Can I change Him?

Hebu niambieni akina mama/dada wenzangu.Pengine nina rafiki nataka kupeleka mahusiano katika hatua nyingine labda ndoa tuseme.Na huyu mlengwa pengine ana tabia fulani au tuseme mazingira fulani ambayo nisingependa awe nayo katika hiyo level nyingine.
Kwa mfano ni mwizi/jambazi,mlevi,Fukara(hana hela wala kazi-naweza kusema ni mvivu) na mambo kama hayo.
Na pengine nishamwambia kuwa sipendi 1,2,3......ya hizo tabia na akaahidi kuwa atabadilika.
Vilevile katika interraction mbali x2 na marafiki hasa wanaume mara nyingi nimekuwa nikiwasikia wakisema kuwa MWANAMKE anauwezo mkubwa wa kumbadilisha na kumtengeneza mwanaume katika mahusiano the way anataka awe.
Sasa swali langu ni kuwa Is this true?
Wakina kaka pia mnaweza kuniambia eti mnaweza kubadilishwa na wanawake mkawa waume wema wenye kuonyesha mfano mwema?
Chrispin naomba usiingie kwenye hii thread inakuhusu

...huwezi kumbadilisha, ni yeye pekee mwenye uwezo wa kubadilika (akitaka.) Unachoweza kumsaidia ni 'kugundua' chanzo cha tabia zake mbaya. Jadiliana nae na tena akubali udhaifu wake, kisha mwenyewe ('labda' kwa msaada wako) aanze mkakati wa kubadilika kuelekea kiwango ambacho nyote mtaafikiana nacho.

Be patient ('Ukitaka.') Relationship's about compromising, tunatofautiana tabia, uwezo na maamuzi.
 
...huwezi kumbadilisha, ni yeye pekee mwenye uwezo wa kubadilika (akitaka.) Unachoweza kumsaidia ni 'kugundua' chanzo cha tabia zake mbaya. Jadiliana nae na tena akubali udhaifu wake, kisha mwenyewe ('labda' kwa msaada wako) aanze mkakati wa kubadilika kuelekea kiwango ambacho nyote mtaafikiana nacho.

Be patient ('Ukitaka.') Relationship's about compromising, tunatofautiana tabia, uwezo na maamuzi.

Mkuu umepotea sana aisee... usilifanyie jukwaa lako hivyo mazee!!! its your baby mazee... kuhusu tabia, dalili ya mvua ni mawingu, na akumulikaye mchana basi usiku atakuchoma!!! kwa dada charity naona hapo anunue fire extinguishers na miamvuli kabisaaaaa maana kama siyo mvua basi ni moto
 
Mwanaume yeyote anaweza kubadilishwa na mkewe, lakini sio kila mwanaume anaweza kubadilishwa. Actually mabadiliko makubwa yanatokea katika stage ya uchumba, kama huku imeshindikana, sahau kwenye ndoa...

Mheshimiwa Ramois haya mabadiliko ya wanaume ya kwenye uchumba yanaitwa "impression management" ni ya muda na yana lengo maalumu la kumnasa mwanamke hasa yule anayetanguliza mabadiliko kama jambo la msingi kabla ya kukubaliana na mwanaume.

Swali langu ni kuwa hivi kwa nini umtafute mtu wa kumbadilisha wakati unaweza kumpata mtu ambaye ana tabia unazodhani kuwa zinaendana na taste yako? Kujibu swali la msingi: huwezi kumbadilisha mwanaume mtu mzima labda kama una mchumba ambaye bado ni minor.
 
