Buriani Amina Chifupa!

Status
Not open for further replies.
Daa mungu aiweke roho ya dada yetu mahali pema.

Mimi nachotaka ni baba yake awe na moyo wa kujiamini aseme yale ambayo amina alikuwa anataka kusema akamkataza.
Bongo naona kunawatu wanajidai ma mafia usiseme ama utaumia na hii tumeona kama mfano mwingine. Lakini hii gang mimi ntaimaliza hata kama sio leo lakini ntaimaliza na hawa watu wa kina nchimbi na timu yake najua mpo huku lakini tutaonana tu sio leo lakini ipo one day.
 
Kama mtavyoona kwenye article hii. Siri kali yetu kila kitu ni siri. Mikataba ta madini ni siri hata wabunge hawaruhusiwi kuiona na kuijadili. Wabunge bungeni wafunge midomo yao. Wale wataojifanya wajuaji watapewa onyo kali kama hawatasikia basi WATAWAKOLIMBA kama walivyomkolimba Amina, Sokoine na Kolimba. Kashfa ya Richmond ambayo inamhusu kingunge wa juu kabisa, aliwaomba wabunge wasiijadili. Nchi yetu inakwenda wapi!!!?

~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+~+

TAARIFA kuwa serikali imewaonya wabunge wa CCM kuwa makini wakati wakichangia hoja bungeni, zimetushangaza.

Zimekuwa ni habari za kushangaza kwetu, kwa sababu uamuzi wa kuwaonya ulifikiwa wakati wabunge hao walipokutana kama kamati ya chama kufanya tathimini ya namna walivyoshiriki katika kuchangia mjadala wa hotuba ya bajeti na ile ya mwelekeo wa uchumi wa taifa.

Moja ya michango iliyotolewa na wabunge wa CCM ni dhahiri kwamba, ilikuwa ikiiweka katika wakati mgumu serikali, kwa kuzingatia kwamba, iliyowaahidi wananchi imeshindwa kuyatekeleza, na hicho ndio chanzo cha kelele za wabunge.

Mmoja wa wabunge waliokuwa mbogo kwa serikali ni Mbunge wa Nzega, Lucas Selelii (CCM) aliyetishia kukwamisha bajeti za wizara tatu, ikiwamo ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushindwa kutekeleza ahadi zake kwa muda mrefu.

Tunapenda kuikumbusha serikali kwamba, wabunge ni wawakilishi wa wananchi, na wameingia bungeni kwa kupigiwa kura na wananchi, hivyo kitendo cha kuwaita kwenye kikao cha faragha na kuwakaripia kinakiuka misingi ya utawala bora.

Tumefikia uamuzi huu wa kuikumbusha serikali jambo hili kwa sababu si mara ya kwanza kwa serikali kuwatisha wabunge wa chama tawala, ambao wamekuwa wakitofautiana na baadhi ya maamuzi yake, hasa yale yenye athari mbaya kwa wananchi.

Jambo kubwa tunalojiuliza kila serikali inapowaita wabunge wa CCM na kuwaonya ni kwamba, iko madarakani kwa maslahi ya nani kama haitaki kushauriwa na wawakilishi wa watu inaowatawala?

Hatutaki kueleweka vibaya, kwa kueleza msimamo wetu kuhusu jambo hili, kwamba tumelazimika kulisema hili kwa sababu tunadhani wakati wa kuwa na wabunge ambao akili na mawazo yao yameshikiliwa na serikali sasa umepitwa na wakati.

Watanzania wanataka maendeleo, yanayopatikana kwa kila mwananchi kutimiza wajibu wake inavyostahili, hivyo anapotokea mtu au chombo chochote kukwamisha jitihada hizo, ni lazima mtu au chombo hicho kikemewe mapema.

Kusema hivi hatuna maana kwamba tunakusudia kuikemea serikali, bali tunaishauri iepuke tabia ya kuziba mdomo wawakilishi wa wananchi wanapokuwa wakitetea maslahi ya hao waliwaochagua kuwatetea.

Na kwa viongozi ambao wamekuwa mstari wa mbele kuwashambulia wabunge wanaoikosoa serikali katika baadhi ya mambo inayoonekana kufanya kwa makosa, tunapenda kuwakumbusha kwamba, wanachokifanya ni usaliti kwa Watanzania.

Watambue kuwa wabunge, sehemu yao ya kuzungumza ukweli ni bungeni, hivyo kuwanyima uhuru huo ni kuwabana na kuwafanya wasitekeleze majukumu yao kama inavyotakiwa.

Tuwakumbushe viongozi wa aina hii kwamba wakati wa Watanzania kuendelea kuburuzwa unazidi kupungua. Hivyo kitendo chochote chenye mwelekeo wa kuziba sauti za wawakilishi wa wananchi, ni chenye nia ya kutaka kuwaburuza wananchi kwa sababu sauti inakuwa haisikiki katika chombo muhimu kabisa kinachohusika na kutunga sheria za taifa letu.
 
Daa mungu aiweke roho ya dada yetu mahali pema.

Mimi nachotaka ni baba yake awe na moyo wa kujiamini aseme yale ambayo amina alikuwa anataka kusema akamkataza.
Bongo naona kunawatu wanajidai ma mafia usiseme ama utaumia na hii tumeona kama mfano mwingine. Lakini hii gang mimi ntaimaliza hata kama sio leo lakini ntaimaliza na hawa watu wa kina nchimbi na timu yake najua mpo huku lakini tutaonana tu sio leo lakini ipo one day.

