Pape
JF-Expert Member
- Dec 11, 2008
- 5,488
- 79
Nanukuu...
Mimi ni mfanyakazi wa kampuni fulani hapa Dar. Ni muajiriwa yapata miezi mi 4 sasa. Tangu nianze kazi hapo kuna dada ambaye ameonyesha kila dalili ya kutaka kuwa na mimi kimapenzi! Ninafamilia na watoto kwahiyo sipendi kujihusisha katika mambo kama hayo. Siku moja wakati wa sherehe ya kuwapongeza baadhi ya wafanyakazi huyu dada alinibana katika kona akataka kunibusu (busu kubwa) lakini nilimzuia na hakufanikiwa!
Siku mbili baadae nilipokuwa nikiingia kazini asubuhi kwa kutumia 'elevator' mambo yalikuwa sivyo kwani dada huyo aliingia katika 'elevator' ambayo mimi nilikuwemo kupitia floor ya 2! Kwabahati mbaya tulikuwa wawili tu! Baada ya kuingia na kuanza kuelekea floor ya 6 hapo katikati alinikumbatia ghafla huku akinibusu kwa lazima! Kitendo hicho kilinihuzunisha kwani halikuwa lengo langu pia nilijua mule ndani ya 'elevator' kuna kamera za ulinzi!!
Ilipofika saa kumi jioni mtu wa IT wa kampuni yetu alinipigia simu kwamba anamazungumzo nami na aliniambia kwamba ameona vyoote 'tulivyofanya katika elevator'
Ameniomba nimpe Tshs. 2.5M haraka iwezekanavyo ili aweke kapuni hizo picha na kama sivyo basi atazipeleka kwa bosi!!!
Sasa mimi uwezo wangu ni mdogo kwani hizo pesa sina...
Je, nikambembeleze huyu IT amezee? Nikajikamatishe kwa bosi na kumueleza ukweli? Je, mke wangu akijua itakuwaje kwani nashindwa namna ya kumuelezea!!
Naomba msaada wenu...
Mimi ni mfanyakazi wa kampuni fulani hapa Dar. Ni muajiriwa yapata miezi mi 4 sasa. Tangu nianze kazi hapo kuna dada ambaye ameonyesha kila dalili ya kutaka kuwa na mimi kimapenzi! Ninafamilia na watoto kwahiyo sipendi kujihusisha katika mambo kama hayo. Siku moja wakati wa sherehe ya kuwapongeza baadhi ya wafanyakazi huyu dada alinibana katika kona akataka kunibusu (busu kubwa) lakini nilimzuia na hakufanikiwa!
Siku mbili baadae nilipokuwa nikiingia kazini asubuhi kwa kutumia 'elevator' mambo yalikuwa sivyo kwani dada huyo aliingia katika 'elevator' ambayo mimi nilikuwemo kupitia floor ya 2! Kwabahati mbaya tulikuwa wawili tu! Baada ya kuingia na kuanza kuelekea floor ya 6 hapo katikati alinikumbatia ghafla huku akinibusu kwa lazima! Kitendo hicho kilinihuzunisha kwani halikuwa lengo langu pia nilijua mule ndani ya 'elevator' kuna kamera za ulinzi!!
Ilipofika saa kumi jioni mtu wa IT wa kampuni yetu alinipigia simu kwamba anamazungumzo nami na aliniambia kwamba ameona vyoote 'tulivyofanya katika elevator'
Ameniomba nimpe Tshs. 2.5M haraka iwezekanavyo ili aweke kapuni hizo picha na kama sivyo basi atazipeleka kwa bosi!!!
Sasa mimi uwezo wangu ni mdogo kwani hizo pesa sina...
Je, nikambembeleze huyu IT amezee? Nikajikamatishe kwa bosi na kumueleza ukweli? Je, mke wangu akijua itakuwaje kwani nashindwa namna ya kumuelezea!!
Naomba msaada wenu...