Bw. Lowassa, A Bitter Pill to Swallow

Kijakazi

JF-Expert Member
Jun 26, 2007
6,407
8,900
Baada ya kumsikiliza Bw. Lowasa (Waziri mkuu aliyepita) kwenye kipindi cha dakika 45 ITV kwa makini sana ninaweza kusema kwamba sijawahi tangu ufwatiliaji wangu wa siasa za hapa kwetu kusikia kiongozi akiongea mambo ambayo yamenigusa kama Bw. Lowasa.

Kwangu mimi ameonekana kama mtu anayeelewa ni nini hasa tatizo letu na kwa nini hatutoki hapa tulipo kwa mfano moja ya vitu alivyonigusa ni pale kwenye Mafuta, anasema kwamba ni lazima tununue mafuta kwa wingi PALE AMBAPO BEI YA MAFUTA INAPOKUWA CHINI (soko la Dunia) ili kuweza kufidia kwa wakati inapopanda, hiyo kwangu mimi ni reasoning ya hali ya juu na ninalazimika kusema sijawahi kusikia kiongozi wa Tz akiweza kuongea na kutoa reasoning kama hiyo, kingine ni kuhusu uwiano wa ukuaji wa Uchumi na mabadilko ya maisha ya mwananchi wa kawaida (trickle down effect) ameweza kuelezea nini kifanyike ili ukuaji wa uchumi uweze kumfikia mwananchi wa chini, hakuna kiongozi wa Tanzania niliwahi kumsikia akiongelea nini kifanyike kutatua matatizo wote wengine nawasikia ni kulialia tu na kulalamika bila kutoa au kushauri nini kifanyike!

Hivyo kwangu mimi pamoja na kusikia yote kuhusu huyu Bw. Lowasa ikiwemo tuhuma za mambo mbalimbali nafikiri ni mtu ambaye tukimtumia vizuri kwa njia yoyote ile, hata kwa usahuri tu, tunaweza kupata kitu!
 
Alikuwa wapi kufanya hayo alipokuwa waziri mkuu?


Hilo swali lingine, lakini nafikiri kama kumbukumbu yangu iko sahihi hakuwa Waziri Mkuu kwa muda mrefu kuweza kufanya mambo mengi anyway simtetei, ila kwangu hata mimi nilikuwa pia na maoni tofauti kuhusu huyu bwana kutokana na ninayoyasikia kuhusu yeye na kwa bahati mbaya sikuwahi kumsikia akiongea mpaka nilipokuja kumsikia hivi karibuni na naweza kusema imenibadilisha kiasi fulani mtazamo wangu juu yake!

Nimeongolea tu yale niliyoyasikia akiyasema na kulinganisha na yale wanayoyasema viongozi wengine wengi wanapopewa nafasi ya kueleza ni nini kifanyike katika nchi!



 
Balabala mlefu haikosi kona, mwanamke mzuri hakosi kasoro. Alishayasema yote marehemu Dr Remmy Ongala. Huwezi kusema mtu huyu ni mbaya 100% au mzuri 100% Binadamu tafsiri yake ndio hiyo.
 
We ni kijakazi wa Lowassa no doubt

Eti mafuta
wakati nchi ina gesi ambayo ni nishati mbadala?
tunaweza tumia gesi na kupunguza kabisa kununua mafuta kwa kiwango kikubwa

na je mbona Zambia wananunua kupitia bandari ya Dar lakini bei zipo chini?

South Africa je?

inflation je?

dollarization je?

Lowass was a mistake then.he is a scandal now,he will be a disaster tomorrow .....mark my words
 
Hadithi kama hizi zinanikumbusha babu yangu mmoja huko kijijini alikuwa na nyumba yake ambayo alikuwa anaipenda sana! Hivyo alikuwa akipata wasaa wa kuifanyia matengenezo kama ni kupaka rangi, kurekebisha paa linalovuja au kioo kilichopasuka alikuwa na kawaida ya (baada ya matengenezo) anapanda baiskeli yake mpaka kwenye mwinuko ulio mbali kidogo na nyumba yake ili kuangalia nyumba inafananaje baada ya marekebisho.

Hyuo alikuwa babu, kwa wakati wake alikuwa sahihi na ilikuwa atakachokiona huko kama kina hitaji marekebisho zaidi alikuwa hamuulizi mtu ila kuendeleza kile alichoamini kitafanya nyumba iwe bora zaidi!

