BUNGENI: Muswada wa mabadiliko ya katiba

Hapa patamu waacheni wajichanganye ili tuwashe moto zaidi ya ule wa Mbeya, maana wamezidi hata tanzania ijay wanatupangia kwa nguvu shiit!
 
Yaani bado viongozi wanadhani Watanzania ni wajinga kiasi kwamba hawajui hata wanachokitaka? Inapofikia mpaka mwanafunzi anamtuzi mwalimu wake, then hapo kuna tatizo kubwa.
 
Yaani bado viongozi wanadhani Watanzania ni wajinga kiasi kwamba hawajui hata wanachokitaka? Inapofikia mpaka mwanafunzi anamtuzi mwalimu wake, then hapo kuna tatizo kubwa.

Mkuu EMT, Serikali taahira ndivyo ilivyo hutaka kuwaendesha Wananchi wake kama gari bovu bila kugundua athari kubwa sana za kufanya hivyo wanachojali wao ni kuandika katiba itakayowahakikishia kuendelea kuitawala Tanzania milele hata kama katiba hiyo haikubaliwi na idadi kubwa la Watanzania.
 
Wasira kichwa bana, anajua kujenga hoja na ni mzoefu wa mambo. ikumbukwe msuada wenyewe unaingiliwa na siasa sana mpaka wataalam wetu wakiwemo hao maprof. wanatumia utalaam wao kufurahisha kundi fulani la wanasiasa. kwa ufupi Wasira sio anafanya siasa ila anatoa taswira jinsi siasa inavyozidi utaalam na hata wataalam wetu wanatumia siasa kuwasilisha utalaam wao wasipofanya hivyo wanaonekana either waunga mkono serikali au wanafuata beat ya opposition. haya yanafanyika hapa Tanzania tu, vukeni mipaka muone. am out.

Wewe kweli hujui kuanalyse mambo. Inaelekea tatizo lako la hizo siasa za Simba na Yanga ndizo zinazokusumbu!! Kwa taarifa yako swala la katiba halihitaji ushabiki wa design hiyo ya kwako. Design zenu mnatakiwa kuogopwa kama ukoma!!! Kwa akili yako unafikiri Prof. Shivji anzungumza vile kufuata beat ya opposition kweli?? Na kwa akili yako inaelekea unaamini serikali inafanya hivi kwa maslahi ya wananchi!! Kama mtizamo wako uko hivyo basi wewe ni zuzu hivyo huwezi kuona the big picture!!
 
Jaji Werema amewataka wanasheria nchini kuwa wakweli, wasiwapotoshe wananchi, kwanza muswada huo sio muswada wa katiba mpya kama wanasheria wanavyohubiri.

Muswada unaosomwa kwa mara ya pili, ni muswada wa kukusanya maoni jinsi ya kuunda tume ya kukusanya maoni na sio muswada wa katiba mpya.
Kwa taarifa yako Jaji Werema na Wasira wamewekwa na rafiki yao JK lazima walinde maslahi ya mtu aliye waweka wala si vinginevyo!!!!!!!!!Hawaja fanyiwa vetting kama tunavyotaka katiba mpya iwekwe, kazi ya hawa watu nikulinda maslahi ya mwajiri wao kirafiki period!!!!!!!!!!!!
 
Yaani bado viongozi wanadhani Watanzania ni wajinga kiasi kwamba hawajui hata wanachokitaka? Inapofikia mpaka mwanafunzi anamtuzi mwalimu wake, then hapo kuna tatizo kubwa.

Na huu muswada ndio kitakuwa kipimo halisi cha uelewa wa watanzania. Tukiamua kukaa kimya na kunyoosha mikono hewani basi tumekwisha, tunahesabu miaka mingine 50 ya mateso bila chuki!
Kama serikali itaamua kuziba masikio na kusonga mbele kuusoma kwa mara ya pili, basi kuanzia hapo itakuwa ni dhahiri kwamba serikali ya ccm imeamua kwa makusudi mazima kuwazika wananchi na kitakachotokea huko mbeleni tunaweza tukakitabiri mapema.
Lakini bado tunadhani serikali inayo nafasi, bunge bado linayo nafasi tena kubwa zaidi ya kuinusuru nchi kuingia katika msukosuko usiokuwa wa lazima.

