CCM dhaifu Vs Lowassa mwerevu: Anguko lililo wazi CCM

leo nimeamini kwamba viongozi wengi wa ccm ni wajinga na mbaya zaidi wameamua kupambana na lowasa mwerevu.

How comes viongozi wa ccm (wakiongozwa na nape) wanamwogopa hivi lowasa? Kama lowasa ni mchafu hivi iweje viongozi wa ccm ( sitta, chiligati na nape) wanatumia njia za majungu, fitna, njia zisizokuwa za moja kwa moja kupambana na lowasa?

1. Juzi tumeshuhudia ccm wakifanyia mabadiliko katiba yao wakiweka vihunzi vingi lakini kwa mjanja ukiangalia lengo ni kupunguza nguvu za lowasa kuelekea 2015, hivi lowasa asipogombea urais 2015 kwa sababu yeyote ile ( aaamue, afe au hata augue) ccm watarudi kurekebisha katiba yao tena? Kama wanaamini kwamba lowasa ni mchafu kiasi hicho kwa nini wasimkamate au kumfukuza uanachama badala yake wanatumia njia za kumvizia/ uoga huu una nini? Au wamegundua aliye mchafu si lowasa?

2. Tumeona kura za maoni arumeru mashariki jinsi sioi sumari alivyotakiwa kutoswa kisa eti ana unasaba na loawas. Hivi chama chenye jeshi, polisi, mahakama, takukuru kimefikia hatua ya kuogopa kivuli cha lowasa kwa namna hii kweli? Walianza akina nape na kina chatanda kupiga majungu ya utata wa uraia wa sioi lengo lao likiwa kumtosa mkwe wa laigwanan wa kimasai. Cc nayo ikaingia mkenge ila ikatumia busara kidogo ya kurudia uchaguzi huku wakiamini kwamba sioi angeshindwa. Mpaka nimefikia sasa na mimi naanza kuamini kwamba tatizo la lowasa si ufisadi bali urais 2015 na kuna watu wameshagundua "werevu wa mtu huyu"

nape, chiligati, mwigulu onesheni uanaume wenu acheni kutumia indirect method kupambana na lowasa kama hamna uhakika na tuhuma zake mwacheni.

Kuna mpuuzi mmoja leo ameleta mada juu ya lowasa kuumbuliwa na takukuru arumeru, mada ilichangiwa na watu wengi sana wakiamini utunzi wa mpuuzi yule.

Wajanja walishagundua kwamba akina nape walishagundua nguvu ya lowasa wakaanza kuleta propaganda zao ili baadae sioi akishinda ionekane ni nguvu za pesa.

Hivi kweli lowasa atume sms kuagiza mtu akatoe rushwa? Lowasa ambaye ccm ya akina sita inatafuta namna ya kumtoa ccm lakini inashindwa?

Haya sasa sioi ameshinda ni jukumu sasa la akina nape kwenda kushirikiana na lowasa kuhakikisha kwamba mkwe wa lowasa anashinda arusha

kitu pekee ninachokiona hapa na mods naomba muweke maneno yangu haya kama kumbukumbu " mwaka 2015 lowasa ahatagombea urais ila ccm itamtegemea sana lowasa kama ilivyomtegemea mwalimu nyerere kushinda 1995" sina lengo la kumfananisha lowasa na mwalimu ( lowasa ni mchafu kama walivyo wachafu wote wa ccm) la hasha ila kwa sasa ndani ya ccm loawas ndiye mwana siasa mwenye mvuto ndani ya ccm na amini usiamini nyota yake imeng'azwa kwa fitna za akina nape, sita, mwakyembe na wengine na amin amin nawaambia katika wote hao hakuna anayeweza kuthibisha uchafu wa edward pasipo kumhusisha nwenyekiti wa chama ndiyo sasa wameamua kutumia njia za uoga kupambana na lowasa

hata nyere pia alikuwa mchafu wa siasa, alichangia kubatilisha ushindi wa wapinzani kule zanzibar.
 
