Wapendwa wana JF,Ukaguzi unaofanywa na CAG ni sampuli (Auditing by Sample) matokeo yake hatupati ukweli wote na kwa maana ya ukaguzi ni kutoa maoni ya kiutalamu tu na siyo uhakika kamili.Ukaguzi ambao umekuwa ukifanyika katika wizara,mashirika,mikoa na wilaya zote umekuwa ni wa sampuli na hauwezi kufuchua uozo wote uliopo katika taasisi zetu.
Ili kuweza kusaidia nchi hii,CAG afanye ukaguzi wa asilimia mia 100% kwa baadhi ya wilaya kwa kila mkoa,kwa mfano mkoa wa mwanza ina wilaya sita,CAG afanye ukaguzi wa asilimia mia kwa wilaya 3 au 2 ili kuweza kutoa picha halisi kwa kila mkoa,ukaguzi huu utaweza kusaidia kwa kufichua hali iliyopo katika wilaya zetu,wizara na mashirika.
Lakini wakaguzi kutoka ofisi ya CAG nao walipwe malipo yatakayowawezesha kufanya ukaguzi tofauti na hali ilivyo sasa,ukaguzi tunaopata matokeo yake ni nusu au robo ya hali halisi katika taasisi zetu.
Naomba maoni yenu
Ili kuweza kusaidia nchi hii,CAG afanye ukaguzi wa asilimia mia 100% kwa baadhi ya wilaya kwa kila mkoa,kwa mfano mkoa wa mwanza ina wilaya sita,CAG afanye ukaguzi wa asilimia mia kwa wilaya 3 au 2 ili kuweza kutoa picha halisi kwa kila mkoa,ukaguzi huu utaweza kusaidia kwa kufichua hali iliyopo katika wilaya zetu,wizara na mashirika.
Lakini wakaguzi kutoka ofisi ya CAG nao walipwe malipo yatakayowawezesha kufanya ukaguzi tofauti na hali ilivyo sasa,ukaguzi tunaopata matokeo yake ni nusu au robo ya hali halisi katika taasisi zetu.
Naomba maoni yenu