BUNGENI: Wenje amlipua Membe; yeye atoa onyo kwa mabalozi!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,428
113,426
Mbunge wa Nyamagana, Mhe. Ezekiel Wenje, ambaye pia ni waziri kivuli wa Mambo ya Nje, amemlipua Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Bernad Membe kuhuhusiana na tuhuma za Wanabalozi wa nje kusaidia vyama vya upinzani.

Ulipuaji huu, unaendelea live kutoka bungeni Dodoma kupitia TBC Live!.

Mhe. Wenje amesoma kifungu cha sheria ya mwaka 1964 kinachowaruhusu mabalozi kutembelea popote ili mradi wawasilishe taarifa wizarani, (taarifa hiyo huitwa Note Verbale), hivyo amesema tuhuma za Membe kuwa baadhi ya wanabalozi wasaidia upinzani ili kupindua nchi, ni tuhuma nzito, hivyo amentaka waziri Membe azithibitishe tuhuma hizo au aombe radhi kwa wanabalozi na kwa kambi ya upinzani.

Akifafanua zaidi alisema shutuma hizo pia ziliungwa mkono na Waziri Mkuu aliposema wanabalozi wanajitembelea tuu majimbo ya wapinzani, hivyo akauliza, kumbe tatizo, ni kwa wanabalozi kutembelea majimbo yanayoongozwa na wapinzani?.

Mhe. Wenje, anaendelea kuichana MFA.

Pasco.
 
Wenje amesema kambi ya upinzani, inapinga ile chanji ya Rada, kurudishwa serikalini. Huu ni ukiukwaji mkubwa wa mising ya utawala bora.
Kwanza wanataka watuhumiwa wote na wahusika watinge mahakamani.
Wanataka fedha hizi ziingizwe kwenye akaunti maalum (Escow Acc.)
Pia wameitaka BAE ilizilipe hizo fedha mapema iwezekanavyo.
 
Pia wamelipua safari za nje, kuwa nyingi ni za kutembeza bakuli, kitendo ambacho kinalidhalilisha taifa.
Wenje amesema, Taifa letu linajulikana sana ulimwenguni kwa kwa kuwa moja ya nchi ambazo zinatembeza bakuli kwa sana huku likibaki ni moja ya mataifa masikini sana Duniani!
 
Hapo hakuna issue, wabunge ni wapinzani tu, wengine ni wala mlungula watupu.
 
Wenje anazidi kumpigilia misumari msalabani Mhe. Membe. Msumari mwingine umehusu shamba fulani la mzungu mmoja huko Arusha (not Silvadale).
 
Pia wamelipua safari za nje, kuwa nyingi ni za kutembeza bakuli, kitendo ambacho kinalidhalilisha taifa.
Wenje amesema, Taifa letu linajulikana sana ulimwenguni kwa kwa kuwa moja ya nchi ambazo zinatembeza bakuli kwa sana huku likibaki ni moja ya mataifa masikini sana Duniani!
Hayo ni mambo ya kawaida tu wewe! unadhani nchi ngapi duniani hazina mikopo?? Acha kushabikia ujinga
 
Hayo ni mambo ya kawaida tu wewe! unadhani nchi ngapi duniani hazina mikopo?? Acha kushabikia ujinga

Kuna tofauti kubwa sana tena sana kati ya mkopo na u-matonya! Anachoongelea Wenje ni hii tabia ya viongozi wetu wakuu kubisha hodi kwa wanaume wengine kila kukicha wakiomba hela ambazo kimsingi tuna uwezo wa kuzitapata kama tutaziba mianya ya ufujaji. Mfano Kama Balozi majaar anaomba Marekani yote Billioni 3 tatu ili kununua madawati kwa shule za kitanzania, huku Jairo anachangisha over a billion kupitisha bajeti! at the same time Ikulu inaleta budget yake ya mwaka 135 billion bila kueleza nini hasa kinanunuliwa na hizo bilioni! Na pia ukikomesha posho za wabunge within 2 months utakuwa tayari umenunua madawati yote anayoembea Balozi Majaar. Umatonya ni kasumba wala sio shida! Ni kukosa aibu!
 
Wenje anazidi kumpigilia misumari msalabani Mhe. Membe. Msumari mwingine umehusu shamba fulani la mzungu mmoja huko Arusha (not Silvadale).
Crap! Wenje is just giving out his opinion wewe unasema msumari, mbona mimi naangalia hapa naona ni mjadala wa kawaida sana? Au umetumwa kumjenga Wenje baada ya wana Mwanza kumtuhumu kuwadanganya na kuhamia Dar? Na kwamba alipokuwa anaomba kura alijidai mlokole na sasa anakunywa pombe ya kufa mtu? Stop manipulating people here!
 
