CCJ's Statement to the Diplomatic Corps

Mwanafalsafa.... CCM wamekuwa wakiwashinda wapinzani kwa mkakati tu hakuna wizi wala nini; safari hii na sisi tutawafunga kwa mkakati hivi hivi... goli ambalo tutawafunga litakuwa ni goli la kihistoria....

I wish Mzee MM statements kama hizi zingekuwa classified kwa sasa, Unakumbuka CUF walipokuwa wanatishia jino kwa jino, hapakaliki, damu itamwagika, statement kama zile ziliwafanya waoga wa CCM kuandaa vita na raia wake na wakati wa uchaguzi mwaka 2000, waliweka ulinzi wa kufa mtu, CUF hawakufanya vurugu japo walinyang'anywa ushindi wakaja fanya january 26 na 27 2001 na kusababisha maafa ambayo impact yake kwenye uchaguzi ilikuwa ndogo. Kama mambo yale yangefanyika kwenye uchaguzi yangevutia hisia za kimataifa na pengine leo hii tungekuwa na serikali ya mseto zanzibar kama Kenya.

Mtazamo ni kuwashitukiza: Yaani washitukie kitu kimejaa wakati wanatafuta mbinu za kukitoa kinazidi kujaa mpaka wanakubali yaishe.
 
If the plan is to have long term impact in the politics of Tanzania, and probably Tendwa under the influence of some ruling elite deny CCJ the registration, the focus in my opinion should be in building the alternative party that people are zesting to see.
Sometimes even in decisive battles, withdrawing from the battle front, could be a winning tactic and not a defeat.
 
STATEMENT TO THE DIPLOMATIC CORPS AND CIVIL ORGANIZATIONS CONCERNING THE POLITICIZATION OF THE PROCESS OF PERMANENT REGISTRATION OF CHAMA CHA JAMII.
JUNE 11, 2010
As soon as the news of the formation of CCJ was leaked to the media earlier this year as many of you now know the ruling party and some government officials have spoken with one voice to deny transitional and permanent registration to CCJ. This was done with one goal in mind which is to deny CCJ any possible participation in the upcoming elections later this year.

Given.

Richard Kiyabo
Chairman, Chama Cha Jamii (CCJ)
Mambo mengi kuhusiana na chama hiki bado hayeleweki:
1. Chama hiki kimeundwa kwa lengo kuu la kushirik uchaguzi wa mwaka huu?
2. Kwanini kilianza kuonekana kama vile ni chama maarufu kabla hata hakijaundwa na sasa kabla hata hakijasajiliwa?
3. Je kuna faida gani kubwa kwaCCJ kung'ang'ania usajili kabla hata hakijafahamika kwa watu?

Nadhani CCJ kingeendelea kujilea na kukua kitakuwa na kila sababu ya kuingia kwenye mapambano na wakati huo kitakuwa kimeufahamu uwanja ukoje
 
Samahani jamani post yangu
Hatimaye mmetia team kwa mabalozi, nice move.

Mwkjj acha kupotosha watu kwa makusudi ama kuto kujua kuhusu madudu yaliofanywa na viongozi wako wa CCJ,
Watu wanakuuliza hoja nzito lakini unajibu majibu mepesi kwa hoja nzito au unauliza swali badala ya kujibu swali, na kukwepa kujibu hoja za msingi.
Inaonekana unapinga sana swala la kadi tu,na hautaki kujibu ya kushindwa hata kuratibu watu wafike 200 tu hapa dar, idadi haikutimia,wengine hata vitambulisho vya kura hawakuwanavyo achilia mbali la kadi za chama.
Hebu kwanza nijaribu kukuweka sawa kwa hili la kadi,maana limekaa kisheria zaidi kuliko porojo za siasa wewe na viongozi wako mnaotuletea.
Kwa kuanza tujiuliza ,Hivi "mwanachama" wa chama cha siasa ni nani?,nani anawajibu wakumfanya mtu kuwa "mwanachama"?,je sheria inasemaje kuhusu ili?,mwisho inakuwaje kadi inaingia katika uhakiki wa CCJ?.

