C.C.M Haina uhalali wa kuendelea kuwa chama cha siasa, 'Hakijasajiliwa'.

Mimi nadhani huwa mnashindwa tu kumwelewa Pasco,huwa anasimamia anachokiamini bila kujali itikadi za chama.
Alisimamia na kuamini kuwa Chadema haingeshinda Arumeru na kwamba Sioi ndiye angeapishwa kama mbunge, sasa hapa alisukumwa na nini kama si itikadi? Je na hapo tulishindwa kumwelewa?

Tukirudi kwenye mada naomba mkumbuke kuwa kesi iliwahi kufunguliwa dhidi ya CCM na mali inazozimiliki isivyo halali na wakili wa kujitegemea Marehemu Mujuna Balozi lakini kama kawaida majaji wetu katika kuisetiri CCM waliitupilia mbali. Kwa sasa hapa Tanzania hatuna jaji mwenye ujasiri wa kutoa hukumu ya haki dhidi ya CCM. Lakini mwaka 2015, CCM isubiri tu kufilisiwa na viongozi wake kuishia Keko kwa wizi, udanganyifu, ufisadi na mauaji ya Watanzania wasio na hatia.
 
Pasco is very correct on this.

In fact Political Parties Act Sec 7 inaipa shavu CCM as follows:

"7. ---(1) Subject to subsection (2) of this section, every political party formed in any part of the United Republic, shall apply to the Registrar in the prescribed manner to be registered as a political party.

(2) Notwithstanding the provisions of subsection (1) of this section Chama cha Mapinduzi, also known by the acronym CCM, which was, immediately before this Act, the sole political party for the whole of the United Republic shall, on the
coming into effect of this Act, and without further requirement, be deemed to have been fully registered as a political party and shall be issued with a certificate of registration in accordance with this Act".

Halafu Sec 8 inaendelea kuwakumbusha kuwa:

"8. –(1) Every political party other than the political party registrable pursuant to
subsection (2) of section 7, shall apply and be registered in two stages, after
fulfilling all the conditions prescribed for each stage."

Sheria hii haina tofauti na mikataba ya upangaji nyumba huku uswahilini kwetu ambapo baba mwenye nyumba haonyeshi wajibu wake ni nini kwenye mkataba huo....mmewahi kuiona mikataba hiyo jamani???
 
Pasco is very correct on this.

In fact Political Parties Act Sec 7 inaipa shavu CCM as follows:

"7. ---(1) Subject to subsection (2) of this section, every political party formed in any part of the United Republic, shall apply to the Registrar in the prescribed manner to be registered as a political party.

(2) Notwithstanding the provisions of subsection (1) of this section Chama cha Mapinduzi, also known by the acronym CCM, which was, immediately before this Act, the sole political party for the whole of the United Republic shall, on the
coming into effect of this Act, and without further requirement, be deemed to have been fully registered as a political party and shall be issued with a certificate of registration in accordance with this Act".

Halafu Sec 8 inaendelea kuwakumbusha kuwa:

"8. –(1) Every political party other than the political party registrable pursuant to
subsection (2) of section 7, shall apply and be registered in two stages, after
fulfilling all the conditions prescribed for each stage."

Sheria hii haina tofauti na mikataba ya upangaji nyumba huku uswahilini kwetu ambapo baba mwenye nyumba haonyeshi wajibu wake ni nini kwenye mkataba huo....mmewahi kuiona mikataba hiyo jamani???

Sheria hii ilitungwa na chama hicho hicho ili kukilinda. Ndio maana kila Tendwa, au viongozi wa tume ya uchaguzi wanapotoa matamko huwa hayaonekani kuigusa ccm. Hata polisi na vyombo vya usalama wanapofanya kazi zao huwa ni kwa mujibu wa maelekezo ya ccm. Hiyo preferential treatment wameipata wapi? Katiba ndiyo sheria mama, inakataza ubaguzi katika sheria. Kila mmoja yuko sawa mbele ya sheria.

Ccm haijakidhi matakwa ya sheria kuendelea kuwa chama cha siasa.
 
Bahati mbaya sikubahatika kumsikia Tendwa, ila kiukweli, mhe. Tendwa ni mmoja wa vilaza wakubwa sana kwenye siasa za Tanzania ambaye kazi yake kubwa ni kupiga kelele tuu kama debe tupu!.

Sii kweli kuwa CCM haikusajiliwa, ukweli ni kuwa CCM ilisajiliwa na kupatiwa certificate namber moja ila kitua mbacho CCM haikufanyiwa, haikupewa intern registration, wala kuhakikiwa na kupatiwa usajili wa kudumu, bali kilipatiwa usajili wa kudumu bila kuhakikiwa kwa hoja kuwa maadamu CCM ndio kilikuwa chama tawala, hivyo kimekidhi vigezo outright!.

Kitu ambacho sio halali kwa CCM, ni kitendo cha kuendelea kuhodhi rasilimali za Watanzania waliochangishwa kwa nguvu enzi za chama kimoja au walizomilikishwa na serikali enzi hizo. Umiliki wa mali nyingi za CCM sio halali na wanasheria makini wanaweza kulisimamia hili haki ikatendeka.

Baada ya kuanzishwa mfumo wa vyama vingi, CCM imeanza na mtaji mkubwa wa wanachama, hivyo kilitakiwa kurejesha serikalini mali zote kilizozipata kiserikali na kingeruhusiwa kuziretain zile mali za Tanu ambazo zimetokana na michango ya wanachama, ili vyama vyote vianze moja na kuleta ushindani wa haki!.

Mpaka sasa, mtaji mkubwa wa CCM ni ruzuku ya hazina inayojivunia kila mwezi kutokana na kuongoza kwa idadi ya wabunge. CCM imekuwa ikichaguliwa kwa mazoea sio kwa sababu inapendwa sana!. Sasa Watanzania wameanza kuamka hivyo 2015 sio tuu inaweza kupoteza mtaji wake mkubwa wa ruzuku, inaweza kupigwa chini jumla, kama Spirit ya Chadema kule Arumeru itasambazwa nchi nzima, there will be no way out 2015 CCM ni chali, na ndipo wanasheria watatinga mahakamani kuipokonya rasmi mali ilizikwapua na to mark the sad end of CCM!.

Paskali naona umeamua kumbishia hata msajili aliyekiri...
Haya mwaego
 
Paskali naona umeamua kumbishia hata msajili aliyekiri...
Haya mwaego
Msajili ni mwanasheria by professional asiyeijua sheria ya usajili. Nilim count out alipoipiga dana dana usajili wa CCJ!. Kusema ukweli, Msajili Tendwa, hana lolote!.
 
Nimependa mchango wako, umejenga hoja vizuri sana. Nilihisi kama si yule 'Pasco' wa kila siku. Big up kamanda.
Mtoto wa Mbale, asante ila Pasco ni yule yule juzi, jana na leo!. Sina chama, sifungamani na itikadi yoyote, sio mshabiki, mkereketewa wala mfukurukutwa wa chama chochote.
 
Back
Top Bottom