Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,295
- 33,079
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF), Ofisi ya Usajili wa Vitambulisho vya Mzanzibari Mkazi, zimekubaliana kubadili utaratibu wa uandikishaji wa vitambulisho na sasa utafanyika shehia kwa shehia na kwa tarehe maalumu kuanzia Jumatatu ijayo.
Hatua hiyo inatokana na utaratibu wa awali ambao uliwalazimu wananchi baada ya kuchukua fomu katika shehia zao kufika ofisi ya Mkuu wa Wilaya, ambako walikuwa wakipata vitambulisho hivyo.
Akizungumza jana mjini hapa, Ofisa Tawala wa Wilaya ya Wete, Khamis Juma Silima, alisema makubaliano hayo yalifikiwa juzi kwenye kikao kilichofanyika ofisini kwa Mkuu wa Wilaya na kuhudhuriwa na Mwenyekiti wa CUF, Khalifa Mohammed Issa na Kaimu Katibu wa CUF wa Wilaya, Haidary Ali Abdallah.
Wengine waliohudhuria ni Katibu wa CCM wa Wilaya, Said Abdallah Suluhu na Mhazini wa CCM, Ramadhan Issa Kipaya na Mkuu wa Idara ya Vitambulisho Pemba, Hamad Shamata Hamad.
Watakaohusika kujiandikisha ni wenye vyeti vya kuzaliwa, na wakishapata vitambulisho hivyo watajiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, ambalo uandikishaji wake umesitishwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kutokana na vurugu zilizojitokeza wakati wa uandikishaji.
Kulingana na ratiba hiyo, inaonesha kuwa Jumatano na Jumanne wiki ijayo uandikishaji utafanyika shehia za Kambini na Kiuyu Minungwini, wakati siku mbili zinazofuata itakuwa Kiuyu Kigongoni na Ole. Agosti 21 na 22 itakuwa Mjini Ole na Kangani, wakati siku mbili baadaye itakuwa Piki na Mzambarauni Takao, huku Agosti 26 na 27 itakuwa Mtambwe Kusini na Kaskazini.
Agosti 28 na 29 itakuwa Kisiwani na Limbani na Agosti 31 na Septemba mosi itakuwa Jadida na Kipangani, wakati Septemba 2 na 3, itakuwa Pandani na Selemu na siku mbili zitakazofuata itakuwa Utaani na Bopwe. Kwa mujibu wa ratiba, Septemba 7 na 8 itakuwa Kizimbani na Fundo, siku mbili zitakazofuata, itakuwa Gando na Ukunjwi, huku Junguni na Mchangamdogo ikiwa ni Septemba 11 na 12.
Kulingana na ratiba hiyo, Maziwani na Kojani A itakuwa Septemba 14 na 15, ambapo siku mbili zitakazofuata, itakuwa Kiungoni na Pembeni, ambapo Shengejuu na Mpambani itakuwa Septemba 18 na 19 na shughuli hiyo itahitimishwa Septemba 25 na 26 kwa shehia za Chwale na Kinyikani.
Hata hivyo licha ya ratiba hiyo, bado jana kulionekana baadhi ya wananchi wakiwa katika makundi wengine waking'ang'ania kutaka wapewe vitambulisho hivyo kwenye ofisi hiyo hiyo ya Mkuu wa Wilaya.
Utaratibu wa awali ingawa ulikuwa mzuri, lakini ulipata upinzani kutoka kwa baadhi ya viongozi wa CUF waliodai una usumbufu mkubwa na kuzua zogo, kwamba baadhi ya wananchi wananyimwa fomu za kuandikishwa hasa wasiokuwa na vyeti vya kuzaliwa.
Hata hivyo Jumanne wiki hii, akizungumza katika mkutano na viongozi wa kisiasa, masheha na baadhi ya watendaji wa Serikali, Mkurugenzi wa Idara ya Vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi, Mohammed Juma Ame, aliwataka wasio na vyeti vya kuzaliwa waende mahakamani waape na kupewa fomu za kuandikishwa.
Uandikishaji wa vitambulisho vya Mzanzibari Mkazi ulianza mwaka 2005, lakini baadhi ya wananchi walikuwa hawajitokezi kuchukua fomu kwa vile masuala ya Serikali yamekuwa hayapewi kipaumbele kisiwani hapa na hayaungwi mkono.