Who told u that Pasco?Arumeru ngoma bado ndefu,usifanye conclusion kirahisi rahisi namna hiyo
Arumeru is done!, kinachoendelea sasa ni kukamilisha tuu taratibu!. Wameru ni watu wenye msimamo, uamuzi wamchague nani, umeishafanyika hivyo hautegemei kampeni yoyote!.

Kama ni kamanda yule yule aliomba kura kwa watu hao hao huku akishindana na kivili cha mahituti kitandani, what chances does he stand?!.
 
Who told u that Pasco?Arumeru ngoma bado ndefu,usifanye conclusion kirahisi rahisi namna hiyo
Arumeru is done!, kinachoendelea sasa ni kukamilisha tuu taratibu!. Wameru ni watu wenye msimamo, uamuzi wamchague nani, umeishafanyika hivyo hautegemei kampeni yoyote!.

Kama ni kamanda yule yule aliyeomba kura kwa watu hao hao huku akishindana na kivuli cha mahututi kitandani, na akatoswa, what chances does he stand now?,
Next....?.
 
Mimi huwa nawashangaa sana hawa vijana wenzetu akina Nape kukingiana vifua na EL. EL is the heavy weight kulinganisha na safu zote za CCM, hii ni taa nyingine iwakayo na itakayogonga vichwa vya wanachama kuelekea mkutano mkuu wa Chama na chaguzi zao zilizoambatana na mabadiliko ya katiba zao.
 
Arumeru is done!, kinachoendelea sasa ni kukamilisha tuu taratibu!. Wameru ni watu wenye msimamo, uamuzi wamchague nani, umeishafanyika hivyo hautegemei kampeni yoyote!.

Kama ni kamanda yule yule aliomba kura kwa watu hao hao huku akishindana na kivili cha mahituti kitandani, what chances does he stand?!.
Huu ndio ukweli mchungu na si wa kupuuza!
 
Arumeru is done!, kinachoendelea sasa ni kukamilisha tuu taratibu!. Wameru ni watu wenye msimamo, uamuzi wamchague nani, umeishafanyika hivyo hautegemei kampeni yoyote!.

Kama ni kamanda yule yule aliomba kura kwa watu hao hao huku akishindana na kivili cha mahituti kitandani, na akatoswa, what chances does he stand now?,
Next....?.
Kuna msemo unasema 'Watanzania si wajinga tena'....So CCM tusitegemee mteremko hapa.....

Binafsi nilitegemea kwenye hatua ya awali ya kura Sioi Sumari(kama kweli anakubalika kutokana na kukubalika kwa baba yake) angepata asilimia 100 kama sio 51 ya kura za maoni....Lakini cha kushangaza alipata asilimia 30+ tu ya kura...Hii ina maana alikuwa hakubaliki hata ndani ya CCM wilayani Arumeru......Kitu ambacho ni hatari sana maana nilitegemea angepata ushindi wa kishindo.....Hayo masuala ya kwamba baba yake alishinda akiwa kitandani so na mwanaye atashinda hayana nafasi na tusiyape nafasi kabisa maana Jery Sumari na Sioi Sumari ni watu wawili tofauti na mbaya zaidi huyo Sioi alikuwa hajishughulishi na mambo ya siasa(ameibuka mara tu baada ya baba yake kufariki)......Sina uhakika kama Wameru wote wana mawazo finyu kama haya unayotaka tuyaamini kwamba wanaendekeza mambo ya kurithishana,kwamba wanamchagua mtu kwa kujuana na si kwa kuangalia sera/Ilani ya chama chake wala uwezo wake....Hili litakuwa ni TUSI kubwa sana kwa Wameru na kama CCM wanataka Sioi ashinde wasijaribu kutumia ama kuitegemea dhana hii mbaya na chafu........