Mwanachama wa chama cha siasa ni mtu aliyetimiza masharti na sifa zote za uanachama kwa mujibu wa katiba ya chama husika.

Ni chama cha siasa husika ndicho chenye mamlaka ya kumfanya mtu kuwa mwanachama baada ya kutimiza masharti na sifa zote za uanachama.

Sheria ya vyama vya siasa ibara ya 9 ina ainisha wakati wa usajili wa muda,in general uanachama uwe wa hiari bila kuwa na ubaguzi wa aina yoyote
Ibara ya 10 ktk usajili wa kudumu ina ainisha chama kiwe na "wanachama" wenye kujiandikisha kura 2000 kutoka......................... ukisoma kwa makini utaona sheria inazungumzia "mwanachama" mwenye kujiandikisha kura. je nisifa zipi zinazo mfanya akawa "mwanachama"?. Kujiandikisha kupiga kura ni swala la pili,lakini huyu "mwanachama"anayetamkwa na sheria ni nani?.
Kwa CCJ huyu ndie "mwanachama" anayetamkwa na Sheria ya vyama vya siasa.

UANACHAMA
8. Sifa za Mwanachama:
1
awe ni raia wa Tanzania;
2
awe na umri usiopungua miakakumi na nane;
3
awe na akili timamu;
4
awe anaikubali, anaiamini nakuitii Katiba ya CCJ na Kanunizilizotungwa chini yake;
5
AWE NA KADI iliyolipiwa adastahili za Chama;
6
asiwe mwanachama wa chamakingine cha siasa;

Hiyo ya uanachama wa itikadi ni sifa no4, Mkjj na hii ni kwa mujibu wa katiba ya CCJ uliotumwagia humu janvini.
Mtu akipungukiwa na sifa mojawapo ya hizo 6 basi si "mwanachama"kwa mujibu wa katiba ya CCJ, na anakua si "mwanachama" anayetamkwa ktk Sheria ya vyama vya siasa.
Kujiandikisha kupiga kura peke yake si uanachama unaotamkwa na Sheria ya vyama vya siasa.sheria inasema huyu "mwanachama"awe kajiandikisha kupiga kura. Kwa maana nyingine unapaswa kutimiza masharti kwanza ya "uanachama"kuwa "mwanachama"wa chama husika alafu ndio uwe umejiandikisha kupiga kura ili uhakikiwe kwa mujibu wa Sheria ya vyama vya siasa.
Kila chama kina masharti yake ya uanachama,lakini ilimradi ukitimiza masharti ya uanachama wa chama husika na ukawa na kitambulisho cha kura basi wewe ndie unayetamkwa na Sheria ya vyama vya siasa.