Nikirudi kwenye mada, inanishangaza kidogo kuhusu viongozi wa kitanzania. Mtu mkubwa na muhimu kama waziri mkuu hatakiwa kuwa analalamika kwenye vyombo vya habari kwamba mambo hayaendi sawa. Kwani tunaamini kwa sheria zetu yeye bado ni mtumishi wa umma kwa maana ya pensheni, kuna ubaya gani mawazo hayo mazuri aliyonayo akawaeleza safu ya uongozi iliyopo madarakania sasa?

Kwa anachokifanya wananchi wanashawishika kuona kwamba mambo hayaendi sawa, na hii si salama sana kwa maisha ya taifa hili, uongozi kama timu lengo ni ushindi na mtu anayetaka ushindi wa peke yake ingawa yuko ndani ya timu kwa vyovyote vile atakuwa na matatizo.

CCM hiyo hiyo hakuna vikao vya chama mkaelezana hizo ngojera badala ya kuwababaisha wananchi? Acheni hizo!
 
Uzuri wa mtu unapimwa kwa hotuba?

Kwanza haikuwa Hotuba, yalikuwa maswali na majibu nafikiri kuna tofauti, pili nafikikiri wote kwa namna moja au nyingine tunakuwa influenced na yale mtu anayoyasema kama ni ya ukweli au si ya kweli hiko ni kitu kingine, lakini cha muhimu ni uwezo wa mtu wa kuelezea na kutambua tatizo, hiyo pekee yake kwangu ni perfomance kubwa tu, ukilinganisha na viongozi wengine niliopata kuwasikia wakijibu maswali wanapoulizwa!
 
Baada ya kumsikiliza Bw. Lowasa (Waziri mkuu aliyepita) kwenye kipindi cha dakika 45 ITV kwa makini sana ninaweza kusema kwamba sijawahi tangu ufwatiliaji wangu wa siasa za hapa kwetu kusikia kiongozi akiongea mambo ambayo yamenigusa kama Bw. Lowasa.

Kwangu mimi ameonekana kama mtu anayeelewa ni nini hasa tatizo letu na kwa nini hatutoki hapa tulipo kwa mfano moja ya vitu alivyonigusa ni pale kwenye Mafuta, anasema kwamba ni lazima tununue mafuta kwa wingi PALE AMBAPO BEI YA MAFUTA INAPOKUWA CHINI (soko la Dunia) ili kuweza kufidia kwa wakati inapopanda, hiyo kwangu mimi ni reasoning ya hali ya juu na ninalazimika kusema sijawahi kusikia kiongozi wa Tz akiweza kuongea na kutoa reasoning kama hiyo, kingine ni kuhusu uwiano wa ukuaji wa Uchumi na mabadilko ya maisha ya mwananchi wa kawaida (trickle down effect) ameweza kuelezea nini kifanyike ili ukuaji wa uchumi uweze kumfikia mwananchi wa chini, hakuna kiongozi wa Tanzania niliwahi kumsikia akiongelea nini kifanyike kutatua matatizo wote wengine nawasikia ni kulialia tu na kulalamika bila kutoa au kushauri nini kifanyike!

Hivyo kwangu mimi pamoja na kusikia yote kuhusu huyu Bw. Lowasa ikiwemo tuhuma za mambo mbalimbali nafikiri ni mtu ambaye tukimtumia vizuri kwa njia yoyote ile, hata kwa usahuri tu, tunaweza kupata kitu!

Hiyo mbona hata wakulima wa mpunga Kilombero wanajua! Kuna muujiza gani kwenye hilo???
 
Ni heri kuwa na "mtuhumiwa" mwenye uwezo wa kufanyq haya hapa chini kuliko kuwa na mtu "asiyechafuka" lakini goigoi.
-mwenye maamuzi
-mwenye kujua tatizo letu
-mwenye solutions za matatizo yetu
-mwenye uwezo wa kujenga hoja
-mwenye udhubutu
Bila hivyo nchi itakuwa na viongozi wasafi wanaojua kuomba maji ila hali wamezungukwa na mito na maziwa
 
Baada ya kumsikiliza Bw. Lowasa (Waziri mkuu aliyepita) kwenye kipindi cha dakika 45 ITV kwa makini sana ninaweza kusema kwamba sijawahi tangu ufwatiliaji wangu wa siasa za hapa kwetu kusikia kiongozi akiongea mambo ambayo yamenigusa kama Bw. Lowasa.