Sina uhakika(pamoja na kuwa ni Mwanasheria) na uwezo wa Sioi wa kumiliki jukwaa la kisiasa(kuongea kwenye haliki kubwa ya wananchi wakati wa kampeni) kama ilivyo kwa mpinzani wake wa karbu Joshua Nasari,...Huyu bwana mdogo anaongea na ana uwezo mkubwa sana wa kulimiliki Jukwaa na pamoja na kushindwa kwa zaidi ya kura 11,000 na Jery Sumary,huyu kijana alionesha kwamba anao uwezo mkubwa wa kuhimili siasa za ushindani hasa ukizingatia kwamba alikuwa akishindana na mtu ambaye pamoja na kwamba ni kama baba yake pia alikuwa ni mwanasiasa mzoefu,Mbunge aliyemaliza muda wake,Naibu Waziri na pia Mzazi mwenza wa aliyepata kuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa.....Pamoja na hayo yoote huyu kijana aliweza kupata kura nyingi kiasi cha kuwa tishio kwa Jerry Sumari....

Ninawashauri wana CCM wasibweteke na waachane na hii dhana mbaya na potofu ya Pasco ya kusema eti 'Arumeru is Done' kisa tu Mkwe wa Lowassa ameshinda kuiwakilisha CCM.....Haiwezekani eti mtu ambaye hakubaliki ndani ya chama chake(kwa matokeo ya awali na hata ya leo) eti ndio apewe nafasi kubwa ya kumshinda kijana mahiri wa aina ya Nasari......Nakataa.....Cha msingi ni CCM kujipanga kwa ajili ya mapambano(ya kisera) na si kubweteka eti watashinda kiulaini.......Tanzania ya sasa si ya mwaka 1995 wala 2000.......Ikumbukwe kwamba mara baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 mkoa wa Arusha hasa wilaya za Arusha mjini na Arumeru umekuwa ni ngome kuu ya CHADEMA na maandamano na hekaheka za kisiasa ambazo zimekuwa zikitokea mara baada ya uchaguzi huo zimeifanya CHADEMA izidi kupata wafuasi na wanachama katika wilaya za Arusha mjini na Arumeru hivyo CCM tusitegemee kushinda kiulaini kama Pasco anavyojaribu kupotosha......Kama Lowassa anakubalika sana Arumeru na ndani ya CCM sidhani kama mkwewe Sioi angeweza kupata asilimia 30+ ya kura za maoni za awali na hata uchaguzi wa leo inajulikana wazi kwamba Sioi ameshinda kutokana na nguvu ya ziada iliyotumika ikiwa ni pamoja na matumizi makubwa ya fedha ambapo imeripotiwa kwamba TAKUKURU wamewakamata watu watatu(03) ambao wanadaiwa ni wafuasi wa Sioi wakijihusihsa na vitendo vya utoaji wa Rushwa kwa wana CCM...

CCM inapaswa kugangamala na kujipanga maana kazi iliyopo mbele ni ngumu hasa tofauti na Pasco anavyotaka tuamini....

Wakatabahu......

Bala.
 
hapo ndipo utamkubali mzee EL, yaani formula anazo yeye, wengine mtabaki kuona majawabu na matokeo tu....


 
  1. Walianza na kumfitini EL ili aache uwaziri mkuu...Nilisikiliza ile hotuba ya mwakyembe bungeni akisoma ripoti ya richmond na akinena kwa nguvu na ujasiri mkubwa, alivyoipamba ile ripoti wananchi tulielewa wazi kuwa lowasa ndio alikuwa tattizo. Kumbe kweli , ukweli huwa haufi, utasimama daima. Hata kama lowasa alishiriki kwenye huo mchakato kweli kulikuwa na ulazima wa kufanya ripoti ionekane ni makosa ya mtu mmoja---yaani waziri mkuu?. Alafu eti unamalizia kwa kusema mambo mengine tumeyaficha kuokoa serikali.! Sasa ndio tunazidi kupata ukweli kuwa fitna, majungu na matusi dhidi ya lowasa toka hapo mwanzo hadi leo hii sio sababu ya ufisadi wala sio kwa sababu ya kusafisha chama , bali ni maslahi ya watu binafsi wenye chuki, roho mbaya ,na tamaa ya urais 2015.
  2. wakaja kujivua gamba-----lengo pia ni lowassa....ikaonekana kila mtu gamba---wavuaji na wavuliwa
  3. mara marekebisho ya katiba ya ccm.......lengo pia kumuondoa lowasa

hivi kweli ccm imekosa sera au ajendanyingine ya kurudisha imani ya wananchi zaidi ya kukuza mgogoro katiyake (ccm) na mtu binafsi (EL)? Sasa tunaaza kupata picha kuwatatizo hasa si lowasa
 
hapo ndipo utamkubali mzee EL, yaani formula anazo yeye, wengine mtabaki kuona majawabu na matokeo tu....