Sasa swala la kadi CCJ ni sifa mojawapo ya uanachama,ukipoteza sifa mojawapo ya hizi 6 then wewe si mwanachama wa CCJ kwa mujibu wa katiba ya CCJ. Hapa ndipo ulazima wa kadi unapokuja kwa CCj.
Tujiulize hivi ukipoteza sifa no1 utakua mwanachama?, vipi no2 au no3,unapaswa kuwa na sifa zote ili uwe mwanachama wa CCJ.
Hapa ndipo tunahoji umakini wa hawa viongozi wa CCJ wasijua hata "mwanachama"ni nani? anatakiwa kuwa na nini wakati wa uhakiki wakati katiba wametunga wao wenyewe, nakuziweka mikobani na kishia kukusanya watu hovyo tu na kihuni huni tu, idadi ndogo.wengine hata kitambulisho cha kura hawana,kadi za uanachama hawana na kushindwa kuratibu watu 200 tu hapa dar. AIBU.
Mkjj kudai tu ohhh msajili anatuonea,alisema hana hela sasa katoa wapi?,wapi kadi imetajwa ktk katiba nadhani ni uelewa wenu mdogo tu katika kufasiri sheria. Msajili anahaki yakuomba mambo mengi tu wakati wa uhakiki ikiwemo cheti cha kuzaliwa kama anamashaka na umri wa mwanachama,vivyo hivyo kwa uthibitisho wa uraia,hata cheti cha daktari kama anamashaka na utimamu wa akili ya mwanachama nk, je hayayote yatamkwe ktk katiba?.
Katiba ni sheria mama inayotoa miongozo kwa sheria na taratibu zingine, katiba haiwezi kutaja kila kitu utakavyo wewe, vinginevyo tungekuwa na katiba yenye kurasa zisizo na idadi.
Sina matatizo na CCJ kama chama cha siasa na sera zao, nina tatizo nao na huu upuuzi wa kutokua makini na mambo yao na kukimbilia kulaumu pasipo mantiki yoyote hadi kwa mabalozi.
Kuwa upinzani si mara zote kuwa sahihi,na kua na serikali onevu si kigezo cha kutetea uozo unaofanywa kizembe naCCJ kwa kufanya mambo kwa kukurupuka bila kujipanga.
Mkjj siasa za bongo sio lelemama kama mlicho kifanya mwembe yanga, tena baada ya kumshinikiza msajili navitisho na mbwembwe nyingi kuwa mtamkopesha kama hana hela ya uhakiki.
Mwisho wasiku huwezi amini madudu yaliyotokea pale, utadhani hawakujua kuna uhakiki, Kisha watu kama Mkjj wanakuja kutuaminisha kwa nguvu zao zote kuwa uliotokea pale ni uonezi, wanataka kutuaminisha rangi ya njano tuone nyukundu wakati watu wote tunaona njano ila wao wanasema nyekundu,labda mabalozi wanaweza kusaidia.
Nadhani watu wengi humu janvini wameshauri vizuri sana, CCJ watambue walipojikwaa,warudi nyuma kujipanga upya vizuri,Mtu kama Mkjj anatumia nguvu nyingi na uwezo wake mkubwa kujengea hoja uozo wa viongozi wake. namuheshimu sana kwa uwezo wake wa kujenga hoja za maana katika mambo ya maana, lakini kwa hili amechemka mbaya. Atumie uwezo wake huo kuwashauri viongozi wake natumai watapata tu usajili wakudumu.
Kupeleka mahakamani issue ya kadi au kwa mabalozi mimi sioni busara yake ipo wapi.kwani kuchapa kadi sh ngapi jamani?. Kunamambo mengi ya kushughulika kama chama ili kupata usajili, na si kukimbilia mahakama au mabalozi kisa kadi
Hebu pateni kwanza huo usajili wa kudumu mje ulingoni kuona jinsi rafu zinavyo chezwa huku ktk chaguzi,ni balaa nini kadi bwani?.
Acheni ubabaishaji ebu nendeni mkatengeneze kadi mje ulingoni tena tunawataka sana mje kufungua kesi zenye msingi huku ulingoni sio huko nje ya ulingo

But i m sorry to tell you that mmechelewa kwa uchaguzi huu mlipata bahati mkaipiga mateke.
Mabalozi hao kilasiku wanaisifu nchii mnategemea nini. usajili hamja nyimwa ninyiwenyewe mmesitisha zoezi
Au issue ya wale mashoga Malawi imewapa hamasa kuwa wafadhili kupita balozi zao watashinikiza. good try
 
Mzee Mwanakijiji,

Kama sijakosea,ulikuwa pamoja na CHADEMA na kushawishi watu watoe support kadri inavyowezekana ili kukipa nguvu chama hicho kilichokuwa chapewa sifa pekee ya siasa za kweli,wazi na makini za kuweza kuing'oa CCM.Recently,u r backing another new political party...ambacho kwa kweli kimepambwa na sifa kemkem za kupendeza.

