Royals
JF-Expert Member
- Nov 19, 2011
- 1,466
- 378
Maneno gani yale uliokiwa unayatoa katika ufunguzi wa kampeni pale Usa river? Ulitutia aibu wanachama wenzako.
Wala hukuwa unashangaa umati woote ule ulikuwa unakushangaa wewe ulikuwa unamwiga masanja wa orijino komedi.
Pale ulitakiwa kuueleza umma uzuri wa mgombea wetu bwana Siyoi na siyo kuonesha ufundi wa kutupa madongo majirani zetu wa Chadema. Wao wakitupiga madongo ni sawasawa yao maana wao hutafuta hasira yetu ilipo ili kwa kutumia nguvu ya hasira tuwe kama wao kisha tuonekane kwa jamii kuwa sisi ni sawa na wao. Ulikosea. Muangalie alivo na busara kubwa mwenyekiti wetu wa chama. Yeye hatupiwi dongo kisha naye akalibeba kwa mikona yake na kulirudisha lilikotoka. Muige huyu.
Kwa mfano uliposema " mtu kama upadri umekushinda ubunge utauweza wapi?". Hapa ni mwehu pekee ndiye ambaye hajui kuwa ulikuwa unamsema mzee wa Chadema.
Au umesahau kuwa alikuwa anaumiza sana vichwa vyetu alipokuwa mbunge wa Karatu?
mtu mzima akichoka akili hubwatuka.
Wala hukuwa unashangaa umati woote ule ulikuwa unakushangaa wewe ulikuwa unamwiga masanja wa orijino komedi.
Pale ulitakiwa kuueleza umma uzuri wa mgombea wetu bwana Siyoi na siyo kuonesha ufundi wa kutupa madongo majirani zetu wa Chadema. Wao wakitupiga madongo ni sawasawa yao maana wao hutafuta hasira yetu ilipo ili kwa kutumia nguvu ya hasira tuwe kama wao kisha tuonekane kwa jamii kuwa sisi ni sawa na wao. Ulikosea. Muangalie alivo na busara kubwa mwenyekiti wetu wa chama. Yeye hatupiwi dongo kisha naye akalibeba kwa mikona yake na kulirudisha lilikotoka. Muige huyu.
Kwa mfano uliposema " mtu kama upadri umekushinda ubunge utauweza wapi?". Hapa ni mwehu pekee ndiye ambaye hajui kuwa ulikuwa unamsema mzee wa Chadema.
Au umesahau kuwa alikuwa anaumiza sana vichwa vyetu alipokuwa mbunge wa Karatu?
mtu mzima akichoka akili hubwatuka.