TUMBIRI
JF-Expert Member
- May 7, 2011
- 1,933
- 1,199
Wakuu heshima mbele,
Nimekuwa nikiisoma Ripoti ya Serikali ya Mdhibiti na Mkaguzi wa hesabu za Serikali ya mwaka wa fedha uliopita (2010/2011) yenye kurusa 216 na nimekuwa pia nikiilinganisha na Taarifa zake za miaka ya fedha iliyopita hususani ya 2008/2009 na 2009/2010.
Katika ripoti ya 2008/2009 Jumla ya Wizara, idara na wakala wa serikali zipatazo 8 zilipata hati safi zisizokuwa na masuala ya msisitizo (Unqualified Audit Opinion without Emphasis of matters). Katika ripoti ya mwaka uliofuata yaani 2009/2010, jumla ya Wizara, idara na wakala wa serikali 21 zilipata hati safi zisizokuwa na masuala ya msisitizo (Unqualified Audit Opinion without Emphasis of matters). Na katika ripoti ya mwaka jana wa fedha yaani 2010/2011, jumla ya Wizara, idara na wakala wa serikali zipatazo 11 zimepata hati safi zisizokuwa na masuala ya msisitizo (Unqualifed Audit Opinion without Emphasis of matters).
Katika ripoti zote hizo tatu zinazofuatana ni taasisi mbili tu yaana Ofisi ya Rais Ikulu na Ofisi ya Waziri Mkuu ndizo zimejitokeza kupata hati safi katika miaka yote hiyo. Kuna baadhi zimepata hati safi kwa miaka miwili ya fedha lakini zikashindwa katika mwaka mwingine. Katika hali ya kawaida imekuwaje Ofisi hizi mbili zimekuwa zikipata hati safi mfululizo kwa kuzingatia kwamba masuala ya msisitizo ambayo yamekuwa yakisisitizwa katika Wizara, idara na Wakala nyingi ni yale yanayohusiana na hali ya kibajeti na Uchumi wa nchi.
Mfano hoja ambayo imeonekana kusisitizwa karibu kila taasisi iliyokaguliwa ni hoja ya Outstanding liabilities (Madeni) na Payment charged to wrong expenditure code ambazo zote kimsingi zinatoka na taasisi huzikuwa zinapewa fedha za kutosha. Sasa mimi najiuliza iweje Wizara nyingi ziwe na Outstanding liabilities alafu Ofisi ya Rais Ikulu na Ofisi ya Waziri Mkuu zisiwe nazo?
Ina maana zenyewe zilipewa migao yao ya fedha kutoka hazina kulingana na bajeti au? Na kama ndivyo iweje zenyewe zipate migawo yote kulingana na bajeti huku Taasisi zingine zikipata migawo ya asilimia 40% hadi 50% ya bajeti nzima?Ina maana hadi kufikia siku ya mwisho ya mwaka wa fedha yaani saa tano na dakika 59 usiku wa tarehe 30/06/2011 hata ile kampuni ya kufanya usafi Ikulu ilikuwa imelipwa deni lake la kufanya usafi wakati tunajua Taratibu za manunuzi ya serikali zinasema huduma kwanza malipo yanafuata?
Twende kwenye hili swala la Payment charged to wrong expendire code. Kwa ofisi ya Rais Ikulu ni vigumu hii hoja isiwepo maana tumekuwa tukisikia wakisafiri mara kwa mara tena kwa misururu ya watu wengi. Ina maana wenyewe kila walipokuwa wakitaka kusafiri vifungu vya Per diem na Air tickets vilikuwa na pesa muda wote?
Utouh, kwa kweli katika hili umetudanganya. Tunaamini Ofisi ya Rais Ikulu na Ofisi ya Waziri Mkuu nako kuna madudu. Kosa hili ulilofanya tunalimjulisha na lile la Jairo. ''You can fool some people but you can't fool all people all the time''.
Kwa wale wanaopenda source hii hapa:
Nimekuwa nikiisoma Ripoti ya Serikali ya Mdhibiti na Mkaguzi wa hesabu za Serikali ya mwaka wa fedha uliopita (2010/2011) yenye kurusa 216 na nimekuwa pia nikiilinganisha na Taarifa zake za miaka ya fedha iliyopita hususani ya 2008/2009 na 2009/2010.
Katika ripoti ya 2008/2009 Jumla ya Wizara, idara na wakala wa serikali zipatazo 8 zilipata hati safi zisizokuwa na masuala ya msisitizo (Unqualified Audit Opinion without Emphasis of matters). Katika ripoti ya mwaka uliofuata yaani 2009/2010, jumla ya Wizara, idara na wakala wa serikali 21 zilipata hati safi zisizokuwa na masuala ya msisitizo (Unqualified Audit Opinion without Emphasis of matters). Na katika ripoti ya mwaka jana wa fedha yaani 2010/2011, jumla ya Wizara, idara na wakala wa serikali zipatazo 11 zimepata hati safi zisizokuwa na masuala ya msisitizo (Unqualifed Audit Opinion without Emphasis of matters).
Katika ripoti zote hizo tatu zinazofuatana ni taasisi mbili tu yaana Ofisi ya Rais Ikulu na Ofisi ya Waziri Mkuu ndizo zimejitokeza kupata hati safi katika miaka yote hiyo. Kuna baadhi zimepata hati safi kwa miaka miwili ya fedha lakini zikashindwa katika mwaka mwingine. Katika hali ya kawaida imekuwaje Ofisi hizi mbili zimekuwa zikipata hati safi mfululizo kwa kuzingatia kwamba masuala ya msisitizo ambayo yamekuwa yakisisitizwa katika Wizara, idara na Wakala nyingi ni yale yanayohusiana na hali ya kibajeti na Uchumi wa nchi.
Mfano hoja ambayo imeonekana kusisitizwa karibu kila taasisi iliyokaguliwa ni hoja ya Outstanding liabilities (Madeni) na Payment charged to wrong expenditure code ambazo zote kimsingi zinatoka na taasisi huzikuwa zinapewa fedha za kutosha. Sasa mimi najiuliza iweje Wizara nyingi ziwe na Outstanding liabilities alafu Ofisi ya Rais Ikulu na Ofisi ya Waziri Mkuu zisiwe nazo?
Ina maana zenyewe zilipewa migao yao ya fedha kutoka hazina kulingana na bajeti au? Na kama ndivyo iweje zenyewe zipate migawo yote kulingana na bajeti huku Taasisi zingine zikipata migawo ya asilimia 40% hadi 50% ya bajeti nzima?Ina maana hadi kufikia siku ya mwisho ya mwaka wa fedha yaani saa tano na dakika 59 usiku wa tarehe 30/06/2011 hata ile kampuni ya kufanya usafi Ikulu ilikuwa imelipwa deni lake la kufanya usafi wakati tunajua Taratibu za manunuzi ya serikali zinasema huduma kwanza malipo yanafuata?
Twende kwenye hili swala la Payment charged to wrong expendire code. Kwa ofisi ya Rais Ikulu ni vigumu hii hoja isiwepo maana tumekuwa tukisikia wakisafiri mara kwa mara tena kwa misururu ya watu wengi. Ina maana wenyewe kila walipokuwa wakitaka kusafiri vifungu vya Per diem na Air tickets vilikuwa na pesa muda wote?
Utouh, kwa kweli katika hili umetudanganya. Tunaamini Ofisi ya Rais Ikulu na Ofisi ya Waziri Mkuu nako kuna madudu. Kosa hili ulilofanya tunalimjulisha na lile la Jairo. ''You can fool some people but you can't fool all people all the time''.
Kwa wale wanaopenda source hii hapa:
MDAs WITH UNQUALIFIED OPINION WITHOUT EMPHASIS OF MATTERS (WIZARA, IDARA NA WAKALA ZENYE HATI ZINAZORIDHISHA NA ZISIZOKUWA NA MASUALA YA MSISITIZO) | |||
No | 2008/2009 | 2009/2010 | 2010/2011 |
1 | Commercial Court | Judiciary | Accountant General's Department |
2 | Drugs Control Commission | Community Dev, Gender and Children | Commission for Mediation and Arbitration (CMA) |
3 | Ethics Secretariat | High Court Commercial Court | Directorate of Public Prosecutions |
4 | Labour Court | High Court Land Court Division | Judicial Service Commission |
5 | President's Office – Cabinet Secretariat | Labour Court | Ministry of Communication, Science and Technology |
6 | President's Office – State House | Ministry of East African Cooperation | Ministry of East African Cooperation |
7 | Prime Minister's Office | Ministry of Livestock Development | Ministry of Finance |
8 | Vice President's Office | President's Office – State House | President's Office and Cabinet Secretariat |
9 | Prime Minister's Office | President's Office, State House | |
10 | RAS Mara | Prime Minister's Office | |
11 | RAS Shinyanga | Treasury | |
12 | RAS Tanga | ||
13 | Tanzania Embassy Berlin | ||
14 | Tanzania Embassy Brasilia | ||
15 | Tanzania Embassy Bujumbura | ||
16 | Tanzania Embassy Geneva | ||
17 | Tanzania Embassy Maputo | ||
18 | Tanzania Embassy Newyork | ||
19 | Tanzania Embassy Ottawa | ||
20 | Tanzania Embassy Pretoria | ||
21 | Vice President's Office |