CC ya ANC imemfukuza Julius Malema uanachama

commonmwananchi

JF-Expert Member
Mar 12, 2011
3,377
1,952
kwa mujibu wa taarifa ya habari ya BBC swahili,asubuhi hii.wamefikia uamuzi huo baada ya kumtuhumu kukigawa chama kwa hatua yake ya kuwatuhumu baadhi ya vigogo ndani ya chama kwa mambo mbalimbali,pia ikiwemo kutoa matamshi ambayo yamekuwa yakipingana na viongozi wa chama chake katika siasa za ndani na kimataifa.

Kwa ujumla suala hili limeshabihiana na kwa kiwango cha juu na yanayoendelea hapa kwetu hususan ndani ya CCM. kati ya Nape nnauye na baadhi ya vigogo ndani ya chama chake kuhusiana na suala la ufisadi.

My take.
Niliwahi kumueleza Nape Nnauye humu ndani ya JF kuhusiana na suala hili hili na nilimpa mfano wa Julius Malema huyuhuyu, nikimshauri kwamba kama ana nia thabiti ya kupambana na ufisadi ndani ya chama chake basi achukuwe hatua thabiti na uamuzi muhimu na mgumu kwa kuhamia chama kingine cha upinzani na kuendeleza mapambano ya kweli.

Katika majibu yake kwangu Nape, hakugusia swali hili bali alinijibu maswali mengine tu ambayo nilikuwa nimemuuliza,pamoja na hili. Sasa imekuwa hivi kwa Julius Malema, kwa vile misimamo yao ilikuwa inashabihiana (ingawa sina uhakika kama kweli Nape ana nia thabiti kama Malema) ndio maana narudia kumuuliza tena.

Je anasemaje kuhusiana na hili?
 
Sasa inabidi Lowassa asome alama za nyakati, kibali cha kumvua gamba NEC walishakitoa kwa CC siku ile alipokuwa akililia kwenye NEC kwamba mwenyekiti bila mzee Mkapa hata wewe usingekuwako hapo, yale yalikua ni maneno ya mfa maji kwa kuwa alijua NEC ambako aliwekeza sana watagoma kutoa kibali, sasa baada ya kuona NEC wamebariki suala lao kuvuliwa gamba liende CC akajua yametimia, mtu mzima yule anaona mbali kuliko wapambe wake humu.

Kurudi kwa Malema, yule kijana alijijengea kahimaya kake ndani ya chama ambako kalipambana sana kumfikisha JZ (Jacob Zuma) pale alipo, kijana nae kama Lowassa na genge lake akaanza kujiona mkubwa kuliko chama, anaweza kufanya lolote kwa kuwa mwenyekiti amewekwa pale na genge lake.

Kijana akaanza kutamani kumn'goa mwenyekiti ili akae yeye au amuweke mtu "wake". Mwenyekiti akasema eboo! huu utakua ujinga na siku zote mtu anakuwa mjinga wakati wa kwenda lakini wakati wa kurudi anajua pabaya na pazuri wapi na yeye apite wapi, ndio yamemkuta yaliyomkuta mambo pia hayo yatamkuta Lowassa.

Mzee wangu Lowassa soma alama za nyakati.
 
mwambieni na lowassa asome alama za nyakati,kibali cha kumvua gamba NEC walishakitoa kwa CC siku ile alipokuwa akililia kwenye NEC kwamba mwenyekiti bila mzee mkapa hata wewe usingekuwako hapo,yale yalikua ni maneno ya mfa maji kwa kuwa alijua NEC ambako aliwekeza sana watagoma kutoa kibali,sasa baada ya kuona NEC wamebariki suala lao kuvuliwa gamba liende cc akajua yametimia,mtu mzima yule anaona mbali kuliko wapambe wake humu.

Kurudi kwa malema,yule kijana alijijengea kahimaya kake ndani ya chama ambako kalipambana sana kumfikisha Jz Jacob Zuma pale alipo,kijana nae kama lowassa na genge lake akaanza kujiona mkubwa kuliko chama,anaweza kufanya lolote kwa kuwa mwenyekiti amewekwa pale na genge lake,kijana akaanza kutamani kumn'goa mwenyekiti ili akae yeye au amuweke mtu "wake",mwenyekiti akasema eboo huu utakua ujinga na siku zote mtu anakuwa mjinga wakati wa kwenda lakini wakati wa kurudi anajua pabaya na pazuri wapi na yeye apite wapi,ndio yamemkuta yaliyomkuta mabyo pia yatamkuta lowassa.

