The Analyst
JF-Expert Member
- Feb 26, 2011
- 464
- 246
Habari zenu wakuu. Najaribu kutafakari Bunge letu na kukiri kwamba limechangamka sana lakini linaanza kukera kwa kelele ambazo mimi naona hazina maana sana. Angalieni usomaji wa kanuni kila dakika mbunge anapotaka kusema jambo na kanuni hiyohiyo kusomwa mara kadhaa kwa kitendo kilekile ndani ya kikao kimoja. Angalieni muda unaotumika kupongeza unaotumiwa na mawaziri na wabunge...baadhi wanawapongeza na kuwashukuru hadi familia zao, wapigakura wao na mbunge au waziri mwenza. Jamani...jamani ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia ya mawasiliano waheshimiwa hawa hawawezi kutumia simu, mtandao kumshukuru wake au waume zao hadi wapewe nafasi ya kuzungumza Bungeni? Haya ni matumizi mabaya ya muda wa kujadili mambo ya msingi. Eti waziri anamshukuru rais kwa kumteua wakati wa kikao cha bunge wakati wanakutana hata kabla ya kuapa kutumikia nafasi hiyo, kwa nini asimshukuru na kutoa ahadi zake huko? ....This is crazy!
Angalieni mipasho, utani, kejeli, vijembe na jinsi mambo hayo yanavyopoteza muda wa Bunge na mwishoni wanaishia kupitisha bajeti haraka haraka pasipo kupitia baadhi ya vifungu kwa kisingizio cha muda kumalizika. Hauhitaji calculator kujua kwamba muda wanaotumia kina Lema, Chatanda, na wapenda vijembe wengine, unatosha kabisa kumalizia zile dakika zinazopungua kila bajeti zinapokuwa zinapitiwa kifungu nadi kifungu especially around saa mbili usiku.
Napendekeza wabunge/mawaziri/spika/wenyeviti wasome kanuni wanapokuwa nje ya ukumbi na kuwa huru kuzitumia pasipo kupoteza muda mwingi kuzisoma wakati wa mjadala. Waheshimiwa hawa pia wakawashukuru wapiga kura wao wanapowatembelea majimboni kwao na si wakati wa kujadili mambo ya maana. Baadhi ya viti maalum wakianza kuzungumza utatamani uzime TV. Baadhi yao wanachojua ni mipasho, masimango, maudhi utadhani........... Jamani mambo mengine yafanyeni wakati wa mapumziko na si wakati wa vikao!
Angalieni mipasho, utani, kejeli, vijembe na jinsi mambo hayo yanavyopoteza muda wa Bunge na mwishoni wanaishia kupitisha bajeti haraka haraka pasipo kupitia baadhi ya vifungu kwa kisingizio cha muda kumalizika. Hauhitaji calculator kujua kwamba muda wanaotumia kina Lema, Chatanda, na wapenda vijembe wengine, unatosha kabisa kumalizia zile dakika zinazopungua kila bajeti zinapokuwa zinapitiwa kifungu nadi kifungu especially around saa mbili usiku.
Napendekeza wabunge/mawaziri/spika/wenyeviti wasome kanuni wanapokuwa nje ya ukumbi na kuwa huru kuzitumia pasipo kupoteza muda mwingi kuzisoma wakati wa mjadala. Waheshimiwa hawa pia wakawashukuru wapiga kura wao wanapowatembelea majimboni kwao na si wakati wa kujadili mambo ya maana. Baadhi ya viti maalum wakianza kuzungumza utatamani uzime TV. Baadhi yao wanachojua ni mipasho, masimango, maudhi utadhani........... Jamani mambo mengine yafanyeni wakati wa mapumziko na si wakati wa vikao!