Unataka abadilike........well jiandae pia na hasara za mabadiliko hayo..........mwenzio mmoja huko uswazi alikuwa akilalamika ooh jama nachelewa kurudi oooh anatumia muda mwingi na marafikize ...............jamaa akabadilika; ni kupatikana home full swing! na ndo hapo kutaka kula chakula kila akijisikia!..............malalamiko yakaanza upya!:A S-eek:
 
Unataka abadilike........well jiandae pia na hasara za mabadiliko hayo..........mwenzio mmoja huko uswazi alikuwa akilalamika ooh jama nachelewa kurudi oooh anatumia muda mwingi na marafikize ...............jamaa akabadilika; ni kupatikana home full swing! na ndo hapo kutaka kula chakula kila akijisikia!..............malalamiko yakaanza upya!:A S-eek:
HAHAHAHAHA!
this is it!lol:A S tongue:
 
Unataka abadilike........well jiandae pia na hasara za mabadiliko hayo..........mwenzio mmoja huko uswazi alikuwa akilalamika ooh jama nachelewa kurudi oooh anatumia muda mwingi na marafikize ...............jamaa akabadilika; ni kupatikana home full swing! na ndo hapo kutaka kula chakula kila akijisikia!..............malalamiko yakaanza upya!:A S-eek:
hahaaaa mabadiliko mengine sio ya kuombea
 
naona hapa uvumilivu umekushinda IMEBIDI UPOSTI TU!
haijambo ''bidhaa feki?''

hahaaaaa mpwaz bwana unaniangusha majaribuni mwenzio nipo SA hata malazi sijapata!!!

bidhaa feki uwiiiiiiiiiiiiiiiii!!!!!!!!! I love u mpwaz lol!!!!!

ntakwambia kipembeni bana!! ila namshuku GS
 
hahaaaaa mpwaz bwana unaniangusha majaribuni mwenzio nipo SA hata malazi sijapata!!!

bidhaa feki uwiiiiiiiiiiiiiiiii!!!!!!!!! I love u mpwaz lol!!!!!

ntakwambia kipembeni bana!! ila namshuku GS
hehehehe!naona sasa inabidi ukajifunze karate sasa
 
1.kwenye ndoa si mahala pa kubadili tabia za msingi labda mchumba awe below 20 yrs
2.tabia ndogo ndogo zaweza badilishwa,kama kuwa msafi...unaweza mbadili.
3.zile tabia zake mbaya,idadi yake zidisha kwa mbili ndizo jumla ya tabia zake zote usizozitaka......nina maana zipo tabia zingine mbaya kabisa hutazijua kamwe hadi uolewe.....usitishike ni mambo ya kawaida.huyo jamaa yako sie yeye wa baadae.
4.hakuna mtu anaeoa/kuolewa na malaika, kila mtu ana kasoro nyingi tu ,hata wewe unazokasoro zako dawa nikuvumiliana
5.akikupenda sana sana,i mean sana...yaani kuzidi maelezo(na sijui utafanyaje hadi awe hivyo)basi aweza kuwa vile upendavyo kwa muda....penzi likichuja anarudia tabia yake ya awali.
6.kwenye uchumba kila mtu ni kondoo,mpole mwema,anajali....kila utakachomweleza ni ndio,yaani hapo nidhamu ni mia.baada ya ndoa nidhamu ni sifuri........
Inapungua hadi siku itafika sifuri.
Hata hivyo usijali sana....ni mawazo yangu tu. Mng'ang'anie sana huyo jamaa hadi kieleweke....si unajua tena?achana na mambo ya kumpekua pekua kuku,utashindwa kumla.

Huu ndio ukweli kabisa,
Charity bora umeuliza huwezi kumbadili mtu na tegemea zile tabia mbaya ziwe mbaya zaidi, ndoa ni kama ku share kijimashua na mtu mwingine wote mnatakiwa kupiga kasia ili kufika mahali, hivyo ukiongezea watoto, ndugu, marafiki, kazi, shida, magonjwa ndivyo zile tabia alizokuwa anatumia kujipozea zinavyozidi kuongezeka, itakuwa kazi ngumu kwako kuufanya kazi ya wawili ili mfike salama maana mwenzio atakuwa ni kama anakurudisha upande mwingine au in distraction, kama unaona una uwezo wa kuvumilia hii mikiki, so much the better vinginevyo...
 
Boys will be boys always ...... Never change. Women have this illusion that they will change their boys, they end in frustrations.

Girls will always be girls .... Always changing. Men have the illusion that his woman will always be the same, they end in frustrations. The first year in wedlock and you are completely living with a different woman ... For ever!!

It is women who change for good or for worse, but men are the same
 
HEHEHE!
umeona eeeehhhhh!
tuimbe kidogo aiseeeee

ANAMEEREMETAAAAAAAAAA.....anameremeeta
charity anameremetaaaaa ANAMEREMETAAAAAAAA!

jeiesi hebu kapitie pitie madesa yako ya accounts naona unakaribia kuchukua kazi


tehe tehe tehe tehe
 
Hebu niambieni akina mama/dada wenzangu.Pengine nina rafiki nataka kupeleka mahusiano katika hatua nyingine labda ndoa tuseme.Na huyu mlengwa pengine ana tabia fulani au tuseme mazingira fulani ambayo nisingependa awe nayo katika hiyo level nyingine.
Kwa mfano ni mwizi/jambazi,mlevi,Fukara(hana hela wala kazi-naweza kusema ni mvivu) na mambo kama hayo.
Na pengine nishamwambia kuwa sipendi 1,2,3......ya hizo tabia na akaahidi kuwa atabadilika.
Vilevile katika interraction mbali x2 na marafiki hasa wanaume mara nyingi nimekuwa nikiwasikia wakisema kuwa MWANAMKE anauwezo mkubwa wa kumbadilisha na kumtengeneza mwanaume katika mahusiano the way anataka awe.
Sasa swali langu ni kuwa Is this true?
Wakina kaka pia mnaweza kuniambia eti mnaweza kubadilishwa na wanawake mkawa waume wema wenye kuonyesha mfano mwema?
Chrispin naomba usiingie kwenye hii thread inakuhusu


Inawezekana mrembo.. ila sio garantii... muhimu mlengwa aonense nia ya dhati kutaka kubadilika... kwa maneno na vitendo.. na we tayari kukabiliana na changamoto za kuachana na tabia/matendo mabaya.. ni kazi ngumu..inachukua muda..ila inawezekana, bila kusahau sala!Binafsi nina mfano hai(my good friend) kuthibitisha hali ya mwanamke kumbadilisha mwanaume!!
 
Hebu niambieni akina mama/dada wenzangu.Pengine nina rafiki nataka kupeleka mahusiano katika hatua nyingine labda ndoa tuseme.Na huyu mlengwa pengine ana tabia fulani au tuseme mazingira fulani ambayo nisingependa awe nayo katika hiyo level nyingine.
Kwa mfano ni mwizi/jambazi,mlevi,Fukara(hana hela wala kazi-naweza kusema ni mvivu) na mambo kama hayo.
Na pengine nishamwambia kuwa sipendi 1,2,3......ya hizo tabia na akaahidi kuwa atabadilika.
Vilevile katika interraction mbali x2 na marafiki hasa wanaume mara nyingi nimekuwa nikiwasikia wakisema kuwa MWANAMKE anauwezo mkubwa wa kumbadilisha na kumtengeneza mwanaume katika mahusiano the way anataka awe.
Sasa swali langu ni kuwa Is this true?
Wakina kaka pia mnaweza kuniambia eti mnaweza kubadilishwa na wanawake mkawa waume wema wenye kuonyesha mfano mwema?
Chrispin naomba usiingie kwenye hii thread inakuhusu