Kambi ya Lowassa yaumiza vigogo CCM Send to a friend
Thursday, 01 March 2012 21:07
0digg

lowassa-top-safi.jpg
Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa

SIYOI AMBWAGA TENA SARAKIKYA
Waandishi Wetu, Arusha
KWA mara ya pili, wana CCM Jimbo la Arumeru Mashariki wamedhihirisha kuwa chaguo lao ni Siyoi Sumari baada ya kumchagua kwa kura 761 na kumtupa mbali mpinzani wake, William Sarakikya aliyepata kura 361 katika uchaguzi wa marudio uliofanyika jana.Matokeo hayo ni kama ushindi kwa mojawapo ya kambi ndani ya CCM inayohusishwa na Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa dhidi ya wanachama waliopo katika makundi mengine, ambayo yalikuwa yakipinga kwa nguvu zote kupitishwa kwa jina la Siyoi.

Vyombo mbalimbali vya habari kwa wiki nzima sasa, vimekuwa vikiripoti kuhusu mgawanyiko ndani ya chama hicho tawala kutokana kuwa na misimamo inayokinza kuhusu nani atakayepeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi huo mdogo.

Siyoi alianza kuzua mtafaruku ndani ya CCM pale suala la uraia wake lilipozua utata ndani ya kikao cha Sekretarieti ya chama hicho, hivyo kusababisha kutolewa kwa mapendekezo kwamba aenguliwe katika kinyang'anyiro hicho.

Kundi linalomtetea limekuwa likilalamikia kile linachodai kwamba ni kuwapo kwa njama za kumtosa mshindi huyo kwa sababu kadhaa za kimakundi.

Hata hivyo, Kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichokutana chini ya Mwenyekiti, Rais Jakaya Kikwete kiliamuru kurudiwa kwa uchaguzi baina ya Siyoi na Sarakikya, kwa maelezo kwamba katika wagombea wote sita hakuna aliyekuwa amepata zaidi ya nusu ya kura zilizopigwa.

Habari zaidi zilidai kuwa, hata baada ya kutolewa kwa uamuzi wa kurudiwa kwa uchaguzi huo, mmoja wa vigogo wa CCM alituma mmoja wa wajumbe wa Kamati Kuu kwenda kumshawishi Siyoi ajitoe kwenye kinyang'anyiro hicho, jitihada ambazo hazikufanikiwa kwani alikataa.

Matokeo ya kura
Matokeo ya uchaguzi huo yaliyotangazwa Saa 11:30 jioni na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa, Sumari aliibuka na ushindi huo wa silimia 67.8 kati ya kura halali 1,122 zilizopigwa, dhidi ya asilimia 32.2 za mpinzani wake anayedaiwa kupigiwa chapuo na viongozi wa chama na Serikali kuanzia ngazi ya Wilaya, Mkoa hadi taifa.

Jumla ya kura 1,124 zilipigwa ambapo mbili ziliharibika na kura halali kubakia 1,122.

Akitangaza matokeo hayo, Msekwa alilazimika kuanza kwa kumtangaza mshindi hali iliyofanya ukumbi kukosa usikivu kwa wapenzi, mashabiki na wafuasi wa Siyoi kuanza kushangilia.

Msekwa alisema ameridhishwa na upigaji kura na matokeo hayo yameonyesha imani kubwa waliyonayo wana Arumeru kwa mgombea huyo.

