MSWADA unasomwa kwa mara ya 2, angalia TBC1, spika anatetea mswada kusomwa kwa mara ya 2.
Kazi ipo
Kazi ipo
Wanabodi, hatimaye Muswada wa Kukusanya Maoni kuhusu Mabadiliko ya Katiba watinga rasmi bungeni na kusomwa kwa mara ya pili!.
Muswada huo umewasilishwa kikao hiki cha jioni. Spika wa Bunge, Mhe. Anna Makinda alianza kwa kuitetea serikali kwa nguvu zake zote japo sauti yake ilikuwa ikitetemeka.
Sasa Waziri wa Sheria, Mhe. Celina Kombani ndio anausoma na kutetea uwasilishaji wa muswada huo kwa mara ya pili.
Nadhani ninavyomsikiliza Mama Kombani, kwa maoni yangu binafsi kama Pasco wa jf, nadhani anajikanyaga kanyaga tuu, kwani ulipowasilishwa kwa mara ya kwanza, si ulikataliwa?!.
Hebu na tusubiri jinsi wanasheria, watakavyomchana Mama Kombani!.