Naamini kabisa kuwa kifo ni njia yetu sote na hiyo ni kazi ya mola lakini kifo hiki kimeniacha mdomowazi kwelikweli; bado namini kuwa ni influence ya mwanadamu tu na ni kwa ajili ya personal gain ya namna fulani.

Huko nyuma Mwanakijiji alitonya kuwa Mzee Chifupa alipigiwa simu na kibosile mmoja kutoka serikalini na kutishiwa kuwa ama amnyamazishe binti yake au atamkosa; akamnyamazisha. Kwa vile ameshamkosa, nadhani wakati umefika atoke mbele na kuuelezea umma ni kibosile gani alitoa tishio lile na Amina alikuwa anataka kuzungumza nini.

Mungu Ailaze Pema Peponi Roho ya Marehemu Amina
 
Poleni sana wafiwa, na Mola aiweke roho ya marehemu pahala pema peponi, Amina

Bob
Katika Intelligence HAKUNA kitu kinachoitwa COINCIDENCE!!! HAKUNA.........
 
Too soon she died.
We wept.
The tears continue.
Love is not affected by the death - Love you Amina

Guys! Let her soul rest in peace then we will deal with these evils! I will be back Dr.
 
Duuh jamani mimi nimestuka hadi nimekuwa baridi. Mungu ailaze rohp ya marehemu mahala pema peponi. Hii ni nyota ya kisiasa iliyozimika mapema tumuombee Mungu aiweke roho yake mahala pema peponi. AMINA.
 
Ina lillah waina ilaih rajuun, Mungu amlaze mahali pema peponi Marehemu Amina Chifupa. kwa sasa jina lake limekuwa ubini.
 
chifupa ni shujaa ambae hatasahaulika katika mioyo yetu mpenda ukweli na muwazi

hizi ni baadhi ya kauli zake

"Nafahamu ninapambana na watu hatari, lakini kesho (leo) namuomba Mwenyezi Mungu aniamshe salama, ili niweze kuliweka bayana suala hili mbele ya waandishi wa habari MAELEZO. Nimekusudia kusema ukweli wote kuhusu suala langu," alisema Amina.

"Daima nasimamia ukweli na sababu ya dhamira yangu. Nipo tayari kufungwa au kuchukuliwa hatua yoyote iwapo nitaonekana sina nidhamu… hata ikibidi kupoteza ubunge na uanachama wangu wa CCM. Mimi si mwanasiasa wa ‘ndiyo mzee'," alisema Amina baada ya kuulizwa iwapo ukweli anaotaka kusema hautamgharimu.
 
ningeweza kuwa na maneno ya kuelezea jinsi ninavyojisikia... nimeyakosa.

jamboonormal_crying.jpg



Mimi naongea hapa japo watu wanasema ni jambo la hatari, mimi ni mdogo. Lakini naamini na ninamuamini Mungu, yeye ndiye mwenye uwezo wa kunisaidia mimi, kama niliandikiwa kufa kwa dawa za kulevya, nitakufa hata nisipozungumza hapa Bungeni.
- Kauli ya Amina Bungeni Novemba 13, 2006


Kauli hii inanifanya niwaze na kuwazua. Labda ni mapenzi ya Mola. Tulikuwa tunasubiria kwa hamu ulipue bomu uliloahidi kulipua ukazimwa kabla ya kufanya vile. Hebu ongea kupitia mwingine kwa njia unayoweza huko uliko tuwajue hawa wanaohusika na madawa haya.

RIP Amina...
 
ningeweza kuwa na maneno ya kuelezea jinsi ninavyojisikia... nimeyakosa.

Kweli mwanakjj nahisi unavyo jisikia kwani ulipigana kwa hoja kwa nguvu zako zote na kwa ushawishi wako wote kuhusu hili swala. Ulikuwa kama nabii lakini watu walikupinga kweli najua unaumia sana na wengi tumestushwa na hili. MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU AMINA MAHALA PEMA PEPONI AMIN.
 
Taifa letu leo limejikuta na uso wa mshangao na kutokuamini. Siyo hivyo tu wengi wetu leo tumeamka na kujikuta midomo imefunguka kwa bumbuwazi na wengine machozi yakitulenga na baadhi yakitiririka. Kijana wetu, binti yetu, mdogo wetu, Mbunge wa Vijana Bi. Amina Chifupa Mpakanjia amefariki dunia katika hospitali ya Lugalo jijini Dar-es-Salaam alikokuwa amelazwa. Hili ni onesho kwa kumbukumbu yake. Pichani, Bi. Amina akila kiapo cha utii na ulinzi wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano.
Sikiliza onesho hili maalum.

jamboonormal_aminachifupa.jpg
 
R.I.P AMINA!!
I am hurt.....siwezi kuelezea.
Nitamwomba Mungu kwa imani. Kama ni mapenzi yake atatuonyesha! Haiwezekani...............Kwa wale tunaomini...JINA MOJA KUU ...nafikiri mmenielewa.
 
Ipyana malecela,Horace Kolimba,Jane Mihanji. Edward Sokoine, Amina Chifupa. Who is next
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom