Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,466
- 113,551
Wanabodi wenye access na TBC, angalieni TBC Live kipindi cha Jambo Tanzania. Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Warema na Waziri Stephen Wasira, wanahojiwa live kuhusu kuwasilishwa Muswada wa Sheria wa Kuundwa Tume ya Kukusanya Maoni ya Kubadilisha Katiba.
aji Werema amewataka wanasheria nchini kuwa wakweli, wasiwapotoshe wananchi, kwanza muswada huo sio muswada wa katiba mpya kama wanasheria wanavyohubiri. Muswada unaosomwa kwa mara ya pili, ni muswada wa kukusanya maoni jinsi ya kuunda tume ya kukusanya maoni na sio muswada wa katiba mpya.
Jaji Werema na Waziri Wasira, wamelishambulia Jukwaa la Katiba na wale wote waliotoa maoni hasi kuhusu kusomwa kwa mara ya pili kwa muswada wakiwataja kwa majina akiwemo Deus Kibamba, Prof. Issa Shivji, Prof. Josephat Kanywanyi na wengine wote wanaopinga muswada huo usiwasilishwe wakiwemo Chama cha Wabasheria Tanzania, TLS, wametajwa kuwa sio wakweli bali wanapinga kwa ushabiki tuu.
Kipindi hicho, kimeongozwa na mtangazaji Elisha Eliya , ambaye ni mmoja wa watangazaji mahiri kabisa wa TBC ambaye sio tuu anakipaji, bali ni kichwa mbaya. Elisha Eliya ameuliza maswali mengi ya msingi Jaji Werema na Waziri Wasira wakitoa majibu ya chenga ya mwili.
uhusu kwanini unaitwa Muswada wa Mapitio ya Katiba iliyopo wakati wananchi wanataka katiba mpya?.
Jaji Werema alijibu, katiba ni living document, ikishaundwa, inaishi milele, hivyo hatuwezi kuwa na katiba mpya wakati tayari tunayo katiba iliyopo, hivyo ni lazima kuifanyia mapitio katiba iliyopo na kuiunda upya na kusisitiza katiba itakayopatikana baada ya mapitio hayo, ndio itakuwa ni Katiba Mpya.
Hoja kuhusu mamlaka kubwa ya rais pia yapanguliwa. Jaji Werema amesema, muswada huo unasomwa kwa mara ya pili na maoni bado yanapokelewa hivyo kama wabunge watatoa maoni madaraka ya rais yapunguzwe, serikali itayazingatia maoni hayo ila hailazimishwi kuyakubali naoni yoyote.
Kuhusu kushirijisha maoni ya wadau kwenye huu muswada mpya, wamedai kuwa baada ya kusomwa kwa mara ya kwanza, wameyazingatia maoni ya wadau, hata maoni ya wanajukwaa la katiba pia wameyazingatia, ila hawawezi kutajumuisha kila maoni, hivyo wameyachambua na kuyajumuisha yale walioona yanafaa.
Muda umemalizika, kipindi kimekwisha.
My Take.
1. Kwa vile muswada huo ulipowasilishwa kusomwa kwa mara ya kwanza, ulikataliwa na serikali ika u withdraw, hii inamaanisha muswada husika haukusomwa kwa mara ya kwanza, hivyo kihalali ulitakiwa kusomwa kwa mara ya kwanza.
2. Kwa walisoma sheria UDSM, wanawafahamu walimu magwiji wa mambo ya Katiba. Prof. Shivji, Prof. Kanywanyi na Prof. Fimbo ni miongoni mwao. Kitendo cha Jaji Werema kuwaponda maprofesa hawa na kitampekekea kupata laana kwa 'karma' ya uadilifu wa walimu hawa kumshukia.
Serikali inamtumia Prof. Kabudi kila inapotaka maoni ya wasomi wa sheria. Ilimtumia wakati wa kuzima hoja ya mgombea binafsi, juzi ndio imemtumia kuendesha semina ya wabunge kuhusu mchakato huu.
Pasco.
Update.1
Muswada huo, bado haujawasilishwa bungeni mpaka sasa,, serikali imekacha kuuwasilisha leo.
Kamati ya Bunge ya Sheria na Katiba, inayoongozwa na Mhe. Pindi Chana, wameitana kukutana saa hizi, kujadili nini cha kufanya, labda sasa utawasilishwa kesho asubuhi na sio leo.