Kwangu mimi ameonekana kama mtu anayeelewa ni nini hasa tatizo letu na kwa nini hatutoki hapa tulipo kwa mfano moja ya vitu alivyonigusa ni pale kwenye Mafuta, anasema kwamba ni lazima tununue mafuta kwa wingi PALE AMBAPO BEI YA MAFUTA INAPOKUWA CHINI (soko la Dunia) ili kuweza kufidia kwa wakati inapopanda, hiyo kwangu mimi ni reasoning ya hali ya juu na ninalazimika kusema sijawahi kusikia kiongozi wa Tz akiweza kuongea na kutoa reasoning kama hiyo, kingine ni kuhusu uwiano wa ukuaji wa Uchumi na mabadilko ya maisha ya mwananchi wa kawaida (trickle down effect) ameweza kuelezea nini kifanyike ili ukuaji wa uchumi uweze kumfikia mwananchi wa chini, hakuna kiongozi wa Tanzania niliwahi kumsikia akiongelea nini kifanyike kutatua matatizo wote wengine nawasikia ni kulialia tu na kulalamika bila kutoa au kushauri nini kifanyike!

Hivyo kwangu mimi pamoja na kusikia yote kuhusu huyu Bw. Lowasa ikiwemo tuhuma za mambo mbalimbali nafikiri ni mtu ambaye tukimtumia vizuri kwa njia yoyote ile, hata kwa usahuri tu, tunaweza kupata kitu!

ngoja wafuasi wa zitto wakusikie umesema hivyo...utapewa mitusi mpaka basi..... Ulichosema ni kweli huyu bwana akichukua nchi tutafika mbali sana lakini tuna bendera fuata upepo wengi tu humu saivi kila mtu anamtaka Zitto...jamani tumechoka watu wa kuuza sura ikulu tunataka rais mwenye uwezo wa kutoa maamuzi magumu ya nchi ili nchi isonge mbele...
 
We ni kijakazi wa Lowassa no doubt

Eti mafuta
wakati nchi ina gesi ambayo ni nishati mbadala?
tunaweza tumia gesi na kupunguza kabisa kununua mafuta kwa kiwango kikubwa

na je mbona Zambia wananunua kupitia bandari ya Dar lakini bei zipo chini?

South Africa je?

inflation je?

dollarization je?

Lowass was a mistake then.he is a scandal now,he will be a disaster tomorrow .....mark my words

Kuhusu Gesi, hayo nafikiri ni mambo ya baadae na yanahitaji pesa, nafikiri alikuwa anaongelea kuhusu sasa hivi nini kifanyike kuondokana au kupunguza kupanda kwa bei ya mafuta, kuhusu hizo nchi nyingine labda wao wanafanya hivyo wananunua kwa wingi Mafuta labda ndio maana bei ziko chini kumbuka hapa kwetu wanapitisha na wanakonunulia ni kwingine!

kuhusu Dollarization, kama uliangalia kipindi chote aliliongelea hilo na pia kupendekeza nini kifanyike na akatoa mpaka mfano wa Afrika Kusini na Misri ambapo hauwezi kuruhusiwa tu kutumia dollar hovyo hovyo bila kuchajiwa na Serikali akapendekeza nini kifanyike!

kuhusu kama yeye ni disaster au sio, hilo sijui mimi nimekuwa tu impressed na jinsi alivyokuwa anajibu maswali na kuelezea nini kifanyike kuboresha na huo uwezo bado sijauna kwa kiongozi mwingine na hivyo tu!

 
Hiyo mbona hata wakulima wa mpunga Kilombero wanajua! Kuna muujiza gani kwenye hilo???
Inawezekana lakini mimi binafsi siajawahi kumsikia kiongozi akijaribu kuchambua na kuelezea tatizo ni nini na nini kifanyike na ukiyapima yako ndani ya uwezo wetu, na sio kuongelea kwamba sijui watanzania tunadharaulika kwa maana hatuji kuvaa suti vitu kama hivyo!
 
Inawezekana lakini mimi binafsi siajawahi kumsikia kiongozi akijaribu kuchambua na kuelezea tatizo ni nini na nini kifanyike na ukiyapima yako ndani ya uwezo wetu, na sio kuongelea kwamba sijui watanzania tunadharaulika kwa maana hatuji kuvaa suti vitu kama hivyo!