Hakika ni kichekesho maana hicho kinachoitwa kulipua ni upuuzi mtupu maana kila tukiangalia hakuna jipya zaidi ya yale ambayo tumezoea kuyasikia na mengine ni yale ya wale wapinzani wake kama issue ya shamba la Arusha ambalo tukio lake lilitokea mwaka 1986 wakati huo Membe akiwa ni mtumishi wa kawaida wa serikali. Hivi unaposema hela iwekwe kwenye escrow account, ana maana gani? Anajua Escrow Account matumizi yake huwa ni vipi? Kwa bahati mbaya sana wakati anaongea hili, bunge la Uingereza na serikali vimeshaiamuru BAE walipe fedha hizo haraka serikalini.

Mimi nashangaa mtu kulalamikia ziara za nje wakati hiyo ni sehemu ya ushirikiano wa kimataifa na linafanywa na kila nchi. Kwani Marekani inapotuma rais au waziri wake wa mambo ya nje kote duniani anatembeza bakuli? Ninachokiona hapa ni ama upeo mdogo wa shughuli za kimataifa au ni kutumiwa katika siasa za amji taka.
 
Membe hawezi kuongoza nyumba yake ataiongoza nchi? hatuwezi kurudia makosa tena tumejifunza kwa kikwete hatuna hamu na magamba tena.nyie chukueni rushwa zenu kwa muda wa mwisho.
Wewe unaongea pumba kabisa eti kumchafua Membe, it doesn't work like that Sister!. Slaa mpaka leo hata mke ameshindwa kuoa, simple meaning ni kwamba hawezi kum control mwanamke tu itakuwa nchi?? Mshkaji miaka 60+ bado ana mchumba! Give me a brake here. Something is wrong with this dude.
 
Nimemsikiliza Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni akidai kwamba Mh Benard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa awaombe radhi Wabunge wa Kambi ya upinzani, Mabalozi na wananchi waliowachagua kwa kudai kwamba mabalozi huwapatia fedha nyingi Wapinzani Majimboni!
Hayo yalisemwa na Waziri Kivuli wa Nchi za Nje na Ushirikiano wa kimataifa, Wenje, akitoa hoja za Kambi Rasmi ya Upinzani leo! Wenje pia alidai kwamba Mabalozi Mh Membe aliwahi kudai kwamba Mabalozi kutembelea majimbo ya upinzani hawaja Sheria yoyote au Waraka Na. 2, 1964 (sijajua huu Waraka unasemaje), inakuwaje basi Waziri kuwalaumu huku akijua kwamba hawajafanya kosa lolote? Kwani kosa hapa ni kutembelea Wapinzani? Huu ni udhalilishaji, Waziri aombe radhi!
 
Kuna tofauti kubwa sana tena sana kati ya mkopo na u-matonya! Anachoongelea Wenje ni hii tabia ya viongozi wetu wakuu kubisha hodi kwa wanaume wengine kila kukicha wakiomba hela ambazo kimsingi tuna uwezo wa kuzitapata kama tutaziba mianya ya ufujaji. Mfano Kama Balozi majaar anaomba Marekani yote Billioni 3 tatu ili kununua madawati kwa shule za kitanzania, huku Jairo anachangisha over a billion kupitisha bajeti! at the same time Ikulu inaleta budget yake ya mwaka 135 billion bila kueleza nini hasa kinanunuliwa na hizo bilioni! Na pia ukikomesha posho za wabunge within 2 months utakuwa tayari umenunua madawati yote anayoembea Balozi Majaar. Umatonya ni kasumba wala sio shida! Ni kukosa aibu!
Kweli kabisa. Kama huu umatonya ungekuwa kwa faida ya Watz wote na siyo majambazi wachache ningeelewa. wanaombaomba kwa niaba yetu ili waibe. Hii nchi imetembeza bakuli kwa miaka zaidi ya nusu karne bado hakuna badiliko. Wenzetu ulaya mashariki wamesaidiwa kidogo tu lakini sasa wanaenda spidi ya ajabu. RA ameenda kutumbua Ulaya. Ee Mungu tunusuru!!
 