Mzee wangu Lowassa soma alama za nyakati.

Ni kweli unayoyasema.na kama umeona kuna thread humu ya tangu usiku wa leo ikitutaarifu jinsi wapambe wa Lowassa walivyonaswa na Rushwa kule Arumeru mashariki kwenye kinyang'anyiro cha kura za maoni ccm.
Na hii inathibisha usemi wako kwamba sasa ccm imeanza rasmi kumchoka EL,kwa kutoa maelekezo rasmi kwa vijana wa Hosea ili wakatimize kazi ya kuondoa Monduli team pale arumeru mashariki.
 
Mimi Nape nasema sisi ccm ningumu kufukuzana tuna utaratibu mzuri wa kulindana na kudeal na bongo za Watanzania kuwapoteza na kuwanyamazisha.
 
Too theoretical mkuu!

Tangu lini Nape ana nia ya dhati ya kupambana na ufisadi

Jengo la umoja wa vijana alipiga kelele na leo hii ninapoandika hapa amepewa vipasent fulani vya share


kwa kifupi ningekujibu.....umtalisha weye??
 
sitaki kumfananisha malema na zitto moja kwa moja..ingawaje fate ya zitto inaweza kuja kuwa sawa na malema..

Uko sawa,lakini kuna tofauti kidoogo kati ya wawili hawa.Zitto kabwe haaelewewki rasmi ni nini anachokubaliana nacho ndani ya chama chake bayana na ni nini hakubaliani nacho ndani ya chama chake.
Halafu pia,kuna suala la kutuhumiwa kutumika na kundi fulani kwa maqslahi fulani.lakini Julius malema alieleweka rasmi msimamo wake.
 
Huwezi kumfananisha Nape na Malema wa ANC lakini naweza kudiliki kumfananisha Ole Millya, yule vuvuzela wa Lowassa na Malema kwani yeye anawadharau viongozi wengine wote wa chama chao kasoro Lowassa; na tabia yake hiyo ya kuwatishia viongozi wake wa juu ili wafuate yale aliyotumwa na Lowassa kusema [kwamba cc lazima irudishe jina la SIOI kugombea Arumeru ama sivyo ccm ingeshindwa] ni dharau moja kwa moja kwa cc ya ccm!!Huyu kijana anatakiwa achukuliwe hatua za kinidhamu ama sivyo atakuwa kirusi kwa ccm!!
 
Huwezi kumfananisha Nape na Malema wa ANC lakini naweza kudiliki kumfananisha Ole Millya, yule vuvuzela wa Lowassa na Malema kwani yeye anawadharau viongozi wengine wote wa chama chao kasoro Lowassa; na tabia yake hiyo ya kuwatishia viongozi wake wa juu ili wafuate yale aliyotumwa na Lowassa kusema [kwamba cc lazima irudishe jina la SIOI kugombea Arumeru ama sivyo ccm ingeshindwa] ni dharau moja kwa moja kwa cc ya ccm!!Huyu kijana anatakiwa achukuliwe hatua za kinidhamu ama sivyo atakuwa kirusi kwa ccm!!
Sasa umesema kweli,na mimi hilo nimekwisha liona sana na huwa nashangaa sana ni kwa nini ccm haimchukulii hatua stahiki huyu kijana.
Kumbuka alisababisha mgogoro wa ufunguaji matawi ya uvccm mjini Arusha na bado hakuguswa na wakubwa ndani ya chama.
 
Mimi Nape nasema sisi ccm ningumu kufukuzana tuna utaratibu mzuri wa kulindana na kudeal na bongo za Watanzania kuwapoteza na kuwanyamazisha.
Muganyizi!
Wacha kusemea watu,wacha watu wajisemee wenyewe,Nape yumo humu ndani ya JF,nakuomba kama uko karibu naye kwa sasa ,mwambie afunguwe JF na aeleze jamii kuhusiiana na hili tumuelewe tena kwa nia nzuri tu.ahsante.
 
Back
Top Bottom