Bw. Ludovick Utoh (CAG) uchunguzi wake ni kutaka kumfurahisha JK kama fadhila?

Nimekuwa ninafuatilia kwa karibu sana kazi aliyoifanya CAG katika uchunguzi wake kwa Jairo. Nimepata mashaka kidogo nikaona ni bora niombe mawazo toka kwenu GREAT THINKERS.

Kwanza nimekuwa nina muheshimu sana kwa kazi nzuri sana ambazo amekuwa akizifanya katika auditing mbalimbali lakini hili la Jairo nionavyo mimi alishinikizwa. Kwa nini ninasema hivyo? Kwa umakini wa huyu mzee na kwa kuwa mtu wa kufuata utaratibu kwa maisha yake yote hayaingekuwa vigumu hata kwa very simple mind kutambua kile kiasi kilichokuwa kimeingia ktk ile akaunti kule Dodoma kilikuwa part ya ile 1B na kwa kwakuwa ile barua tayari ilikuwa na maelezo hayo basi mechi ya uchunguzi ilikuwa imepatikana. Kwa hilo hakuna ambacho kingemfanya Jairo kukwepa kujibu tuhuma.

Ninaogopa sana pale mzee wetu huyu atakapojivunjia heshima yake alioijenga kwa miaka mingi na hasa kwa kuwa tricked na walinda hujuma wazoefu.

Embu tujadili hili jamani.

Asanteni sana.
 
Huyu naye kifo chake kinaweza kuwa kama cha Hosea na TAKUKURU kwani kwa wale mnaokumbuka ni kuwa Hosea alipochunguza Richmond na kuja na majibu ya kinyumenyume alipotezea heshima yake na ya ofisi yake hapo hapo na huyu hili la Jairo linaweza likaharibu kazi yake nzuri aliyowahi kufanya huko nyuma .

Kama aliambiwa afanye hivyuo na mteule wake anapaswa kujitokeza na kusema wazi kwani watu wanaanza kuonyesha mashaka na ripoti zake na hivyo kuiondolea heshima ofisi yake anapaswa kuchukua hatua kikamilifu.
 
Wakuu, kuna mtu anamwamini huyu mzee hapa JF? kama yupo atakuwa ni wale wanaovuruga mijadala mingi hapa jamvini hata kama haihitaji kwenda shule.
Ofisi nyingi tena hizi ambazo zinaongozwa na wateule wa magogoni hazina ukweli zaidi ya kupika uongo uweze kuwa karibu na ukweli. Mimi nilishatoa imani yangu siku nyingi, nimebaki kusubiri katiba mpya ndo nitaweza kuziamini hizi ofisi.
 
Nimekuwa ninafuatilia kwa karibu sana kazi aliyoifanya CAG katika uchunguzi wake kwa Jairo. Nimepata mashaka kidogo nikaona ni bora niombe mawazo toka kwenu GREAT THINKERS.

Kwanza nimekuwa nina muheshimu sana kwa kazi nzuri sana ambazo amekuwa akizifanya katika auditing mbalimbali lakini hili la Jairo nionavyo mimi alishinikizwa. Kwa nini ninasema hivyo? Kwa umakini wa huyu mzee na kwa kuwa mtu wa kufuata utaratibu kwa maisha yake yote hayaingekuwa vigumu hata kwa very simple mind kutambua kile kiasi kilichokuwa kimeingia ktk ile akaunti kule Dodoma kilikuwa part ya ile 1B na kwa kwakuwa ile barua tayari ilikuwa na maelezo hayo basi mechi ya uchunguzi ilikuwa imepatikana. Kwa hilo hakuna ambacho kingemfanya Jairo kukwepa kujibu tuhuma.

Ninaogopa sana pale mzee wetu huyu atakapojivunjia heshima yake alioijenga kwa miaka mingi na hasa kwa kuwa tricked na walinda hujuma wazoefu.