Hii political flip-flop imekaaje?Kwangu mimi ndio nazidi kukosa uaminifu na siasa hususwan za Afrika.Kibaki aliingia kwa kishindo cha mapinduzi Kenya,akawauzia watu karanga,akashindwa uchaguzi..akanyang'anya madaraka.Kenya kuna hata HQ ya UN in Africa,achilia mbali balozi nyingi ambazo hapa Tz hakuna,lakini hawakusema lolote...jamaa anaendelea kupeta.Mpinzani wake nae kapewa shibe....nae katulia.Utakubali vipi kujiunga na serikali ambayo imefanya dhulma ya kura mchana kweupe,hata commissioner wa tume anakiri kulikuwa na fraud na hajui ni vipi Kibaki alishinda?

Nadhani inabidi nichukue muda nile shule kidogo kuhusu politics....maana sielewi wht goes on in it.....ni ngumu sana kuni convince kuhusu aina yetu ya politicians..husuwan wa nyumbani Africa
 
I wish Mzee MM statements kama hizi zingekuwa classified kwa sasa, Unakumbuka CUF walipokuwa wanatishia jino kwa jino, hapakaliki, damu itamwagika, statement kama zile ziliwafanya waoga wa CCM kuandaa vita na raia wake na wakati wa uchaguzi mwaka 2000, waliweka ulinzi wa kufa mtu, CUF hawakufanya vurugu japo walinyang'anywa ushindi wakaja fanya january 26 na 27 2001 na kusababisha maafa ambayo impact yake kwenye uchaguzi ilikuwa ndogo. Kama mambo yale yangefanyika kwenye uchaguzi yangevutia hisia za kimataifa na pengine leo hii tungekuwa na serikali ya mseto zanzibar kama Kenya.

Mtazamo ni kuwashitukiza: Yaani washitukie kitu kimejaa wakati wanatafuta mbinu za kukitoa kinazidi kujaa mpaka wanakubali yaishe.

Nakubaliana nawe. CCJ wamekuwa wakifanya makosa kadha wa kadha ya ki-'intelijensia' wakati wanajua 'mahasimu' wao hawataki/hawapendi ushindani wa kweli. Naelewa kwamba Mzee Mwanakijiji anajitahidi kwa kadri ya uwezo wake kudhihirisha nia njema ya chama kipya cha CCJ na katika kufanya hivyo inamlazimu aje na maelezo ambayo anategemea yatawafanya watu wasiotaka kuelewa waelewe kwamba CCJ ni chama makini chenye mikakati thabiti. Lakini, adui ukishamwambia mbinu unazodhamiria kutumia na yeye atatafuta mbinu zingine dhidi ya mbinu zako ulizobainisha.

Viongozi na wanachama wa CCJ wasife moyo maana ni haki yao ya kidemokrasia kuunda chama cha siasa kwa mujibu wa Katiba ya nchi yetu. Iko siku haki itashinda udhalimu.
 
Duh Mkuu nafkili ulidhamiria kumtaja Ngambo Ngali..!

Sure, asante mawazo matatu mzigo huu ni wangu, lakini jibu kwa Mwanakijiji ni kuwa moja hakuna maamuzi yasio ya kimahakama ambayo ni final.

Maamuzi yoyote ya kiutawala yanaweza kupingwa mahakamani. Maamuzi ambayo ni final ni yale tu ambayo yanafuata mlolongo wa mahakama vinginevyo administrative decision yoyote inaweza kuwa challeged.

Issue ya pili inaweza kuwa sababu fika ya kuchallenge kwa sababu mwanzo alisema hana hela ya kufanya uhakiki, lakini baadaye hakuwaambia wananchi kuwa amepata hela na kama amepata amepata wapi kumuwezesha kuendelea na uhakiki. Badala yake anendelea na uhakiki in a negative way.
 
kwenda kwa mabalozi wana CCJ wananikumbusha "KUMBATIO LA MWENYE MAKOSA"
 
tatizo ni kuwa mnafikiri tumepoteza pambano...!!!