Katiba ya wananchi ni lazima itungwe na wananchi wenyewe! tena hatua kwa hatua bila kuacha hata nukta moja.
 
Wanabodi wenye access na TBC, angalieni TBC Live kipindi cha Jambo Tanzania. Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Warema na Waziri Stephen Wasira, wanahojiwa live kuhusu kuwasilishwa Muswada wa Sheria wa Kuundwa Tume ya Kukusanya Maoni ya Kubadilisha Katiba.
aji Werema amewataka wanasheria nchini kuwa wakweli, wasiwapotoshe wananchi, kwanza muswada huo sio muswada wa katiba mpya kama wanasheria wanavyohubiri. Muswada unaosomwa kwa mara ya pili, ni muswada wa kukusanya maoni jinsi ya kuunda tume ya kukusanya maoni na sio muswada wa katiba mpya.

Jaji Werema na Waziri Wasira, wamelishambulia Jukwaa la Katiba na wale wote waliotoa maoni hasi kuhusu kusomwa kwa mara ya pili kwa muswada wakiwataja kwa majina akiwemo Deus Kibamba, Prof. Issa Shivji, Prof. Josephat Kanywanyi na wengine wote wanaopinga muswada huo usiwasilishwe wakiwemo Chama cha Wabasheria Tanzania, TLS, wametajwa kuwa sio wakweli bali wanapinga kwa ushabiki tuu.

Kipindi hicho, kimeongozwa na mtangazaji Elisha Eliya , ambaye ni mmoja wa watangazaji mahiri kabisa wa TBC ambaye sio tuu anakipaji, bali ni kichwa mbaya. Elisha Eliya ameuliza maswali mengi ya msingi Jaji Werema na Waziri Wasira wakitoa majibu ya chenga ya mwili.

Kuhusu kwanini unaitwa Muswada wa Mapitio ya Katiba iliyopo wakati wananchi wanataka katiba mpya?.
Jaji Werema alijibu, katiba ni living document, ikishaundwa, inaishi milele, hivyo hatuwezi kuwa na katiba mpya wakati tayari tunayo katiba iliyopo, hivyo ni lazima kuifanyia mapitio katiba iliyopo na kuiunda upya na kusisitiza katiba itakayopatikana baada ya mapitio hayo, ndio itakuwa ni Katiba Mpya.

Hoja kuhusu mamlaka kubwa ya rais pia yapanguliwa. Jaji Werema amesema, muswada huo unasomwa kwa mara ya pili na maoni bado yanapokelewa hivyo kama wabunge watatoa maoni madaraka ya rais yapunguzwe, serikali itayazingatia maoni hayo ila hailazimishwi kuyakubali naoni yoyote.

Kuhusu kushirijisha maoni ya wadau kwenye huu muswada mpya, wamedai kuwa baada ya kusomwa kwa mara ya kwanza, wameyazingatia maoni ya wadau, hata maoni ya wanajukwaa la katiba pia wameyazingatia, ila hawawezi kutajumuisha kila maoni, hivyo wameyachambua na kuyajumuisha yale walioona yanafaa.
Muda umemalizika, kipindi kimekwisha.

My Take.
1. Kwa vile muswada huo ulipowasilishwa kusomwa kwa mara ya kwanza, ulikataliwa na serikali ika u withdraw, hii inamaanisha muswada husika haukusomwa kwa mara ya kwanza, hivyo kihalali ulitakiwa kusomwa kwa mara ya kwanza.
2. Kwa walisoma sheria UDSM, wanawafahamu walimu magwiji wa mambo ya Katiba. Prof. Shivji, Prof. Kanywanyi na Prof. Fimbo ni miongoni mwao. Kitendo cha Jaji Werema kuwaponda maprofesa hawa na kitampekekea kupata laana kwa 'karma' ya uadilifu wa walimu hawa kumshukia.

Serikali inamtumia Prof. Kabudi kila inapotaka maoni ya wasomi wa sheria. Ilimtumia wakati wa kuzima hoja ya mgombea binafsi, juzi ndio imemtumia kuendesha semina ya wabunge kuhusu mchakato huu.

Pasco.

Update.