Kamwe huwezi kumpata mpenzi aliyekamilika kama unavyotaka kwa 100%. Hivyo, kuna vitu vya kumtengeneza, vya kumbadilisha, na vya kumvumilia. Kwa hiyo uangalie sifa zake hizo kama ni za kumbadilisha, au ni za kumvumilia. Iwapo huwezi kuvibadilisha, basi jaribu kama vinavumilika, kama sivyo pia, basi chukua zako 50, na uachane naye maana si wako. Aidha kwa hivyo ulivyotaja hapo jaribu kama ifuatavyo;

mwizi/jambazi: Hakikisha kila siku unalala naye, na uvunje urafiki, uhusiano, na mawasilano baina yake na makundi yale. Mchukue mpeleke mahali ambapo hajapazoea, ili atengane na mtandao wao huo. Muelimishe juu ya madhara ya vitendo hivyo. Mshawishi aviteketeze zana zote anazotumia kwa kazi hiyo. Kama unaweza, umpatie kazi mbadala iliyo halali, na mfanye wote kwa pamoja.

mlevi: Hapa inategemeana na aina ya ulevi wake, lakini kwa vyovyote, options nyingi hapo juu huenda vikasaidia.

Fukara: Muoneshe kuwa umempenda pamoja na hayo, lakini ungependa zaidi kumuona akijitahidi. Kama hali inaruhusu, anzisha mradi ambao mtakuwa mkiattent wote kwa pamoja na kujishughulisha; kama kwenda shambani, atakuwa akiona aibu kukaa chini huku wewe ukishughulika. Msome tabia vizuri, kama ni wa kupenda kutukuzwa na kusifiwa, kubembelezwa, kupigwa dongo, nk. yoyote utakayoona italeta matunda utumie kwa wakati na hali maalum.

Just to suggest few.....
 
Wanaume wengi hawabadiliki. Nashauri utafute mwenye tabia unayeweza kuendana nayo. Kuna extreme cases ambapo mwanaume hubadilika for good, yaani mpaka mnashngaa hii njemba vipi? Sijui wanawake hao wanawapaga nini?????:heh:
 
...huwezi kumbadilisha, ni yeye pekee mwenye uwezo wa kubadilika (akitaka.) Unachoweza kumsaidia ni 'kugundua' chanzo cha tabia zake mbaya. Jadiliana nae na tena akubali udhaifu wake, kisha mwenyewe ('labda' kwa msaada wako) aanze mkakati wa kubadilika kuelekea kiwango ambacho nyote mtaafikiana nacho.

Be patient ('Ukitaka.') Relationship's about compromising, tunatofautiana tabia, uwezo na maamuzi.
Tatizo lipo hapa kwenye kubadilika mwenyewe ,nitajuaje anataka/ana nia ya kubadilika hata kama amesema anataka mabadiliko? Mawazo ya mtu kuyasoma ni kazi kweli......
................Labda kwa kufunga na kuomba
 
Mheshimiwa Ramois haya mabadiliko ya wanaume ya kwenye uchumba yanaitwa "impression management" ni ya muda na yana lengo maalumu la kumnasa mwanamke hasa yule anayetanguliza mabadiliko kama jambo la msingi kabla ya kukubaliana na mwanaume.

Swali langu ni kuwa hivi kwa nini umtafute mtu wa kumbadilisha wakati unaweza kumpata mtu ambaye ana tabia unazodhani kuwa zinaendana na taste yako? Kujibu swali la msingi: huwezi kumbadilisha mwanaume mtu mzima labda kama una mchumba ambaye bado ni minor.
Kumtafuta ninayeendana kitabia,??????.....INAWEZEKANA lakn sio kirahisi kama unavyofikiria.
Hata mimi sijakamilika 100% Thanks though kwa ushauri.Nitafanyia kazi pamoja na ushauri mwingine wote niliopewa humu.
Nathamini mawazo ya kila mtu.Na nikiyaunganisha yote yanalenga nia moja.
 
Kuwa makini maana wengi wameolewa au kuoa na watu walio wadhania.
Malizia sentensi hii....Naona kama haijakamilika vile.Niwe makini na watu gani? ninaoendana nao kitabia?( wamaanisha kuwa wanaweza kuwa mbwamwitu wenye ngozi ya kondoo?)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom