BUNGENI: Muswada wa mabadiliko ya katiba

Hadi sasa huu muswada ni wa kurekebisha katiba na sio kwa kutunga katiba mpya. Kwa Werema kuutetea ni sawa kabisa maana tangu hapo awali alisema waziwazi kuwa katiba ya sasa haina shida kama kuna jambo la kurekebisha basi watu waseme na litarekebishwa. Maneno haya ya Werema pia yalisemwa na Celina Kombani.

Kwa hiyo Serikali ya ccm haina nia ya kuandika katiba mpya - that's very obvious. Kama walikuwa na nia ya kuandika katiba mpya kwa nini hawataki kusikiliza maoni ya wananchi? Ni kitu gani kinawafanya watake kusoma huu muswada kwa mara ya pili? Ni ni lini muswada wa KUTUNGA katiba mpya uliwahi kupelekwa bungeni? Ule mwingine ulipelekwa tena kwa lugha ya kiingereza ulikuwa wa KUREKEBISHA katiba.

Naye Steven Wasira na utaalam gani kwenye mambo ya katiba kiasi kwamba ccm wanamtumia kuhubiri huu muswada uliojaa matatizo? Kwa nini watu kama Wasira na Werema wanajiona wanajua mambo ya katiba kuliko Prof Shivji? Shida kubwa ninayoona ni kwamba kuna gap kubwa sana kati ya ccm na wananchi. Wakishapata Ubunge hawa ccm ni kama wanajigeuza baraza la mawaziri tena mawaziri wasiosikiliza wale wanaowaongoza. Huu muswada unaweza kuipeleka kuzima ccm mapema kuliko ilivyokuwa iwe.

Ningeomba kuuliza, Spika wa bunge ana uwezo/nguvu gani katika hali kama hii ambapo serikali inaonekana waziwazi kwenda kinyume na public interest?

Spika yupi unayemwongelea??? Sijui kama kuna mtu anayeitwa Spika sasa anayeweza walau kuhoji maelekezo ya serikali!!

Tusubiri tuone....!
 
Swali linahusu maji kutoka jimbo la nkasi kwenye mji wa namanyere. jibu fedha hazijapatikana kuendeleza mradi huwo.
 
Huyu ni Mwanasheria Mkuu wa ajabu sana. Yaani hawa wote wanaopinga ni wajinga isipokuwa wao tu ndio wapo sahihi? Shivji, Kanywanyi, TLS, Jukwaa la Katiba, na wananchi wengine wote hawajui wanachokipinga?

Mimi nafikiri hatua iliyobaki ni moja, nayo ni wanaharakati wote na vyama vya upinzani kuibuka na mchakato sambamba na ule wa serikali ambao hawa bwana wamekamia kuupitisha wiki hii. Kisha kukusanya maoni sambamba na hiyo tume ya kwao na kuibuka na rasimu ya katiba mbadala. Itakapofika wakati wa kura ya maoni, ifanyike kampeni ya kura ya 'HAPANA' dhidi ya kura ya 'NDIYO' ya serikali.
 
Swali la nyongeza mpango gani wa haraka kusaidia upatikanaji wa maji? Jibu wamekasimu mamlaka hayo kwenye mamlaka ya mjibu wa sumbawanga
 
Jamani tutumie uwanja huu kuchambua,kukosoa,na kujuzana mambo yanayoendelea bungeni.
Mana sio kila mtu mwenye access na TV.
Nawasilisha.
Kikao cha bunge kimeanza asubuhi hii na muswada tajwa haijawasilishwa!.

Kwa kawaida vikao huanza na hati za kuwasilishwa mezani. Labda utawasilishwa baada ya kipindi cha maswali na majibu.
 
Swali linahusu maji kutoka jimbo la nkasi kwenye mji wa namanyere. jibu fedha hazijapatikana kuendeleza mradi huwo.

nakumbuka kikwete alishawahi kusema kwenye safari zake na hotuba zake huko kwa wazungu kuwa AFRIKA HAIJAENDELEA KWA SABABU HAINA PESA: sasa jibu gani hili? Nani hajui kuwa pesa haipo ndio maana mradi haijaanza .majibu yao bhana aa
 
hivi hawa watu wanafikiria hatujui tunachopinga ni nini? Tunachopinga ndicho hicho kinachowasilishwa. Tunapinga mpango na utaratibu ambao umewekwa kwa ajili ya kukusanya maoni na hatimaye kuandika Katiba mpya. Hakuna mtu mwenye akili timamu anayefikiria huu mswada ni mswada wa Katiba mpya. Tunaelewa kuwa ni mswada ambao una lengo la kuweka utaratibu wa hatimaye kufikia Katiba mpya, unaweka vyombo, taratibu na sheria ya kufikia Katiba Mpya. Na hicho ndicho tunachokipinga. Tunakipinga kwa sababu kubwa mbili.

a. Rais amechukua madaraka ya wananchi kuandika Katiba yao
b. Utaratibu mzima utasimamiwa na CCM na wajumbe wengi wa CCM na jhivyo kufanya Katiba mpya kuwa ni Katiba ya CCM.

Hili lina ugumu gani wa kulielewa?
Whats the alternative??????
Ningependa CUF, CDM, NCCR, watoe alternatives za kukusanya maoni, jinsi ya kuunda tume na composition yake........ etc
 
Huyu ni Mwanasheria Mkuu wa ajabu sana. Yaani hawa wote wanaopinga ni wajinga isipokuwa wao tu ndio wapo sahihi? Shivji, Kanywanyi, TLS, Jukwaa la Katiba, na wananchi wengine wote hawajui wanachokipinga?

Mimi nafikiri hatua iliyobaki ni moja, nayo ni wanaharakati wote na vyama vya upinzani kuibuka na mchakato sambamba na ule wa serikali ambao hawa bwana wamekamia kuupitisha wiki hii. Kisha kukusanya maoni sambamba na hiyo tume ya kwao na kuibuka na rasimu ya katiba mbadala. Itakapofika wakati wa kura ya maoni, ifanyike kampeni ya kura ya 'HAPANA' dhidi ya kura ya 'NDIYO' ya serikali.
Naomba utoe mfano, nani achague/teue tume?
 
Kwa mujibu wa ratiba ya bunge leo. Muswada wa katiba unasomwa kwa mara ya pili. Kinachoniuma. Kweli viongozi wa bunge ni viziwi kiasi hiki? Wanainchi wameshakataa kusomwa mara ya pili. Kinachofanya waharakishe ni nini wakati katiba ni ya wananchi wote?
 
Kipindi hicho, kimeongozwa na mtangazaji Elisha Eliya , ambaye ni mmoja wa watangazaji mahiri kabisa wa TBC ambaye sio tuu anakipaji, bali ni kichwa mbaya.

Elisha Eliya ameuliza maswali mengi ya msingi Jaji Werema na Waziri Wasira wakitoa majibu ya chenga ya mwili.

Ni kichwa maji mbaya! Hakuwa na maswali yeyote ya maana zaidi ya kuuliza maswali yaliyoandaliwa kuisaidia serikali. Werema na wassira hawajui hata wanachotetea, hawakuweza kuelezea hoja za msingia zaidi ya kujaribu kueleza kuwa eti muswada si wa katiba mpya bali wa mchakato wa marejeo ya katiba!

Waandishi wetu wa habari walio wengi wana uelewa mdogo sana wa masuala ya msingi ya nchi yetu. Nawapongeza wale wote ambao hutumia taaluma zao kwa manufaa ya taifa badala ya kuwasafisha na kuwalamba miguu waajiri wao.
 