Mkuu,nadhani wanaofikiri mmepoteza pambano wanasukumwa na ukweli kuwa "timu inayoshindwa kujipanga yenyewe kabla ya pambano,eg ktk soka kushindwa kutengeneza starting line up,imeshajitengenezea kushindwa katika pambano."

Hivi,muda huu tungekuwa bado tunazungumzia usajili laiti CCJ wangekuwa wamejipanga vizuri na kuwaandaa hao wanachama wao (kama kweli wapo) na kadi kwa ajili ya uhakiki?
Yah,pengine Tendwa anatumiwa na CCM lakini CCJ yenyewe "imemrahisishia mazingira ya kuwahujumu" kwa vile laiti idadi ya wanachama wa kuhakikiwa ingetimia sambamba na mahitaji yote kutimizwa,Tendwa angekuwa 'mchawi alopewa mtoto alee",na sidhani kama angekuwa na kisingizio cha kuinyima CCJ usajili wa kudumu.

Mwanakijiji,ushauri wa bure kwenu ni huu: kama hamdhani kuwa ushauri wa bure tunaowapa (kuwa mrekebishe kasoro zenu na kujipanga vizuri zaidi) hauna maana,basi la busara zaidi lingekuwa kwenda mahakamani.Na pengine haihitaji hata busara kuelewa kuwa haki haitolewi na mabalozi au nchi wahisani bali mahakamani.Kama mnaota kuwa kuzungukwa katika balozi na taasisi mbalimbali za kimataifa kutamlazimisha Tendwa awapatie usajili,you could as well wish for JK to be your presidential candidate.Sanasana hao mabalozi watawashauri kama tunavyowashauri sie kuwa NENDENI MAHAKAMANI KAMA MNAAMINI TATIZO SI UZEMBE WENU BALI MMEONEWA.

Haki haipatikani kwa kulialia au kulalamika bali kuidai.Na mahala pa kudai haki sio balozini bali mahakamani.By the way,Tendwa keshawaambia hana muda wa kubishana nanyi na kuwashauri kwenda mahakamani (na mlishatishia kwenda huko lakini bado mnasuasua).
 
Hata TANU wakati inagombea uhuru haikukubalika na watawala. CCM waendelee tu lakini siku yao ya arobaini iko njiani huwezi kuwanyima haki walipa kodi. Muda upo sana kwa walipa kodi na mafedhuli wote waliovaa ngozi ya kondoo watapata malipo hapa hapa duniani. Dunia siku zote inazunguka.
 
Mkuu,nadhani wanaofikiri mmepoteza pambano wanasukumwa na ukweli kuwa "timu inayoshindwa kujipanga yenyewe kabla ya pambano,eg ktk soka kushindwa kutengeneza starting line up,imeshajitengenezea kushindwa katika pambano."

Hivi,muda huu tungekuwa bado tunazungumzia usajili laiti CCJ wangekuwa wamejipanga vizuri na kuwaandaa hao wanachama wao (kama kweli wapo) na kadi kwa ajili ya uhakiki?
Yah,pengine Tendwa anatumiwa na CCM lakini CCJ yenyewe "imemrahisishia mazingira ya kuwahujumu" kwa vile laiti idadi ya wanachama wa kuhakikiwa ingetimia sambamba na mahitaji yote kutimizwa,Tendwa angekuwa 'mchawi alopewa mtoto alee",na sidhani kama angekuwa na kisingizio cha kuinyima CCJ usajili wa kudumu.

Mwanakijiji,ushauri wa bure kwenu ni huu: kama hamdhani kuwa ushauri wa bure tunaowapa (kuwa mrekebishe kasoro zenu na kujipanga vizuri zaidi) hauna maana,basi la busara zaidi lingekuwa kwenda mahakamani.Na pengine haihitaji hata busara kuelewa kuwa haki haitolewi na mabalozi au nchi wahisani bali mahakamani.Kama mnaota kuwa kuzungukwa katika balozi na taasisi mbalimbali za kimataifa kutamlazimisha Tendwa awapatie usajili,you could as well wish for JK to be your presidential candidate.Sanasana hao mabalozi watawashauri kama tunavyowashauri sie kuwa NENDENI MAHAKAMANI KAMA MNAAMINI TATIZO SI UZEMBE WENU BALI MMEONEWA.