Embu tujadili hili jamani.

Asanteni sana.
Do you mean Ludovick is very clean than all? Re-thing again.
 
Mwaka jana alikuwa na mpango wa kugombea ubunge Rombo kwa tiket ya CDM, japo alikuja kubadil mawazo baadae. Cjui kama bado ana hyo spirit!
 
Analipa fadhila...za kuendelea kula kuku wa bure na bata kibaoo maana umri wake ulishapita...wastaafu wamezidi serikalini jamani sasa vijana watakuja kurithi lini na kuanza kupata uzoefu??
 
Nimekuwa ninafuatilia kwa karibu sana kazi aliyoifanya CAG katika uchunguzi wake kwa Jairo. Nimepata mashaka kidogo nikaona ni bora niombe mawazo toka kwenu GREAT THINKERS.


Ninaogopa sana pale mzee wetu huyu atakapojivunjia heshima yake alioijenga kwa miaka mingi na hasa kwa kuwa tricked na walinda hujuma wazoefu.

Embu tujadili hili jamani.

Asanteni sana.

Hiyo heshima unayodai atajivunjia ameijenga lini? Nina wasiwasi unampa sifa asizokuwa nazo kwa kutomfahamu vyema. Waulize wanaomfahamu tangu akiwa IDM.
 
nazani walikosea ktk uchunguzi wao walipoanzia na kuishia kwa maoni yangu uchnguzi ungeenda kama ifuatavyo:
>> uhalali wa jairo kuchangisha fedha
>> barua alisaini nani? (((kwan luhanjo hakulizungumzia hilo cjui ni kwanini?)
>> sheria inasemaje juu ya hili
>> je? aliyeandika barua ni nani?
2kisha pata majibu ya haya ndipo ukweli ungejulikana kirahic.
 
Nilikuwa namheshimu sana Ludovick kwa umakini wake na intergrity.
Nimefanya kazi naye muda mrefu sana uliopita alipokuwa NBAA, Bodi mambayo hata Mzee Mengi na wazito kama Sayore walikuwemo.
Lakini katika sakata hili amejichafua sana kwa uchafu aliojipaka kwa hili sakata la David Jairo.
Haingii akilini kuwa fedha ambayo ilichangwa na Idara za serikali, fedha ambazo hazina baraka ya Bunge , Katibu mkuu kiongozi na CAG wanasema hilo ni kawaida.
Huu ni wizi wa mchana na CAG ametumika kama toilet paper.
Msimamo wa wananchi mitaani ni kuungana na Bunge na Waziri Mkuu katika hili.
Ikulu imejivalisha joho la kondoo aliaye kutetea wananchi huku makucha ya mbweha yamejitokeza kupitia Katibu Mkuu wake Luhanjo.
Hii si picha nzuri hata kidogo.
Well, i agree with all the condemnations with all evidence being true, of course kama hizo pesa kutolewa namna hii ni kawaida then alitakiwa kurejea au kukariri vifungu vinavyoruhusu hilo, hopeful vipo katika maandiko ya serikali yoyote hata yasiyo rasmi labda(Classified) being a huge amount of money ambazo no doubt ni za walipa kodi siye, ni lazime ziwe accounted for kwa sheria zote za good governance, meaning auditing and so for, pia alikosea CAG alipotoa an independent opinion ambayo kwenye report yake hakui-document----- kwenye auditing tunasema,any material mistatement that may be undocumented may lead to implification....... Lakini CAG alikuwa sahihi kutoa report ambayo inaendana na SCOPE of the audit ambapo alibanwa ku-audit mambo kadhaa tu na siyo the whole system!
 
Hapo chuki kwa Pinda itaongezeka maana dharau ya Luhanjo kwa Pinda ndio ilisababisha bunge liwageuzie kibao!!ni hatari sana serikali imepanguka ni anguko lingine kwa JK
 
Mwaka jana alikuwa na mpango wa kugombea ubunge Rombo kwa tiket ya CDM, japo alikuja kubadil mawazo baadae. Cjui kama bado ana hyo spirit!