Muswada huo, bado haujawasilishwa bungeni mpaka sasa,, serikali imekacha kuuwasilisha leo.
Kamati ya Bunge ya Sheria na Katiba, inayoongozwa na Mhe. Pindi Chana, wameitana kukutana saa hizi, kujadili nini cha kufanya, labda sasa utawasilishwa kesho asubuhi na sio leo.

Hapo kwenye rangi ya purple, nadhani Jaji Werema anafanya projection: Anachukua udhaifu wake halafu anawatupia watu makini. Huu ni udhaifu mkubwa sana.

Hapo kwenye blue hasemi ukweli. Baadhi ya wabunge ambao wamependekeza kutolewe tafsiri kuhusu 'mitambo iliyotumika' na pia kwenye baadhi ya vipengele, Jaji Werema mwenyewe amesimama mara kadhaa kudai hivyo vifungu vibaki kama vilivyo na kwa hivyo haiwezekani kusema eti wabunge wataweza kujadili bungeni. Naona kama hawako free, hasa wale wanaotaka kuwepo na mabadiliko katika sheria ili kuwabana wanaofuja mali ya umma. Hata kwa hili la mwisho Jaji Werema amesimama mara kadhaa kutetea sheria isiwe kali sana kwa watu hao akidai "wabunge waache jazba."

Kama wakati wa sheria iliyokuwa ikikataza manunuzi ya mitambo chakavu (used), baadhi ya vigogo waliikiuka na kununua mitambo chakavu; je sasa hivi ambapo sheria inaruhusu kununua mitambo chakavu wakati wa dharura itakuwaje? Nani atashindwa kuona kuna dharura ya manunuzi ya mitambo chakavu kama anaona kufanya hivyo ana 10% commission? Uadilifu wa kusema: "tuwe wakali katika usimamizi wa sheria" umetoka wapi kama sheria zingine wanaozisimamia ndio wa kwanza kuzivunja? Kwa kweli, we are at the crossroads and what we see is grey colour and not black and white!
 
Wao wanafikiria kuwa tunasema huu ni mswada wa katiba yenyewe mpya. Sijui ni kitu gani kinawafanya wafikirie hatuna uwezo wa kusoma madudu yao.


Serikali na wabunge wa ccm wana madharau ya hali ya juu. Kila siku utawasikia wasima watu walio na mawazo tofauti kuwa 'wametumwa'. Walishaamua siku nyingi kuwa watanzania wengine (except wao) ni wajinga hawana uwezo wa kufikiri. Na hii ndio inawasumbua maana wanafikiri hizi kelele ni za wabunge wachache wa upinzani hivyo wanaona wapambane na hao watu wachache.
 
Jamani Tupeni UPDATES juu ya kinachojiri Bungeni sasa hivi maana bado tuko Ofisini wengine laini tunapenda kujua kinachoendelea jamani tusaidieni wa JF mlio Karibu na TV.
 
Wao wanafikiria kuwa tunasema huu ni mswada wa katiba yenyewe mpya. Sijui ni kitu gani kinawafanya wafikirie hatuna uwezo wa kusoma madudu yao.

Wanafanya makusudi kuwapotosha wananchi ili wanaharakati, wanamageuzi na wengine wote wanaoupinga muswada waonekane wana nia mbaya ama hila dhidi ya serikali. Si kwamba wanafikiri kwamba hamjui mnachokipinga, la hasha wanawaelewa sana lakini kwa kuwa hawana nia njema ndio sababu wanapotosha wananchi kwa kuwasingizia ninyi.
 
TBC wangekuwa basi na live feed kwenye channel yao...ingesaidia kweli kujua kinachoendelea. any updates jamani?
 
Serikali na wabunge wa ccm wana madharau ya hali ya juu. Kila siku utawasikia wasima watu walio na mawazo tofauti kuwa 'wametumwa'. Walishaamua siku nyingi kuwa watanzania wengine (except wao) ni wajinga hawana uwezo wa kufikiri. Na hii ndio inawasumbua maana wanafikiri hizi kelele ni za wabunge wachache wa upinzani hivyo wanaona wapambane na hao watu wachache.

Hawana kitu! Wameshikwa pabaya na sasa wanatapatapa tu! Reasoning yao so poor!
 
Back
Top Bottom