Baadhi ya wana CCM walidai kuwa kauli tata za Msekwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), John Chiligati katika ufunguzi wa mkutano mkuu maalum wa Wilaya ya Arumeru jana zilimponza, Sarakikya baada ya wajumbe kuamua kupiga kura za hasira wakipinga kile walichodai kushinikizwa kumchagua mtu aliyeelezwa anatakiwa na mfumo (system), wa Serikali na uongozi wa chama.

Awali wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa ufunguzi wa mkutano huo uliohudhuriwa na idadi kubwa ya maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), maofisa usalama wa taifa na askari kanzu kutoka Jeshi la Polisi, Msekwa na Chiligati waliwataka wajumbe kutumia vyema kura yao kumchagua mtu atakayemudu na kuhimili vishindo vya upinzani kutoka vyama vingine vitakavyosimamisha wagombea.

"Ndugu wajumbe napenda kuwakumbusha jambo moja muhimu kabla ya kupiga kura, leo hatuchagui mbunge, mnachofanya ni kupiga kura za maoni. Mgombea atateuliwa na kikao cha Kamati Kuu Machi 3, mwaka huu," alisema Chiligati.

Wakati Chiligati akisititiza hoja hiyo, Msekwa alikuwa akitikisa kichwa kuonyesha kukubaliana na maneno aliyokuwa akiyasema Naibu Katibu Mkuu huyo huku baadhi ya wajumbe wakiguna.

Msekwa aliyetumia muda mwingi kuzungumzia historia yake ya uongozi ndani ya chama kuanzia TANU hadi CCM aliwataka wajumbe kutoangalia uswahiba wala ushawishi wa aina yoyote katika maamuzi yao bali wahakikishe wanayemchagua anastahili kupeperusha bendera ya chama hicho tawala na kukiletea ushindi.

juusiyoi.jpg
Siyoi Sumari akiwa amebebwa na wafuasi wa CCM baada ya kuibuka mshindi wa kura za maoni za mgombea Ubunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki kupitia chama hicho, jana. Picha na Filbert Rweyemamu

Katika uchaguzi wa awali wa kura za maoni uliofanyika Februari 20, mwaka huu, Siyoi ambaye ni mtoto wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Jeremia Sumari aliyefariki hivi karibuni aliongoza kwa kupata kura 361 akifuatiwa na Sarakikya alijinyakulia kura 259.

Wagombea wengine na kura walizopata katika uchaguzi wa awali kwenye mabano ni pamoja na Elirehema Kaaya (205), Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC), Elishilia Kaaya (176), Antony Msami (22) na Elishiankira Urio aliyeambulia kura 11.

Msami tayari amehamia Chadema alikochukua fomu kuomba uteuzi wa kupeperusha bendera ya chama hicho na kuambulia kura 8 katika uchaguzi wa kura za maoni ndani ya chama hicho zilizopigwa juzi eneo la Maji ya Chai wilayani Arumeru.

Kamatakamata ya Takukuru

Katika hatua nyingine, kitendo cha kuwakamata baadhi ya viongozi na makada wa chama hicho juzi kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa kwa lengo la kumsaidia mmoja wa wagombea jana kilibadilisha upepo miongoni mwa wapiga kura ambao wengi walidai kitendo hicho kililenga kumnufaisha mmoja wa wagombea na hivyo kuazimia kuonyesha hasira yao kwenye sanduku la kura.

Miongoni mwa viongozi na makada wa CCM aliyekamatwa kwa kudaiwa kujihusisha isivyo halali katika kampeni za Siyoi ni pamoja na Diwani wa Kata ya Mbuguni, Thomas Mollel maarufu kwa jina la ‘Askofu' aliyesema baada ya kutiwa mbaroni kwa maagizo ya watu aliowaita wakubwa, alihojiwa kwanini anamfanyia kampeni mgombea huyo na aliyemtuma kufanya hivyo.

Ingawa kamanda wa Takukuru Mkoa wa Arusha, Mbengwa Kasomambuto alikataa kuwataja viongozi wengine walioshikiliwa juzi kwa mahojiano, waandishi wetu waliofika ofisi za taasisi hiyo walimshuhudia mmoja wa waliogombea katika awamu ya kwanza ya kura za maoni pamoja katibu wa UVCCM katika moja za Wilaya za Mkoa wa Arusha wakihojiwa na maafisa wa idara hiyo ya dola.