Hakika ni kichekesho maana hicho kinachoitwa kulipua ni upuuzi mtupu maana kila tukiangalia hakuna jipya zaidi ya yale ambayo tumezoea kuyasikia na mengine ni yale ya wale wapinzani wake kama issue ya shamba la Arusha ambalo tukio lake lilitokea mwaka 1986 wakati huo Membe akiwa ni mtumishi wa kawaida wa serikali. Hivi unaposema hela iwekwe kwenye escrow account, ana maana gani? Anajua Escrow Account matumizi yake huwa ni vipi? Kwa bahati mbaya sana wakati anaongea hili, bunge la Uingereza na serikali vimeshaiamuru BAE walipe fedha hizo haraka serikalini.

Mimi nashangaa mtu kulalamikia ziara za nje wakati hiyo ni sehemu ya ushirikiano wa kimataifa na linafanywa na kila nchi. Kwani Marekani inapotuma rais au waziri wake wa mambo ya nje kote duniani anatembeza bakuli? Ninachokiona hapa ni ama upeo mdogo wa shughuli za kimataifa au ni kutumiwa katika siasa za amji taka.
Mkuu mbona wewe umeandika vizuri sana? Mwenzio aliiandika"Escow Acc" kuonyesha kwamba hata maana yake hajui leave alone kuliandika neno lenyewe. Anakurupuka tu akiwa haelewi maana yoyote.
 
Wenje alimaliza na sasa ni wachangiaji.
Shibuda ndio anachangia kwa methali, nahau na tamathali za semi, ukumbi wa bunge mbavu chini.
 
Mawe..na bado atakoma.sijui kwa nini membe ana-compromise masters yake ya international Relations.Huwa namuheshimu,he's intelligent but nadhani huwa linapokuja swala la maslahi yake linaenda beyond academic credentials. sasa sijui ni kwa nini anatoia accusation za kitoto namana hii kwa kupotosha maazimio ya vienna convetion juu ya kinga za mabalozi,na pia onyo la kutoingilia mambo ya ndani ya nchi nyingine.ni8 lazima asome sheria za kimataifa vizuri,kinga zinazowalinda mabalozi na zinazolinda uhuru wa kutoingiliwa kwa mamabo ya ndani ya host countries imeelezwa.Sasa hapo ni kama vile kama anawatuhumu kwa Espionage,political participation,Internal affairs intervention,hostility acts,attempt on agression move,favouring political movements na pengine encouraging sub-nationalism,treason etc.

Huyu inabidi siku moja arudi shule ya diplomacy tena akasome Diplomacy foreign policy and National security hata kama alishawahi kufanya kazi UWT,asiogope matusi ya huyu Lecturere wa Galillee university -Israel,and for his own good inabidi akutane na Ambassador Dr. Yitzhak Gerberg.
 
Kuna tofauti kubwa sana tena sana kati ya mkopo na u-matonya! Anachoongelea Wenje ni hii tabia ya viongozi wetu wakuu kubisha hodi kwa wanaume wengine kila kukicha wakiomba hela ambazo kimsingi tuna uwezo wa kuzitapata kama tutaziba mianya ya ufujaji. Mfano Kama Balozi majaar anaomba Marekani yote Billioni 3 tatu ili kununua madawati kwa shule za kitanzania, huku Jairo anachangisha over a billion kupitisha bajeti! at the same time Ikulu inaleta budget yake ya mwaka 135 billion bila kueleza nini hasa kinanunuliwa na hizo bilioni! Na pia ukikomesha posho za wabunge within 2 months utakuwa tayari umenunua madawati yote anayoembea Balozi Majaar. Umatonya ni kasumba wala sio shida! Ni kukosa aibu![/QUOTE]

nakuunga mkono mkuu..uko sahihi kabisa na huu ni ukweli mtupu
 
Crap! Wenje is just giving out his opinion wewe unasema msumari, mbona mimi naangalia hapa naona ni mjadala wa kawaida sana? Au umetumwa kumjenga Wenje baada ya wana Mwanza kumtuhumu kuwadanganya na kuhamia Dar? Na kwamba alipokuwa anaomba kura alijidai mlokole na sasa anakunywa pombe ya kufa mtu? Stop manipulating people here!

Mkuu si uchangie mada bila ku-atack mtajwa personally. Ina tija gani kuingiza personal life ya Wenje ktk mada hii. Wewe unaagalia TV na kumwelewa Wenje unavyomuelewa na mwingine vivyo hivyo. Wote mna haki ya maoni yenu lakini si sahihi kumatack mtu directly namna hiyo. Jenga hoja yako!
 
Back
Top Bottom