Vyama vyote vinavyoongozwa kisasa lazima vijiwekee utaratibu wa kupika makada wao na kutengeneza tabaka la viongozi wao. Kwanza unapoenda kuokota makada wa chama kingine unamaanisha kuwa falsafa za vyama vyenu zinalingana.Ni sawa na Marekani watu wa Democtrats wakanunue mtu wa republican haiingii akilini kwa sababu vyama hivi ni tofauti sana kiitikadi. Na ukumbuke itikadi ni kama imani.Kufuata watu wenye umaarufu siyo njia itumiwayo na CDM pekee ni njia inayotumiwa na vyama vingi vya siasa,ila kwa kipindi kile kama CDM wasingemuokota angetokea wapi kuja kupiga hizo kelele leo? Na kwa sasa angalia upepo vizuri je umaarufu wa CDM (nikimaanisha chama) huko maswa ni uleule ulikokuwepo kabla ya 2010?