Katika orodha hiyo pia walikuwapo madiwani wawili wa Kata za Arumeru na jana eneo lote la mkutano ulijaa maafisa wa Takukuru, na askari kanzu waliokuwa wakiranda kila kona na kujisogeza kwenye kila kundi la watu zaidi ya wawili walioonekana kuzungumza kwa lengo la kunasa mazungumzo yao.

Maofisa wa Takukuru jana waliendela na kamatakamata hadi muda mfupi kabla ya matokeo ambapo mmoja wa kada maarufu wa vijana wa CCM wilayani Arumeru, Ally Majeshi alitiwa mbaroni kwa mahojiano baada ya kudaiwa kutajwa na baadhi ya watuhumiwa waliokamatwa juzi.

Shamrashamra
Baada ya matokeo, Siyoi alitoka ukumbini akiwa amebebwa juu juu na wafuasi wake kwa umbali wa zaidi ya kilomita mbili huku watu wanaoaminika kuwa wafuasi wa Sarakikya wakiwa wamebaki eneo la ukumbi wa mkutano katika makundi wakijadiliana.

Akizungumzia matokeo hayo, Sarakikya alikubali kushindwa na kumpongeza mgombea mwenzake akimtakia kila la kheri katika uchaguzi ujao wakati mshindi akiwashukuru wajumbe kwa imani waliyoonyesha kwake akiwataka kuanza kampeni za kutafuta ushindi wa CCM.
 
Arumeru is done!, kinachoendelea sasa ni kukamilisha tuu taratibu!. Wameru ni watu wenye msimamo, uamuzi wamchague nani, umeishafanyika hivyo hautegemei kampeni yoyote!.

Kama ni kamanda yule yule aliomba kura kwa watu hao hao huku akishindana na kivili cha mahituti kitandani, na akatoswa, what chances does he stand now?,
Next....?.
Tatizo wana Magamba somo la Igunga mnajifanya halijawaingia kabisaaa...
 
Kuna msemo unasema 'Watanzania si wajinga tena'....So CCM tusitegemee mteremko hapa.....

Binafsi nilitegemea kwenye hatua ya awali ya kura Sioi Sumari(kama kweli anakubalika kutokana na kukubalika kwa baba yake) angepata asilimia 100 kama sio 51 ya kura za maoni....Lakini cha kushangaza alipata asilimia 30+ tu ya kura...Hii ina maana alikuwa hakubaliki hata ndani ya CCM wilayani Arumeru......Kitu ambacho ni hatari sana maana nilitegemea angepata ushindi wa kishindo.....Hayo masuala ya kwamba baba yake alishinda akiwa kitandani so na mwanaye atashinda hayana nafasi na tusiyape nafasi kabisa maana Jery Sumari na Sioi Sumari ni watu wawili tofauti na mbaya zaidi huyo Sioi alikuwa hajishughulishi na mambo ya siasa(ameibuka mara tu baada ya baba yake kufariki)......Sina uhakika kama Wameru wote wana mawazo finyu kama haya unayotaka tuyaamini kwamba wanaendekeza mambo ya kurithishana,kwamba wanamchagua mtu kwa kujuana na si kwa kuangalia sera/Ilani ya chama chake wala uwezo wake....Hili litakuwa ni TUSI kubwa sana kwa Wameru na kama CCM wanataka Sioi ashinde wasijaribu kutumia ama kuitegemea dhana hii mbaya na chafu........