Haki haipatikani kwa kulialia au kulalamika bali kuidai.Na mahala pa kudai haki sio balozini bali mahakamani.By the way,Tendwa keshawaambia hana muda wa kubishana nanyi na kuwashauri kwenda mahakamani (na mlishatishia kwenda huko lakini bado mnasuasua).

wamechungulia mahakamani wakaona parefu, ndio maana wameona watest zari kwa mabalozi ili angalau wasitoke masikioni mwa watu kupitia media
 
Mwanafalsafa.... CCM wamekuwa wakiwashinda wapinzani kwa mkakati tu hakuna wizi wala nini; safari hii na sisi tutawafunga kwa mkakati hivi hivi... goli ambalo tutawafunga litakuwa ni goli la kihistoria....

Mkuu,inaelekea CCJ ni kama mjumuiko wa malaika kwani kila jambo linaloihusu linatajwa kuwa "la kihistoria".Tuliambiwa CCJ wana "ajenda ya kipekee" (au ya kihistoria) na sasa tunaelezwa tutarajie chama hicho kifunge bao la kihistoria.

Wasiwasi wangu ni kuwa historia haiko upande wenu.Kuna mangapi ya muhimu yalitokea huko nyuma,na mabalozi na nchi zao wakaishia kuuchuna tu?Hebu jiulize,kama wanakuwa wapole hata pale fedha za walipakodi wao (misaada wanayotupatia) unategemea wawe mbogo kwa vile CCJ wamenyimwa usajili?Kama hawajaweza kuchukua hatua katika wizi wa mabilioni huko Tanroads (inayotegemea fedha za wafadhili),trilioni moja na ushee ya economic stimulus package ya kisanii,mauaji ktk uchaguzi znz (ambayo yalipelekea wafadhili hao "kubeba mzigo wa wakimbizi" hadi leo),na mifano mingine kadha wa kadha,kipi hasa cha kukuaminisha Mwanakijiji na CCJ yenu kuwa mabalozi watawawezesha kufunga bao hilo la kihistoria?

Mkuu,angalia isijekuwa bao pekee la kihistoria likawa ni katika reputation yako (ambayo umeamua kuiweka on the firing line kwa sababu unazojua mwenyewe).Nahofia kuwa laiti utapokuja kutambua kuwa tunachosema sasa kina ukweki kuhusu CCJ unayoiamini kupindukia,itakuwa too late.Imekuchukua muda mwingi na nguvu nyingi (plus kuzalisha maadui wengi) kufika ulipo sasa.Sidhani kama ni jambo la busara kuhatarisha reputation yako kwa ajili ya cause hii ya CCJ,ambayo imejaa blah blah na ubabaishaji kuliko wanavyokuaminisha.Wanafahamu unataka nini,nao wanakupatia kile roho yako inapenda.Unfortunately,same tricks zimekuwa zikitumiwa na CCM: feeding hungry and poor Tanzanians with what they are dying to hear.

It's not too late,Mkuu.
 
Hata TANU wakati inagombea uhuru haikukubalika na watawala. CCM waendelee tu lakini siku yao ya arobaini iko njiani huwezi kuwanyima haki walipa kodi. Muda upo sana kwa walipa kodi na mafedhuli wote waliovaa ngozi ya kondoo watapata malipo hapa hapa duniani. Dunia siku zote inazunguka.

