Bora wazipige watie adabu,kwa matusi haya na ushabiki wa kisiasa kweli wananchi tutaambulia kitu kweli,bajeti ni mbofu mbofu ila ccm wanaunga mkono mia kwa mia.
Aisee kumbe Mwigulu Mchemba hana akili kabisa. Anahitaji kupelekwa Mirembe CCM inakufa anaamua kutupa matope Bungeni kutukana upinzani waigizaji na vichaa na eti wana pepo mtaka vyeo. Hasira zake nafikiri ni failure kule arumeru. Anataka kurudia yale ya Lusinde arumeru ama kweli CCM imekwisha. Ametupa bajeti ya Upinzani na kuiita rubbish
Mwigulu anataka kuwazamisha wabunge wa CCM wakiwa wanacheka wakidhani wako salama.
1. Anasema OC ni kwa ajili ya mambo kama katiba mpya, kulipia fidia watu wanaohamishwa. Sasa kwanini wasitaje ni kiasi gani kinaenda kwenye fidia au katiba badala ya kusema OC? Nini maana ya budget kama husemi how much is going kwenye kila area? Kila mtu anajua OC ndiko watu wanakula.
2. Mwigulu anasema ahadi ya serikali katika mpango wa maendeleo 2011/16 kutenga 35% inajumulisha human capital investiment yaani kusomesha wanafunzi! hivyo serikali kuweka 30% ni kwamba hiyo nyongeza ya 5% inakuwa kwenye human capital. Kama ndivyo kwa nini serikali ilisema 35% na sasa wanajitetea kuwa kuna human capital investment baada ya kubanwa kutenga hela hafifu?
3. Lakini kubwa, Mwigulu anaweza kusema kwa nini Tanzania ni maskini?
hata jina geni ndg lete details na hata amina mwenyewe na ajitokeze. Pili sijawahi kulala stanley hata mara moja tangu ijengwe na tangu nizailiwe. Kwa ufupi najua nawakera sana cdm ila kwenye uzinzi sipo na hawatanipata angalia aibu hiyo tangu utoto wangu sijawahi kuwa na mpenzi anaitwa amina rashidi na sijawahi kulala hata ile ya pekee yangu stanley. Pili iramba nikiwa ziara nina utaratibu wa ajabu kidogo huwa nachukua double nalala na washikaji wanne kupiga story tena sijawahi kulala hayo mahotel ya ghali hapo singida ndg ulizia vizuri utanikuta mzinga sgd au mapokezi misigiri
Nchemba kwa jumla kachemka..kuna haja gani ya kuita OC kwenye budget.. Tunataka detail in tuweze kufanya tracking. Sioni kama sensa ni kitu cha kuandikwa OC au katiba mpya tuseme ni OC..hivi vyote vinahitaji kunyambulishwa, tuache siasa jamani. Hata hivyo mbona waziri hakuvitaja ila wabunge wameanza kuhoji ndio tuanaanza kutafuta sababu.. Bado nina wasiwasi na hii OC ya Nchemba.
Hii imekaaje? Ni ile V8 ya KUB?Lissu nae katoa matusi na kaambiwa afute, katumia neno 'silly'
naona mipasho inatikisa bunge.
Nchemba anasema Mbowe alirudisha gari la zamani kachukua jipya na kali zaidi