Update. 2
Muswada uliwasilishwa jana jioni na majadiliano yanaendelea.
aji Werema amewataka wanasheria nchini kuwa wakweli, wasiwapotoshe wananchi, kwanza muswada huo sio muswada wa katiba mpya kama wanasheria wanavyohubiri. Muswada unaosomwa kwa mara ya pili, ni muswada wa kukusanya maoni jinsi ya kuunda tume ya kukusanya maoni na sio muswada wa katiba mpya.
Jaji Werema na Waziri Wasira, wamelishambulia Jukwaa la Katiba na wale wote waliotoa maoni hasi kuhusu kusomwa kwa mara ya pili kwa muswada wakiwataja kwa majina akiwemo Deus Kibamba, Prof. Issa Shivji, Prof. Josephat Kanywanyi na wengine wote wanaopinga muswada huo usiwasilishwe wakiwemo Chama cha Wabasheria Tanzania, TLS, wametajwa kuwa sio wakweli bali wanapinga kwa ushabiki tuu.
Kipindi hicho, kimeongozwa na mtangazaji Elisha Eliya , ambaye ni mmoja wa watangazaji mahiri kabisa wa TBC ambaye sio tuu anakipaji, bali ni kichwa mbaya. Elisha Eliya ameuliza maswali mengi ya msingi Jaji Werema na Waziri Wasira wakitoa majibu ya chenga ya mwili.
uhusu kwanini unaitwa Muswada wa Mapitio ya Katiba iliyopo wakati wananchi wanataka katiba mpya?.
Jaji Werema alijibu, katiba ni living document, ikishaundwa, inaishi milele, hivyo hatuwezi kuwa na katiba mpya wakati tayari tunayo katiba iliyopo, hivyo ni lazima kuifanyia mapitio katiba iliyopo na kuiunda upya na kusisitiza katiba itakayopatikana baada ya mapitio hayo, ndio itakuwa ni Katiba Mpya.
Hoja kuhusu mamlaka kubwa ya rais pia yapanguliwa. Jaji Werema amesema, muswada huo unasomwa kwa mara ya pili na maoni bado yanapokelewa hivyo kama wabunge watatoa maoni madaraka ya rais yapunguzwe, serikali itayazingatia maoni hayo ila hailazimishwi kuyakubali naoni yoyote.
Kuhusu kushirijisha maoni ya wadau kwenye huu muswada mpya, wamedai kuwa baada ya kusomwa kwa mara ya kwanza, wameyazingatia maoni ya wadau, hata maoni ya wanajukwaa la katiba pia wameyazingatia, ila hawawezi kutajumuisha kila maoni, hivyo wameyachambua na kuyajumuisha yale walioona yanafaa.
Muda umemalizika, kipindi kimekwisha.
My Take.
1. Kwa vile muswada huo ulipowasilishwa kusomwa kwa mara ya kwanza, ulikataliwa na serikali ika u withdraw, hii inamaanisha muswada husika haukusomwa kwa mara ya kwanza, hivyo kihalali ulitakiwa kusomwa kwa mara ya kwanza.
2. Kwa walisoma sheria UDSM, wanawafahamu walimu magwiji wa mambo ya Katiba. Prof. Shivji, Prof. Kanywanyi na Prof. Fimbo ni miongoni mwao. Kitendo cha Jaji Werema kuwaponda maprofesa hawa na kitampekekea kupata laana kwa 'karma' ya uadilifu wa walimu hawa kumshukia.
Serikali inamtumia Prof. Kabudi kila inapotaka maoni ya wasomi wa sheria. Ilimtumia wakati wa kuzima hoja ya mgombea binafsi, juzi ndio imemtumia kuendesha semina ya wabunge kuhusu mchakato huu.
Pasco.
Update.1
Muswada huo, bado haujawasilishwa bungeni mpaka sasa,, serikali imekacha kuuwasilisha leo.
Kamati ya Bunge ya Sheria na Katiba, inayoongozwa na Mhe. Pindi Chana, wameitana kukutana saa hizi, kujadili nini cha kufanya, labda sasa utawasilishwa kesho asubuhi na sio leo.
Update. 2
Muswada uliwasilishwa jana jioni na majadiliano yanaendelea.