Kifuatacho ni maswali na majibu.
hakuna kitu kincho niudhi katika bunge kama kipindi hiki kwani maswali kila siku ni yale yale maijbu yale yale wanapoteza muda mwingi sana hebu fikiri bunge kukaa miezi 3 ,siku 5 kwa week j3-ijumaa ,kila siku maswali ni saa 1 mara mwezi yaani 5 X 4=20X3=60 kwa hio masaa sitini ukifanya mara miaka 5 =300 chakujiuliza nini kimefanyika kutokana na kipindi cha maswali nahio ni bunge la budget pekee bado vile vikao vingine ,kila mbunge anuliza bara bara maji simu nk
 
Huyu ni Mwanasheria Mkuu wa ajabu sana. Yaani hawa wote wanaopinga ni wajinga isipokuwa wao tu ndio wapo sahihi? Shivji, Kanywanyi, TLS, Jukwaa la Katiba, na wananchi wengine wote hawajui wanachokipinga?

Mimi nafikiri hatua iliyobaki ni moja, nayo ni wanaharakati wote na vyama vya upinzani kuibuka na mchakato sambamba na ule wa serikali ambao hawa bwana wamekamia kuupitisha wiki hii. Kisha kukusanya maoni sambamba na hiyo tume ya kwao na kuibuka na rasimu ya katiba mbadala. Itakapofika wakati wa kura ya maoni, ifanyike kampeni ya kura ya 'HAPANA' dhidi ya kura ya 'NDIYO' ya serikali.

Dr Mkumbo, nakuheshimu sana. Huwa naheshimu sana michango yako kwa maendeleo ya Taifa hili. Nilimsikiliza Werema (A.G) na Wassira, kwa kweli sikuelewa kama watu hawa wanajua hasa kinachozungumzwa au wameamua kuziba fahamu zao na kufuata hisia zao za kisiasa na woga wa kijinga. Hawakuwa na hoja za kumshawishi mtu yeyote mwenye fikra huru juu ya azma yao ya kuendelea na muswada huu hatari kwa ustawi wa Taifa letu.

Naungana nawe katika wazo la kuandaa muswada mbadala na kuwa na katiba mbadala dhidi ya hiyo ya serikali.
 
hakuna kitu kincho niudhi katika bunge kama kipindi hiki kwani maswali kila siku ni yale yale maijbu yale yale wanapoteza muda mwingi sana hebu fikiri bunge kukaa miezi 3 ,siku 5 kwa week j3-ijumaa ,kila siku maswali ni saa 1 mara mwezi yaani 5 X 4=20X3=60 kwa hio masaa sitini ukifanya mara miaka 5 =300 chakujiuliza nini kimefanyika kutokana na kipindi cha maswali nahio ni bunge la budget pekee bado vile vikao vingine ,kila mbunge anuliza bara bara maji simu nk

Asante kwa uchambuzi makini
 
Kwa mujibu wa ratiba ya bunge leo. Muswada wa katiba unasomwa kwa mara ya pili. Kinachoniuma. Kweli viongozi wa bunge ni viziwi kiasi hiki? Wanainchi wameshakataa kusomwa mara ya pili. Kinachofanya waharakishe ni nini wakati katiba ni ya wananchi wote?

Iwe koku! kwani si tunataka katiba kabla ya mwaka 2014 ili itumike mwaka 2015 na kumbuka bado tuna katiba na nchi haija pinduliwa kuifanya katiba hii kuwa batili hovyo kinacho pitishwa sii katiba ni sheria inatungwa kuhalalisha uundwaji wa katiba mpya badala ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, vinginevyo mwambie shemeji yako dokta slaa apindue nchi ili aunde katiba mpya kwa mwaka mmoja kama alivyoahidi mwaka jana. vinginevyo kwa uswahili wetu itafika mwaka 2015 hatuna katiba wala nini. tatizo ni uswahili! we talk too much!! iwe bojo!!
 
huku kishakata umeme..daaah ngeleja tumekukosea nini shemeji

kila siku anakungeleja wewe tuu lazma kuna azma yake, heeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee na hapa ulikata ila umerudi ngoja nikae kimya usijekatika mazima
 
Werema, Wasira wote hawa ni wateule wa rais hawawezi kutoa maoni yanayoweza kusimama upande wa wanyonge. Wanafanya hivyo si kwa matakwa yao ila kwa matakwa ya bosi wao. Wamesahau kusimamia haki. Sishangai sana ninapoona hali kama hii, tatizo ni mfumo tulionao!
 
Back
Top Bottom