Asprin
JF-Expert Member
- Mar 8, 2008
- 68,012
- 95,358
Wajameni salaam kwa mpigo.
Ukubwa dawa wajameni......
Hii biashara ya mabinti na baba zao kuwa "washkaji" sijui imetokea wapi. Jana nlikapeleka kabinti kangu kapendwa shule kuanza maisha rasmi ya boarding. Shule imekomaa mabinti lazima wahamie hostel kwa ajili ya maandalizi ya "kufa mtu" ya mitihani ya kitaifa mwaka huu. Ikawa haina jinsi.....Sikuwahi kuwaza kabinti kangu kataenda boarding katika elimu ya msingi asee.....
Tumekapeleka haka kabinti nikiwa na mama yake.... wakati ndo tunamkabidhi kwa "wazazi wake wapya" kabinti kakatoka mbio na kunirukia na kuniambia "Bye daddy"... kisha hakooo kakatokomea..... Cha kustaajabisha, mamake alipewa bye ya mbaaaali lol
Hii "bye daddy" bado haijatoka masikioni asee.... kwamba ntarudi home leo bila kulakiwa na kamatesha kangu... damn!.... Na haya maisha ya mimi na mama Matesha wangu kubaki peke yetu nyumba nzima, si honeymoon nyingine hii wajameni? Atanikomaje?
Baada ya kusema hayo naomba msaada...... Eti kuna kitu gani kinawafanya mabinti "wazimike" namna hii kwa baba zao? Ni kwanini mababa wengi nao pia wanakuwa kama "wamelogwa" na mabinti zao? (Hapa ODM nakiri, vibinti vyangu navizimikia kinoma asee... tena haka kamatesha ndo usiseme.....)
Bye Daddy... dah!
Ukubwa dawa wajameni......
Hii biashara ya mabinti na baba zao kuwa "washkaji" sijui imetokea wapi. Jana nlikapeleka kabinti kangu kapendwa shule kuanza maisha rasmi ya boarding. Shule imekomaa mabinti lazima wahamie hostel kwa ajili ya maandalizi ya "kufa mtu" ya mitihani ya kitaifa mwaka huu. Ikawa haina jinsi.....Sikuwahi kuwaza kabinti kangu kataenda boarding katika elimu ya msingi asee.....
Tumekapeleka haka kabinti nikiwa na mama yake.... wakati ndo tunamkabidhi kwa "wazazi wake wapya" kabinti kakatoka mbio na kunirukia na kuniambia "Bye daddy"... kisha hakooo kakatokomea..... Cha kustaajabisha, mamake alipewa bye ya mbaaaali lol
Hii "bye daddy" bado haijatoka masikioni asee.... kwamba ntarudi home leo bila kulakiwa na kamatesha kangu... damn!.... Na haya maisha ya mimi na mama Matesha wangu kubaki peke yetu nyumba nzima, si honeymoon nyingine hii wajameni? Atanikomaje?
Baada ya kusema hayo naomba msaada...... Eti kuna kitu gani kinawafanya mabinti "wazimike" namna hii kwa baba zao? Ni kwanini mababa wengi nao pia wanakuwa kama "wamelogwa" na mabinti zao? (Hapa ODM nakiri, vibinti vyangu navizimikia kinoma asee... tena haka kamatesha ndo usiseme.....)
Bye Daddy... dah!