Kijakazi,
Tatizo la Tanzania siyo kukosa viongozi wenye kujua solutions. Kinachokosekana ni political will ya kuyashughulikia matatizo kwa wakati.
 
linganisha lowassa alivyokuwa waziri mkuu na huyu mtoto wa mkulima au sumaye
Ndugu hatufanyi comparison ya mbovu kwa mbovu ili kutafuta ipi afadhali,Lowasa alikuwepo serikarini na hatukuona jema la kumnasibisha nalo iweje sasa?
 
Ndugu hatufanyi comparison ya mbovu kwa mbovu ili kutafuta ipi afadhali,Lowasa alikuwepo serikarini na hatukuona jema la kumnasibisha nalo iweje sasa?

Nimesikia kwamba mradi wa maji kutoka Ziwa Viktoria kwenda Shinyanga mpaka Kahama ni moja kati ya Miradi aliyoisimamia yeye Bw. Lowasa sina uhakika na hilo lakini kama lina ukweli wowote basi ni bonge la Plus kwake kwani nimefika huko na kuona jinsi ule mradi ulivyowakomboa watu wa kule!
 
We ni kijakazi wa Lowassa no doubt

Eti mafuta
wakati nchi ina gesi ambayo ni nishati mbadala?
tunaweza tumia gesi na kupunguza kabisa kununua mafuta kwa kiwango kikubwa

na je mbona Zambia wananunua kupitia bandari ya Dar lakini bei zipo chini?

South Africa je?

inflation je?

dollarization je?

Lowass was a mistake then.he is a scandal now,he will be a disaster tomorrow .....mark my words

Eliah G Kamwela says thanks for this very useful post
 


Baada ya kumsikiliza Bw. Lowasa (Waziri mkuu aliyepita) kwenye kipindi cha dakika 45 ITV kwa makini sana ninaweza kusema kwamba sijawahi tangu ufwatiliaji wangu wa siasa za hapa kwetu kusikia kiongozi akiongea mambo ambayo yamenigusa kama Bw. Lowasa.


Hivi EL aliposema UCHUMI wetu unapaa wewe ulikuwa Tanzania au wapi? Sifa moja ya watanzania wengi sio wafuatiliaji wa mambo consistently na siyo watunza kumbukumbu wa mtiririko wa visa au matukio yanayohusu siasa, uchumi au hata watu!! wanasahau haraka sana, hivi wewe Lowassa mpaka JK (Baba wa Taifa) anamkataa kwamba siyp presidential material ulikuwa wapi?

Kinachowatesa NYINYIEM kwa sasa ni kukataa mambo ambayo kambarage aliyasimamia kwa kucha na vidole, ndicho kinachowamaliza NYINYIEM.... stay tuned...
Kwangu mimi ameonekana kama mtu anayeelewa ni nini hasa tatizo letu na kwa nini hatutoki hapa tulipo kwa mfano moja ya vitu alivyonigusa ni pale kwenye Mafuta, anasema kwamba ni lazima tununue mafuta kwa wingi PALE AMBAPO BEI YA MAFUTA INAPOKUWA CHINI (soko la Dunia) ili kuweza kufidia kwa wakati inapopanda, hiyo kwangu mimi ni reasoning ya hali ya juu na ninalazimika kusema sijawahi kusikia kiongozi wa Tz akiweza kuongea na kutoa reasoning kama hiyo, kingine ni kuhusu uwiano wa ukuaji wa Uchumi na mabadilko ya maisha ya mwananchi wa kawaida (trickle down effect) ameweza kuelezea nini kifanyike ili ukuaji wa uchumi uweze kumfikia mwananchi wa chini, hakuna kiongozi wa Tanzania niliwahi kumsikia akiongelea nini kifanyike kutatua matatizo wote wengine nawasikia ni kulialia tu na kulalamika bila kutoa au kushauri nini kifanyike!

Hivyo kwangu mimi pamoja na kusikia yote kuhusu huyu Bw. Lowasa ikiwemo tuhuma za mambo mbalimbali nafikiri ni mtu ambaye tukimtumia vizuri kwa njia yoyote ile, hata kwa usahuri tu, tunaweza kupata kitu!
 
Back
Top Bottom