Bungeni: Zitto aigalagaza Serikali, Spika ashindilia msumari wa moto!

Hakuna haja ya kuuliza kwa nini Spika wa bunge Anne Makinda hakushinikiza Mkulo atoe majibu ni kwamba huyu mama si kawekwa pale kwa kulinda Sirikali na sio Serikali na bado mengi mtarajie kuyasikia.Sheme on you voted to Ccm Magamba na poleni sana kwa wote wenye kuongozwa na wabunge wa Ccm Magamba kwa kuwa hata kwenye mikutano yao na wananchi hawapendi waulizwe maswali Lol!!! imekula kwenu mnaokumbatia Magamba na kuyaneemesha ilhali nyie mwashindia dona na matembele wenzenu wanakula kuku.
 
Hisoap kwetu, na nk. Vi wapi?. Kule Gongo lamboto unapata kokoto za kujengea pale sungura tex.
 
Kiwanda cha nyma kimegeuka kiwanja cha ufufuo!
Si ndo faida ya ubinafusishaji kwa mtizamo wa serikali ya magamba? Badala ya majengo ya Tanganyika Peckers kusindika nyama na kutengeneza ajira kwa wtz, majengo hayo ni kwa mapepo na misukule. Vitu vya kufikirika, mwache Gwajima ajinafasi asije akasema tunamwonea gele! Mitanzania ndivyotulivyoridhika na ccm yetu.
 
Usiendeleze hizo RETCO unaongeza machungu mkuu.
Hayo mafanikio ya kuua mashiri ndiyo ambayo Serikali inajivunia.

Wameusha mashirika yote ya umma sasa wamemaliza, wamegeukia kuuza wanyapori. Sasa sijui wakimaliza watauza nini tena. Pengine wataanza kuuza masaburi yao.
 
Wapi Tanzania bag corporations, Kiltimbers, Moshi tanneries, Kilimanjaro Machine Tools, Imara Wood Products Limited, Moshi Plywood
Mkuu, jibu la hili ni rahisi sana! Mafanikio Kwa mtazamo wa serikali ya mgamba ni kuviua visiwepo kabisaa!
 
Kama Bunge aliwezi kuibana Serikali ili iseme nani alipewa Pesa za STIMULURS PARCKAGE nahisi kuna mchezo mchafu umefanyika, hivyo nashauri NGUVU YA UMMA ITUMIKE ILI TUJUE PESA HIZO ZAIDD YA TRILIIIIIIIIIIII,,,,,,,,ONI ZILIKWENDA WAPI? MNAONAJE WADAU


fafanua mkuu..tafadhali.

stimulus package ipi??
 
Kanumba si alikuwa mshereheshaji wao.Kwani Tanzania kuna kiongozi anayejali mambo ya msingi.Wanajali starehe tu.
Waziri Mkulo anataka akaangalie msiba wa kanumba cloud Tv. Ukimuuliza Kanumba ameshatoa Filamu ngapi atakujibu bila hata ya kusoma mahali pia hata historia ya kanumba anayo kichwani .Lakini kwenye mambo ya uchumi wa nchi kupita korosho mpaka akasome du!!! hawa ndio mawaziri wetu
 
Kanumba si alikuwa mshereheshaji wao.Kwani Tanzania kuna kiongozi anayejali mambo ya msingi.Wanajali starehe tu.
Ndio maana kuna vikao vya michango ya harusi lakini hata siku moja huwezi sikia michango ya kwa ajili ya kusomesha ndugu loh hii ndio Tazania bana
 
Zana za Kilimo Mbeya, Hisoap, Mbeya Ceramic navyo viko wapi wakuu

Naibu Waziri Fedha akijibu swali Bungeni leo,alisifia mafanikio ya Ubinafsishaji.Mh. Zito akauliza swali la nyongeza na kusema anasikitishwa na Serikali kusifia mafanikio ya ubinafsishaji na kutoa mifano kuwa 1980s, viwanda vya korosho vilikuwa 12 leo 1 tu chafanya kazi.

Akaongeza Mwatex, Mbeyatex, Sunguratex viko wapi leo. Mkulo kajibu ati swali la Zito ni jipya (kwa kuwa kataja Textile Industry)! Spika Makinda akamgeuzia kibao Mkulo kuwa swali la Zito ni valid lakini hamshinikiza atoe jibu!

Kanuni ko vipi?
 
Mkulo anapwaya sana! Spika alikuwa na fursa ya kumpasha Mkulo lakini anazuiwa na Party coccous. Nimeangalia kwa makini mchezo wa Mkulo alipokuwa anajibu swali as if ana ubia na serikali. Ameniboa sana~!

Watu kama hao ndo wale waliopewa vyeo kama fadhila tu,lakini ukweli ni kwamba aidha wana uwezo mdogo wa kufikiri au wanaamua tu kuupuza ukweli.Kwa mfano,wakati ule wa mgawo wa umeme nchi nzima ni huyuhuyu Mkulo aliyesema kwamba uchumi wa nchi hauathiriki kutokana na mgao uliokuwepo.Hivi aina kama hii ya mawaziri mpaka lini?
 
Tuacheni tumalize awamu yetu ya pili jamani. Mbona mnatuandama hivo? Nchi hii poa kabisa ati.
 
Ni sifa gani inatumika kuwapa watu nafasi za kuwa mawaziri? Kuna wengine hawastahili kabisa kuwemo ndani ya baraza la mawaziri. Uchumi umeporomoka ndani ya miaka hii ya huyu bwana kuwa waziri lakini bado yumo tu. What point does he want to prove?
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom