Nimesoma kwa masikitiko makubwa kile kilichoandikwa katika gazeti la habari leo la jana tarehe 5/12/2011 likimnukuu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali akiwalaumu watendaji mbalimbali wanaohusika katika usimamizi wa miradi ya maendeleo kwa kushindwa kusimamia miradi hiyo na hivyo kupelekea ongezeko kubwa la 'Special Audits' hapa nchini. Alidokeza pia kaguzi hizi zimesababisha ofisi kushindwa kutekeleza wajibu wake kikamilifu.
Katika gezeti la leo (6/12/2011) la Habari leo Waziri wa Fedha alionyesha kushangazwa kwake na mzigo huo unaosemwa na CAG.
My take:
Kwa ujumla CAG anaupotosha umma kwa sababu ukiangalia sheria ya ukaguzi wa umma, Public Audit Act, inampa mamlaka yote ya yeye kuamua nini cha kukagua na kwa wakati gani. Sheria hiyo imeainisha wazi kabisa ya kwamba hakuna chombo au mamlaka yoyote itakayomuamuru nini cha kuchagua. Vyombo au mamlaka nyingine vitamuomba kukagua na kama ataridhia basi kazi hiyo itafanyika.
Cha kusikitisha huyu mheshimiwa CAG anaupotosha umma na kuonyesha ya kwamba alikuwa anashurutishwa kufanya kaguzi hizo za special. Hili si la kweli nadhani mwenye udhaifu ni yeye pale anaposhindwa kusimamia sheria inayompa mamlaka ya kuamua ni nini akague na nini asikague.
Pili, ni ukweli uliowazi ya kwamba 'quality' ya kaguzi zinazofanywa na ofisi ya CAG na yenyewe inachangia sana kuwepo na kaguzi hizi za special. Inasikitisha pale unapoona mradi wa maendeleo ambao ni wazi kabisa umetekelezwa kwa uzembe na udhaifu mkubwa lakini ofisi hii inatoa hati safi kwa wahusika. Wananchi wanapotoa malalamiko yao ndipo hapo uamuzi wa kaguzi maalumu unapochukuliwa. Hivyo ofisi hii inaposhindwa kutekeleza wajibu wake inachangia hili.
Na katika maelezo ya CAG hajalisema hili hata kidogo. Hapo ndipo napooona upotoshaji. Yeye kafanya nini kuboresha utendaji wa ofisi yake katika kaguzi za miradi ya maendeleo? Je, ni kwa nini alikubali kukagua kila aina ya ukaguzi anao-amriwa na serikali na vombo vingine? Je, alikuwa anafanya wajibu wake professionally? Je, katika hizo kaguzi za special alizofanya ameweza kuwaainisha watendaji wanaokwamisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na hatua gani zimechukuliwa dhidi ya maofisa hao?
Ni muhimu aache siasa na kutumia vyombo vya habari kupaka watu watope huku naye akiwa na madhaifu mengi tu.
Katika gezeti la leo (6/12/2011) la Habari leo Waziri wa Fedha alionyesha kushangazwa kwake na mzigo huo unaosemwa na CAG.
My take:
Kwa ujumla CAG anaupotosha umma kwa sababu ukiangalia sheria ya ukaguzi wa umma, Public Audit Act, inampa mamlaka yote ya yeye kuamua nini cha kukagua na kwa wakati gani. Sheria hiyo imeainisha wazi kabisa ya kwamba hakuna chombo au mamlaka yoyote itakayomuamuru nini cha kuchagua. Vyombo au mamlaka nyingine vitamuomba kukagua na kama ataridhia basi kazi hiyo itafanyika.
Cha kusikitisha huyu mheshimiwa CAG anaupotosha umma na kuonyesha ya kwamba alikuwa anashurutishwa kufanya kaguzi hizo za special. Hili si la kweli nadhani mwenye udhaifu ni yeye pale anaposhindwa kusimamia sheria inayompa mamlaka ya kuamua ni nini akague na nini asikague.
Pili, ni ukweli uliowazi ya kwamba 'quality' ya kaguzi zinazofanywa na ofisi ya CAG na yenyewe inachangia sana kuwepo na kaguzi hizi za special. Inasikitisha pale unapoona mradi wa maendeleo ambao ni wazi kabisa umetekelezwa kwa uzembe na udhaifu mkubwa lakini ofisi hii inatoa hati safi kwa wahusika. Wananchi wanapotoa malalamiko yao ndipo hapo uamuzi wa kaguzi maalumu unapochukuliwa. Hivyo ofisi hii inaposhindwa kutekeleza wajibu wake inachangia hili.
Na katika maelezo ya CAG hajalisema hili hata kidogo. Hapo ndipo napooona upotoshaji. Yeye kafanya nini kuboresha utendaji wa ofisi yake katika kaguzi za miradi ya maendeleo? Je, ni kwa nini alikubali kukagua kila aina ya ukaguzi anao-amriwa na serikali na vombo vingine? Je, alikuwa anafanya wajibu wake professionally? Je, katika hizo kaguzi za special alizofanya ameweza kuwaainisha watendaji wanaokwamisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na hatua gani zimechukuliwa dhidi ya maofisa hao?
Ni muhimu aache siasa na kutumia vyombo vya habari kupaka watu watope huku naye akiwa na madhaifu mengi tu.