Mkuu hakuna asiye juwa kuwa CCM wana hila sana, wala watu hawasemi CCM pamoja na msajili wake wanavitendea haki vyama ikiwemo chama kitarajiwa CCJ, Hapa tatizo ni CCj wenyewe jinsi walivyokuja ni tofauti na matarajio ya wengi. wapo too soft in almost everthing, wanaonekana wamekurupuka tu bila kujipanga vizuri, siasa za Nchi zetu silelemama hasa kama unamjua adui yako yukoje hupaswi kumpa nafasi kama wao walivyo fanya pale mwembe yanga, this is not a party, this is batlle. ili kumpokonya mtu tonge yabidi ujizatiti mkuu.
 
duh.. I wish I could tell you whats up to give you hope.. but for now I can't but keep hope alive... you have to be in warfare mode... have you ever read "The Art of War"? Things are not what they seem.... Don't quit on me now...

Next week.. CCJ has some appointments with some "influential" ambassadors to Tanzania..

You have to learn to push when the government say "no".. otherwise.. they will push you out completely..

Thanks Mkuu, lets be patient and remain strong in this war zone.
I am sure something will work out for good.

Amandla.
 
Hivi hamjiulizi kwanini Msajili alisema hana "bajeti" ya kufanya uhakiki, na Marmo siku moja kabla akarudia hivyo hivyo na kesho yake wakakubali kufanya uhakiki? Hakuna chombo cha habari kilichomuuliza Tendwa "imekuwaje tena" au "fedha za uhakiki" umezitoa wapi?.
[/QUOTE]
Mzee Mwanakijiji, Kwa Tendwa kutoulizwa swali hili, ni uthibitisho hawa ndio waandishi wa Tanzania, na hizi ndizo media zetu. Ndio maana watu walikuwa wakisubiria kile kijarida cha 'Cheche' na kusikiliza podcast ya Mwanakijiji. Kama wale wengine wote uliweza kuwapata mpaka Waziri Mama Mipasho, huyu Tendwa mnamshindwa nini?.
 
STATEMENT TO THE DIPLOMATIC CORPS AND CIVIL ORGANIZATIONS CONCERNING THE POLITICIZATION OF THE PROCESS OF PERMANENT REGISTRATION OF CHAMA CHA JAMII.
JUNE 11, 2010

Since the re-introduction of multiparty democracy in Tanzania in 1992 the government of Tanzania which is under Chama Cha Mapinduzi has worked to frustrate the process of peaceful democratization of political institutions in Tanzania. Among them are the Office of the Registrar of Political Parties and National Election Commission. As a result of this the ruling party has only given tokens of independence to these institutions while at the same time it has continued to deny true freedom to function without interference from state organs or political operatives.

As soon as the news of the formation of CCJ was leaked to the media earlier this year as many of you now know the ruling party and some government officials have spoken with one voice to deny transitional and permanent registration to CCJ. This was done with one goal in mind which is to deny CCJ any possible participation in the upcoming elections later this year.


Knowing fully how the political mechanisms in Tanzania work we have tried to demand fairness and transparency when it came to the registration of our party. We didn't expect anything more or less than what has been required in past registrations of political parties. Unfortunately, from the beginning of this process, the Office of the Registrar of Political Party Mr. John Tendwa under the Minister of State (Parliament and Political Affairs) Hon. Philip Marmo has continually and methodically tried to prevent the formation and eventual permanent registration to our political party. They have been joined several times in this sentiment by a number of high ranking political leaders in their party.


The highlight of this frustration came last week at what should have been a clear and open process of validation of our members. Unfortunately as expected, the Registrar purposefully applied very different standards which could be seen as unconstitutional when rejecting some of our members. The law put very simple standards (Political Parties Act of 1992 S 10) for permanent registration of political parties none of which seem to have been of interest to the Registrar except the standards that he invented or those created by the Minister – a political appointee of the President and staunch cadre of the ruling party.


For this reason, we ask you our democratic partners to urge and demand fairness and impartiality as far as the registration of our party and others in the future. Even more, we ask to join our voices in your own ways to demand the creation of true independent government entities that deal with the registration of political parties and supervise elections in Tanzania. As most of you have been our partners in development through the years we believe history is calling you now with a loud and an ambiguous voice to be our partners in democracy, justice, fairness, and equality. You should not support in anyway a government that is devoid of those sentimental but very necessary values in any democratic society.


