Buriani Shelembi, mpiganaji shujaa wa CHADEMA - Zitto

Shukrani Mh Zito kwa maelezo yako sadifu. Nawapa Pole ndugu, wana- CDM na wana nchi wa huko Shinyanga. Kama Bwana alivyotoa, ametwaa..
 
Kudoz Mh.Zitto,hii makala imekaa kiufundi wa kiuandishi lakini pia inamliza yoyote atakayepata kuisoma. Inatia uchungu lakini pia inatia matumaini ya Tanzania mpya ijayo kwa kuwa wapo watu ambao Mungu amewaweka kupigania nchi yao bila kujali magumu wanayoyapitia! RIP Mpiganaji Shelembi.
 
Wanachadema wote wamuenzi kwa kuyafanya yale aliyokuwa akiyasimamia na kujenga chama chao mkoa wa Shinyanga na nchini kiujumla,Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi
 
Jana niliangalia kwa hamu kubwa ili nione jinsi wana Shinyanga walivyomuaga shujaa wao, lakini kwa bahati mbaya TV zote hazikulimulika tukio hili, sidhani kuwa hawakuwa na taarifa nalo bali inawezekana ni juhudi za CCM kuwanyima sauti wananchi waamini kuwa vyama vya upinzani (hasa Chadema) havina wafuasi na wanalipoti pale tu kunapokuwepo na habari yenye mtizamo hasi.

Hawataweza.... RIP Shelembi!
 
jamani! Kizuri hakidumu nadhani shibuda anaweza akawa mbadala wake akipewa ushirikiano wa kutosha kutoka makao makuu ya cdm, shy wapo wapanaji wengi sana. Niliumia sana moyoni mwangu niliposikia hayo.
 
Ni ubaguzi mbaya sana. Chama cha Magamba kimekosa uhalali wa kuongozi, lazima watakuwa wameyaziba mdomo hayo matelevisheni kuripoti chochote kinachohusu huu msiba kwani walimchakachua ubunge.
 
Naona Ntemi alipoandika hii thread alikuwa hajaangalia ITV kama anavyodai. ukweli nimeona hii habari ITV tena kwa kirefu sana. Naona ni vema kuwe na data muafaka jamani.
 
Jana niliangalia kwa hamu kubwa ili nione jinsi wana Shinyanga walivyomuaga shujaa wao, lakini kwa bahati mbaya TV zote hazikulimulika tukio hili, sidhani kuwa hawakuwa na taarifa nalo bali inawezekana ni juhudi za CCM kuwanyima sauti wananchi waamini kuwa vyama vya upinzani (hasa Chadema) havina wafuasi na wanalipoti pale tu kunapokuwepo na habari yenye mtizamo hasi.

Hawataweza.... RIP Shelembi!

Chanel 10 walionyesha. Hao ITV, Star TV na TBC achana nao.
 
Habari sio za kweli. ITV na Chan 10 walionyesha jana, labda ulitaka umati uonekane. Habari kama habari ilikuwepo.
 
Channel 10 walionyesha jana jioni na asubuhi ,ITV walionyesha asubuhi ilikuwa coverage nzuri,swali ni kwa TBC1 television ya taifa wanathubutu kutonyesha mikutano ya vijana 10-12 wa UVCCM wanashindwa kuonyesha tukio la chama kikuu cha upinzani kupoteza mwenyekiti wao wa mkoa,ipo siku tutakuja kuamua kuichukua TBC! na kuiweka mikononi mwa wananchi badala ya kuwa mikononi mwa vibaraka wa CCM,hapaswi kuwa wabaguzi ingekuwa Private TV tusingedai haki ya wananchi kupatiwa habari zinazohusu makundi yote ya kijamii,ni TV isiyofuata maadili ni watu wa hovyo na ujinga wa propaganda
 
Shelembi kwa jadi alikuwa kama Derefa kwani lafudhi yake ya kisukuma kamwe haikuachi mbavu zikiwa salama.RIP ''lutunya mwana nyenze Shilembi".Upande wa Pili wa ujumbe wa Zitto unatuonyesha jinsi Shilembi alivyosurvive kigumugumu ndani ya Chadema maake kumtetea Wange Rasta ilikuwa ni kugeuka adui wa moja kwa moja kwa Mbowe.Hii inanipa imani kuwa msimamo wake upande wa Zitto ni "changamoto" lakini kwa Mbowe ni "uadui".

Jiwe la pili limedondoka huku likiwa bado kazini sasa sijui ni nani tena atawarithi hawa maake kumkabili mbowe si kazi ya kitoto .Sijui Zitto ama Shibuda wanaweza kumuenzi Mzee huyu?

Hapo juu ya post yako kwenye rangi nyekundu inabidi upunguze uzandiki wa kuchochea vitu unavyohisi kinadharia, Zitto kaelezea vizuri sana nanukuu "Hili ni fundisho kwa Wanachadema tuliobakia. Kuwa na misimamo bila kuathiri uhai wa chama. Kwamba tofauti ya mawazo ndiyo kushamiri kwa demokrasia." mwisho wa kunukuu. hivyo usichomeke maneno ya uchonganishi ambayo hayana msingi kwani hata nyumbani kwako lazima kuna tofauti nyingi tu za kifamilia au ofisini kwako lazima utakuwa na tofauti na bosi wako hiyo ni sehemu ya maisha, hamuwezi kukubaliana kwa kila kitu kama makondoo.
 
Back
Top Bottom