Sina uhakika(pamoja na kuwa ni Mwanasheria) na uwezo wa Sioi wa kumiliki jukwaa la kisiasa(kuongea kwenye haliki kubwa ya wananchi wakati wa kampeni) kama ilivyo kwa mpinzani wake wa karbu Joshua Nasari,...Huyu bwana mdogo anaongea na ana uwezo mkubwa sana wa kulimiliki Jukwaa na pamoja na kushindwa kwa zaidi ya kura 11,000 na Jery Sumary,huyu kijana alionesha kwamba anao uwezo mkubwa wa kuhimili siasa za ushindani hasa ukizingatia kwamba alikuwa akishindana na mtu ambaye pamoja na kwamba ni kama baba yake pia alikuwa ni mwanasiasa mzoefu,Mbunge aliyemaliza muda wake,Naibu Waziri na pia Mzazi mwenza wa aliyepata kuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa.....Pamoja na hayo yoote huyu kijana aliweza kupata kura nyingi kiasi cha kuwa tishio kwa Jerry Sumari....

Ninawashauri wana CCM wasibweteke na waachane na hii dhana mbaya na potofu ya Pasco ya kusema eti 'Arumeru is Done' kisa tu Mkwe wa Lowassa ameshinda kuiwakilisha CCM.....Haiwezekani eti mtu ambaye hakubaliki ndani ya chama chake(kwa matokeo ya awali na hata ya leo) eti ndio apewe nafasi kubwa ya kumshinda kijana mahiri wa aina ya Nasari......Nakataa.....Cha msingi ni CCM kujipanga kwa ajili ya mapambano(ya kisera) na si kubweteka eti watashinda kiulaini.......Tanzania ya sasa si ya mwaka 1995 wala 2000.......Ikumbukwe kwamba mara baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 mkoa wa Arusha hasa wilaya za Arusha mjini na Arumeru umekuwa ni ngome kuu ya CHADEMA na maandamano na hekaheka za kisiasa ambazo zimekuwa zikitokea mara baada ya uchaguzi huo zimeifanya CHADEMA izidi kupata wafuasi na wanachama katika wilaya za Arusha mjini na Arumeru hivyo CCM tusitegemee kushinda kiulaini kama Pasco anavyojaribu kupotosha......Kama Lowassa anakubalika sana Arumeru na ndani ya CCM sidhani kama mkwewe Sioi angeweza kupata asilimia 30+ ya kura za maoni za awali na hata uchaguzi wa leo inajulikana wazi kwamba Sioi ameshinda kutokana na nguvu ya ziada iliyotumika ikiwa ni pamoja na matumizi makubwa ya fedha ambapo imeripotiwa kwamba TAKUKURU wamewakamata watu watatu(03) ambao wanadaiwa ni wafuasi wa Sioi wakijihusihsa na vitendo vya utoaji wa Rushwa kwa wana CCM...

CCM inapaswa kugangamala na kujipanga maana kazi iliyopo mbele ni ngumu hasa tofauti na Pasco anavyotaka tuamini....

Wakatabahu......

Bala.
Mkuu Balantanda, where are you now days?. JF we are missing analysis za kihivi!. Anayejua huyu member yuko wapi atujuze, that was some 10 years back!.
Hiki alichoandika ndicho kilikuja ku tokea!.
P
 
Mkuu Balantanda, where are you now days?. JF we are missing analysis za kihivi!. Anayejua huyu member yuko wapi atujuze, that was some 10 years back!.
Hiki alichoandika ndicho kilikuja ku tokea!.
P
Nipo Comrade.

Siku hizi nimekuwa Msomaji na Mtazamaji zaidi..Si Mchangiaji sana…Nachangia kwa kuibiaibia..Ila siku zote nipo humu ndani..

Bala.
 
Nipo Comrade.

Siku hizi nimekuwa Msomaji na Mtazamaji zaidi..Si Mchangiaji sana…Nachangia kwa kuibiaibia..Ila siku zote nipo humu ndani..

Bala.
Mkuu Bala, thanks for knowing upo, leo nilikuwa napitia hoja zako kwenye hili, I was very wrong and you were very right, kitu nilichopenda zaidi ni kule kutoa hoja supported by reasons. Hiki kitu jf ya sasa ina ki miss. Nashauri kwenye issues za maslahi ya taifa, uwe unakuja kuja ili tulisaidie taifa letu.

Bado sijajua kwanini nimeletwa huku, I think these is something about the oldman, tutasikia soon!.
P
 
Back
Top Bottom