata kidogo.
 
Nimesoma michango hapa. Wengi wa wachangiaji hawategemei chochote kipya. Isipokuwa mmoja ama wawili tuu. Hii ina maanisha kwamba watu wameshakata tamaa kabisaaa. Na hili ni hatari sana. Kuna theory moja katika economics kwenye mambo ya stock exchange kama sikosei one of the solusion to a problem is "TO DO NOTHING" for sometimes. Nafikiri mimi ni "do nothing" kwanza kwa kuwa vitu vingi hapa kwetu ni vya ajabu sana tuache huo uajabu uendelee kwa kipingi then mambo yanaweza kujipangua yakapisha mengine yakajipanga then tukawa kwenye mstari. Ila tusikate tamaaa....lets fight as usual hizi cheche za fikra zina nguvu sana katika mabadiliko.
 
unachosema ni kweli kaka. juzi tu kiongozi mkuu ikulu ametuhumiwa kwa ukabila vielelezo vichache vikatolewa... lakini kuna hata msemaji mmoja wa ikulu amenyanyua mdomo kujibu? au hata yeye mwenyewe mtuhumiwa? wanajua, watanzania kazi yao kusema tu lakini 'no action' . hatuna meno ya kuuma wala kutafuna. tunameza vizima vizima tu. kwa nini akose usingizi?. Ukabila hoyeeeeeee!!!
 
Hii inanikumbusha nikiwa JKT. Watu wanakamatwa na kuwekwa Lupango (jela ya jeshi). Wakiwa ndani ya Lupango, wanasikia kishindo cha buty na wanaanza kubishana:
Kuruta1. Huyo atakuwa Afande Manyirizu.
Kuruta2. Hapana huyo atakuwa Captain Wawa.
Kuruta3. Hamna kitu, huyo kwa vyovyote ni Afande Magwega.

Si tusubiri tu siku ifike tutasikia kilichotokea? Na hasa CCM ambayo siku hizi vikao na mafaili yao yanamatundu yanayovujisha habari bila hata ya kuombwa. Sijui huwa wanauza hizi habari au wenyewe tu wanabadilishana na Waandishi wa habari kwa makubaliano kuwa waje wapigiwe debe?

Mkuu Fidel, hivi inakuwaje hii tabia ya kufunga mtaa mzima eti kwa sababu fulani yuko jengo fulani au anapita? Mtaa unakuwa umefungwa muda wote wakati yeye yupo pale au kwa muda tu?

Dr. Slaa, hivi CHADEMA mna mpango gani wa kuja kupendekeza muda ambao POLISI wanaweza kufunga barabara wakati kiongozi fulani anatarajiwa kupita? Hii tabia ya kufunga barabara ambazo mkuu fulani atapita kwa kweli inaumiza sana wananchi. Wakati Kigogo ndiyo kwanza anaingia bafuni kuoga, aje apate kifungua kinywa na ndiyo aondoke, Polisi huku wao tayari wameshafunga barabara. Hivi haziwezi kufungwa dakika 5-15 kabla? Si itatosha kabisa kusimamisha na kuweka magari pembeni? Ikibidi, basi Chadema wapendekeze Rais anunuliwe Helcopiter. Na mwisho itakuwa safi tu maana anapenda sana kuruka. Kuna haja sheria za ufungaji barabara ziwepo na si watu wanajiamulia tu kufunga kwa muda wanaotaka kwa sababu tu hawataki kufanya kazi ngumu/kazi ya ziada. Na kama sehemu hiyo si salama, basi watafute sehemu iliyojitenga na salama na wafanyie vikao vyao/mikutano.
 
JK must wake up, and I pray he does. He must appreciate absence of life-long friend or enemy in politics. In politics friends can be just as deadly as enemies and so they should be treated....kama mafisadi wamefikia hatua ya kupata support ya wanajeshi crisis bells must go off and president must act. I live to think he will act, I don't want to think otherwise.

I wish you all the best as you continue with your day dreaming. Huwezi kumbadilisha chui madoa yake kwa kuomba dua.
 
Hii inanikumbusha nikiwa JKT. Watu wanakamatwa na kuwekwa Lupango (jela ya jeshi). Wakiwa ndani ya Lupango, wanasikia kishindo cha buty na wanaanza kubishana:
Kuruta1. Huyo atakuwa Afande Manyirizu.
Kuruta2. Hapana huyo atakuwa Captain Wawa.
Kuruta3. Hamna kitu, huyo kwa vyovyote ni Afande Magwega.

Si tusubiri tu siku ifike tutasikia kilichotokea? Na hasa CCM ambayo siku hizi vikao na mafaili yao yanamatundu yanayovujisha habari bila hata ya kuombwa. Sijui huwa wanauza hizi habari au wenyewe tu wanabadilishana na Waandishi wa habari kwa makubaliano kuwa waje wapigiwe debe?

Mkuu Fidel, hivi inakuwaje hii tabia ya kufunga mtaa mzima eti kwa sababu fulani yuko jengo fulani au anapita? Mtaa unakuwa umefungwa muda wote wakati yeye yupo pale au kwa muda tu?

Dr. Slaa, hivi CHADEMA mna mpango gani wa kuja kupanga muda ambao POLISI wanaweza kufunga barabara wakati kiongozi fulani anatarajiwa kupita? Hii tabia ya kufunga barabara ambazo mkuu fulani atapita kwa kweli inaumiza sana wananchi. Wakati Kigogo ndiyo kwanza anaingia bafuni kuoga, aje apate kifungua kinywa na ndiyo aondoke, Polisi huku wao tayari wameshafunga barabara. Hivi haziwezi kufungwa dakika 5-15 kabla? Si itatosha kabisa kusimamisha na kuweka magari pembeni? Ikibidi, basi Chadema wapendekeze Rais anunuliwe Helcopiter. Na mwisho itakuwa safi tu maana anapenda sana kuruka. Kuna haja sheria za ufungaji barabara ziwepo na si watu wanajiamulia tu kufunga kwa muda wanaotaka kwa sababu tu hawataki kufanya kazi ngumu/kazi ya ziada. Na kama sehemu hiyo si salama, basi watafute sehemu iliyojitenga na salama na wafanyie vikao vyao/mikutano.

Naunga mkono wazo la kununua helicopter kwa ajili ya rais na viongozi wengine wanaohitaji msafara. Ila itabidi wanunue helicopter nyingi maana msafara wa mkuu wa nchi una watu wengi ati. Au wapunguze idadi ya wajumbe wanaoongozana na rais kila anaposafiri au kufanya ziara.
 
Matumaini ya kukomaa kwa CCM au niseme kumeguka kwa CCM nilikuwa nayo wakati wanaenda kikao cha Butiama (Musoma). Baada ya pale, sioni tena chini ya huyu jamaa.
 
JK must wake up, and I pray he does. He must appreciate absence of life-long friend or enemy in politics. In politics friends can be just as deadly as enemies and so they should be treated....kama mafisadi wamefikia hatua ya kupata support ya wanajeshi crisis bells must go off and president must act. I live to think he will act, I don't want to think otherwise.

I wish you all the best as you continue with your day dreaming. Huwezi kumbadilisha chui madoa yake kwa kuomba dua.


Mkuu, hapo kwenye Nyekundu una uhakika napo? Unaweza kufafanua zaidi? Panatisha ati. Yaani wanajeshi wamewekwa mfukoni na Mafisadi na JK bado anatabasamu?
 
Back
Top Bottom