Pemba asilimia kubwa ni wafuasi wa CUF. Lakini baada ya kutolewa tamko kwamba wasio na vitambulisho hawataingia kwenye Daftari, sasa mwamko umekuwa mkubwa, kila mtu akitaka kujiandikisha na kusababisha vurugu katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya, ambazo ndizo zinatoa vitambulisho, wakati shehia zinatoa fomu za kupata vitambulisho hivyo.
http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=3192
Hatua hiyo inatokana na utaratibu wa awali ambao uliwalazimu wananchi baada ya kuchukua fomu katika shehia zao kufika ofisi ya Mkuu wa Wilaya, ambako walikuwa wakipata vitambulisho hivyo.
Akizungumza jana mjini hapa, Ofisa Tawala wa Wilaya ya Wete, Khamis Juma Silima, alisema makubaliano hayo yalifikiwa juzi kwenye kikao kilichofanyika ofisini kwa Mkuu wa Wilaya na kuhudhuriwa na Mwenyekiti wa CUF, Khalifa Mohammed Issa na Kaimu Katibu wa CUF wa Wilaya, Haidary Ali Abdallah.
Wengine waliohudhuria ni Katibu wa CCM wa Wilaya, Said Abdallah Suluhu na Mhazini wa CCM, Ramadhan Issa Kipaya na Mkuu wa Idara ya Vitambulisho Pemba, Hamad Shamata Hamad.
Watakaohusika kujiandikisha ni wenye vyeti vya kuzaliwa, na wakishapata vitambulisho hivyo watajiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, ambalo uandikishaji wake umesitishwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kutokana na vurugu zilizojitokeza wakati wa uandikishaji.
Kulingana na ratiba hiyo, inaonesha kuwa Jumatano na Jumanne wiki ijayo uandikishaji utafanyika shehia za Kambini na Kiuyu Minungwini, wakati siku mbili zinazofuata itakuwa Kiuyu Kigongoni na Ole. Agosti 21 na 22 itakuwa Mjini Ole na Kangani, wakati siku mbili baadaye itakuwa Piki na Mzambarauni Takao, huku Agosti 26 na 27 itakuwa Mtambwe Kusini na Kaskazini.
Agosti 28 na 29 itakuwa Kisiwani na Limbani na Agosti 31 na Septemba mosi itakuwa Jadida na Kipangani, wakati Septemba 2 na 3, itakuwa Pandani na Selemu na siku mbili zitakazofuata itakuwa Utaani na Bopwe. Kwa mujibu wa ratiba, Septemba 7 na 8 itakuwa Kizimbani na Fundo, siku mbili zitakazofuata, itakuwa Gando na Ukunjwi, huku Junguni na Mchangamdogo ikiwa ni Septemba 11 na 12.
Kulingana na ratiba hiyo, Maziwani na Kojani A itakuwa Septemba 14 na 15, ambapo siku mbili zitakazofuata, itakuwa Kiungoni na Pembeni, ambapo Shengejuu na Mpambani itakuwa Septemba 18 na 19 na shughuli hiyo itahitimishwa Septemba 25 na 26 kwa shehia za Chwale na Kinyikani.
Hata hivyo licha ya ratiba hiyo, bado jana kulionekana baadhi ya wananchi wakiwa katika makundi wengine waking'ang'ania kutaka wapewe vitambulisho hivyo kwenye ofisi hiyo hiyo ya Mkuu wa Wilaya.
Utaratibu wa awali ingawa ulikuwa mzuri, lakini ulipata upinzani kutoka kwa baadhi ya viongozi wa CUF waliodai una usumbufu mkubwa na kuzua zogo, kwamba baadhi ya wananchi wananyimwa fomu za kuandikishwa hasa wasiokuwa na vyeti vya kuzaliwa.
Hata hivyo Jumanne wiki hii, akizungumza katika mkutano na viongozi wa kisiasa, masheha na baadhi ya watendaji wa Serikali, Mkurugenzi wa Idara ya Vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi, Mohammed Juma Ame, aliwataka wasio na vyeti vya kuzaliwa waende mahakamani waape na kupewa fomu za kuandikishwa.
Uandikishaji wa vitambulisho vya Mzanzibari Mkazi ulianza mwaka 2005, lakini baadhi ya wananchi walikuwa hawajitokezi kuchukua fomu kwa vile masuala ya Serikali yamekuwa hayapewi kipaumbele kisiwani hapa na hayaungwi mkono.
Pemba asilimia kubwa ni wafuasi wa CUF. Lakini baada ya kutolewa tamko kwamba wasio na vitambulisho hawataingia kwenye Daftari, sasa mwamko umekuwa mkubwa, kila mtu akitaka kujiandikisha na kusababisha vurugu katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya, ambazo ndizo zinatoa vitambulisho, wakati shehia zinatoa fomu za kupata vitambulisho hivyo.
http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=3192