Bus la jm linaloenda dar mbeya halifai kupanda hawadhamini abiria wao

satellite

JF-Expert Member
Nov 18, 2010
616
164
Bus la JM ni jipya limeanza safari zake za Mbeya dar muda si mrefu sana ila wameanza vibaya kwa kutaka uroho wa pesa,ilikua hivi nilikata tiketi siku ya j4 nikitaka kujaribu likoje(ndo mara yangu ya kwanza kulipanda)ilipofika siku ya J5 jioni wakanipigia simu kuwa bus linamatatizo haliwezi kusafiri na wametutafutia bus lingine luxury lenye gharama sawa na JM(nauli ya bus la JM ni 35,000 hadi mbeya) ambapo walisema ni SUMRY na MBEYA EXPRESS kiukweli sikupenda ila baada ya kuona ni luxury coach nikaona niepushe shari kama bus lao limearibika,kufika asubuhi stend ya ubungo nikakuta mzozo wa baadhi ya abiria wenzangu wa JM wanamwakia wakala wa bus kumbe lilikua limekodiwa na timu ya yanga na sio kuwa lilikua bovu nikagundua abiria wametugawa magari 3 mimi kwa vile nilikua naongea sana na wenzangu kama 7 hivi tukapewa SUMRY luxury,wengine sumry zile za kawaida na Pricess muro,Abiria tulikereka sana kutoheshimiwa na kupewa mabus mengine.sitakuja kulipanda tena na mjihadhari wadau mtakaofikiria kulipanda hilo gari wanathamini pesa kuliko utu.
 
Mlitaka "kudhaminiwa" katika nini mkuu?

Kama abiria mmeshakata tiketi then wanakuja abiria wengine nyuma nyie mnauzwa kwenye mabus mengine tena kwa kuunga unga huoni unaleta usumbufu kwa abiria?fikiria unaopandia njiani then unaambia upanda bus lingine huko njiani itakuaje?ingekua umekata hilo kampuni ni rahisi kujua namba za gari likisogea ss umekata tiketi bus lingine then unapandishwa kampuni nyingine hivi ukiachwa na hilo bus si wamekuaribia siku?
 
Mlitaka "kudhaminiwa" katika nini mkuu?

Nilitegemea wakodi bus lote kwa ajiri ya abiria wao na sio kuwagawanya mabus matatu otherwise wangewakatalia timu ya yanga kuwa bus litu lina abiria tayari hatuwezi kubachukua wote mgawanyike,hiyo timu imekodi siku moja kwa mwaka na wnapoteza abiria wanaosafiri kila wiki au mwezi wao hilo hawajaliona
 
...Umeelewa swali la Bibie aliye mtamu hapo juu? Unapaswa kusema 'HawaThamini' na sio 'HawaDhamini'! Hizo herufi mbili zinaleta maana mbili tofauti kabisa ya hilo Neno!
 
...Umeelewa swali la Bibie aliye mtamu hapo juu? Unapaswa kusema 'HawaThamini' na sio 'HawaDhamini'! Hizo herufi mbili zinaleta maana mbili tofauti kabisa ya hilo Neno!

Matatizo ya kusoma kwa wahindi miaka mingi hadi lafudhi zao tumeshazicopy,kazi ipo nimekusoma babaDesi
 
Hizo lawama zilistahili zibebeshwe kwa Sumatra.

Mkuu Ndibalema sumatra na wamiliki wa makapuni au mabus ni chupa na kizibo mara nyingi abiria wamekua wakisumbuliwa pale ubungo ila hawatake reaction mapema ila wenye mabus wakipata matatizo ndo wanakua frontline,hapa ni kusemelea kwa jamii tu maana wao ndo wahanga wa moja kwa moja ili wajue kampuni gani wahuni na kampuni gani wastaarabu
 
Back
Top Bottom