Kaka CAG mstaafu haruhusiwi kufanya kazi yoyote ile,na selikali inamlipa 80% ya mshahara wa CAG aliye madarakani mpaka anakufa!so huu wako ni uongo na wewe ni wa kupuuzwa
 
Kuna tetesi kwamba Bw. Ludovick Utoh amepoteza uwezo na ujasiri wa kuibua ubadhilifu wa fedha za serilkali na kuchunguza usahihi wa matumizi ya fedha za serilkali na mashirika ya umma kwa sababu tayari alishamaliza muda wake na kuongezewa muda mara mbili.

Kwa nafasi ya Bw. Utoh ni mtu anayepaswa kufanya kazi kwa uzalendo mkubwa sana maana watanzania wamempa dhamana kubwa, sijui kama mnafahamu kuna nyazifa kwa mujibu wa katiba ya Tanzania, Rais ana uwezo wa kuteua tu lakini hana uwezo wa kuachisha yeye kama yeye bali itakuwa hivyo kupitia jopo la majaji kadhaa wakiwemo wengine kutoka nchi za jumuiya ya madola? nyazifa hizo ni pamoja na CAG na JAJI MKUU.

Kinachofanyika sasa Bw Utoh anataka kumsaidia na kumfurahisha Mhe, Rais Kikwete na serikali yake isiendelee kupata wakati mgumu lakini vile vile kuongezewa tena muda mwingine pengine amalize kabisa awamu hii ya pili ya JK. Lakini pia tetesi zinasema Bw. Jairo na mhe Rais ni maswahiba wa siku nyingi tangu bwana Jairo akifanyia kazi ikulu pale magogoni.

Ndugu zangu, ikiwa hizi ni tetesi najua fika humu ndani kuna Great thinkers na kuna watu wenye first hand information nitafurahi kusikia zaidi.Nawasilisha.
Hata Luhanjo alikwisha maliza muda wake akaongezewa nae anaongezea wengine ambao sasa Wanaumbuka!!
 
Mheshimiwa Spika,

Ukweli uliothibitika katika suala hili ni kama ifuatavyo:-

( a ) Wakati Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini alidai kutenga Sh.39,000,000.00 kwa ajili ya ushiriki wa Wizara na kukodisha ukumbi, Kamati Teule imethibitisha kuwa Ukumbi wa Pius Msekwa huwa haukodishwi.

(b) .....Kwa maana hiyo, malipo ya nyongeza ya Sh. 100,000/= yaliyooneshwa kwa kila mtumishi si halisi bali ni ya kughushi. Kutokana na kughushi huko, jumla ya fedha kiasi cha Sh.13,900,000.00 ambazo ni asilimia 15% ya jumla ya fedha zilizokusanywa (88,000,000.00) ni malipo hewa.

( c ) Baadhi ya watumishi walioorodheshwa kuwa walipokea malipo hayo hawakuwepo Dodoma siku hiyo.

Imagine that, Kamati ambayo haina hata ma accountant wenye uzoefu wa ma audits ya Serikali wameshtukia vitu obvious kama hivyo na CAG kavi miss. Ni bonge la fisadi au auditor mmoja kilaza wa kutupwa jalalani.

Watu oooh, kachaguliwa Umoja wa Mataifa sijui kitu gani, nasema jamani, zile nafasi zinatolewa kwa affirmative action, kama viti maalum vya kina Stella Manyanya, kujazia jazia nafasi za nchi masikini. Think about, wewe Mkaguzi Mkuu wa nchi yenye uchumi wa wakulima na wamachinga, bado mpaka leo mnatumia ma kaunta buku kurekodi ma transactions ya nchi, utaenda kumu audit nani ulimwenguni huko?
 
Back
Top Bottom