To a better, freer, prosperous and democratic Tanzania.



Given.




Richard Kiyabo

Chairman, Chama Cha Jamii (CCJ)

Mzee Mwanakijiji, Statement nimeiona, ila nina mashaka kama kweli imepelekwa kwa hizo balozi. Ninarafiki yangu mmoja, yeye ni Mshauri wa Siasa kwenye moja ya balozi kubwa humu nchini, amenithibitishia barua hiyo yenu ya CCJ, haijafika ubalozini kwake.

Nakushauri Mzee Mwakijiji, kwa heshima yako uliojijengea hapa JF na kwingineko, kuwa makini sana na hii CCJ, isije kukuvunjia heshima hiyo ukaishia kuoneka kituko.

Lile la wanachama ni uzembe, hili la barua tusema bado iko posta haijapelekwa tangu ile Ijumaa, isikuwa wanakuzuga wewe na wafadhili wao kuwa barua tumepeleka, in actual fact hawajapeleka popote kama wale wanachama wenu wa kiitikadi.
 
Unfortunately as expected, the Registrar purposefully applied very different standards which could be seen as unconstitutional when rejecting some of our members. The law put very simple standards (Political Parties Act of 1992 S 10) for permanent registration of political parties none of which seem to have been of interest to the Registrar except the standards that he invented or those created by the Minister – a political appointee of the President and staunch cadre of the ruling party.

Makes you wonder why no details of claimed "very different standards" are mentioned in this statement. Mambo ya msingi na rahisi kabisa kama kuelezea kiundani na kutoa mifano ya ni namna gani au vipi haswa hawakutendewa haki wameshindwa ku-document zaidi ya blah blah blah. Kulialia kwa Wazungu hakutasaidia chochote kwa kweli. Ni kujiharibia zaidi tu.
 
mawazomatatu, mahakama haiwezi kuingilia maamuzi ya msajili. Sheria iko wazi uamuzi wa msajili ni final.


Hivi hamjiulizi kwanini Msajili alisema hana "bajeti" ya kufanya uhakiki, na Marmo siku moja kabla akarudia hivyo hivyo na kesho yake wakakubali kufanya uhakiki? Hakuna chombo cha habari kilichomuuliza Tendwa "imekuwaje tena" au "fedha za uhakiki" umezitoa wapi? Mabalozi wako interested kuona CCJ inatendewa haki kwani toka mwanzo wameona haijatendewa haki na suala la kadi ni dogo tu ambalo wao wamelitumia. Kama kila mtu angekuwa na kadi msajili asingezikubali vile vile kwa sababu majina yanaweza kuwa yamekosewa, jina la mtaa halikuwa sahihi, au kadi haina picha n.k!

Msajili hakuwa na hana interest ya kutenda haki. Tumempa nafasi ya kuwa impartial na ameshindwa.

Sasa basi lazima utafutwe mbadala, kupoteza pambano sio kushindwa vita na kupoteza pambano sio vibaya vibaya ni kushindwa vita.
[/QUOTE]
Naona sheria hii inayo mpa mamlaka msajili kuwa uamuzi wake ni wa mwisho , kisheria ni tatizo hivyo uamuzi wake unaweza kupingwa, hili ni suala jingine la kikatiba ambalo chama tuwala wanatumia kukandamiza demokrasia, ni katika nchi yoyote yenye kufuata utawala wa sheria uamuzi wa juu kabisa ambao hauwezi tenguliwa na wa mahakama ya rufaa kwa tanzania na nchi nyingi, labda uamuzi wa Raisi ndio unaweza kuwa final.
kumbuka nguzo tatu za nchi/serikali Judicial, Bunge na Raisi , lakini anaye cheza balance role ni mahakama zaidi kuliko hizi institution nyingine
 
Back
Top Bottom