Bungeni: Kamati ya kuchunguza tuhuma za rushwa yaundwa

Wana JF nimekuwa nasikiliza taarifa ya habari ya CLOUDS FM saa 12 jioni nikasikia kwamba Spika Anna Makinda ameteua kamati ya wabunge watakaofanya uchunguzi wa tuhuma za rushwa zinazowakabili baadhi ya wabunge. Moja ya jina nililolisikia kwenye kamati hiyo ni Gozibert Blandes Mbunge wa Karagwe, Nilijiuliza kama bunge limekosa watu wasio na doa kuwapo kwenye kamati ya uchunguzi.

Huyu bwana kwanza si mbunge harali, alitangazwa mshindi mbele ya mtutu wa bunduki, askari walitumwa toka Bukoba mjini kwenda karagwe kuwatisha wananchi waliokuwa wanasubiri matokeo ya uchaguzi. Alisindikizwa na askari mpaka airport Bukoba na sasa hivi hawezi kukanyaga huko wananchi wana hasira naye. Sasa mtu kama huyu anatoa wapi moral authority ya kwenda kuwahoji watuhumiwa wakati yeye ni mtuhumiwa wa vote rigging?

Nawakilisha.
 
Nia yao si kuja na majibu sahihi na kuwawajibisha bali ni kupoteza muda then wapotezee kwakutokuja na majibu
 
Wajumbe wengine, ni Hasan Ngwilizi, John Chiligati, Said Alfi na Mwanamama mwingine ambaye jina lake sijalinyaka vizuri
 
yaani hadi Chiligati????

Hii ni kamati ya maandalizi ya harusi labda.
 
Sioni mtu hapo, tangu mwanzo nilizikataa kabisa hizi tume sijui kamati!!!!!
 
Nahamia Somalia Mimi I'm seek and tired of this poor govt I'll rather be a slave somalia than being a resident I'n this corrupt counry.
wait... ngoja tuende wote subiri nafungasha
 
Wana JF nimekuwa nasikiliza taarifa ya habari ya CLOUDS FM saa 12 jioni nikasikia kwamba Spika Anna Makinda ameteua kamati ya wabunge watakaofanya uchunguzi wa tuhuma za rushwa zinazowakabili baadhi ya wabunge. Moja ya jina nililolisikia kwenye kamati hiyo ni Gozibert Blandes Mbunge wa Karagwe, Nilijiuliza kama bunge limekosa watu wasio na doa kuwapo kwenye kamati ya uchunguzi.

Huyu bwana kwanza si mbunge harali, alitangazwa mshindi mbele ya mtutu wa bunduki, askari walitumwa toka Bukoba mjini kwenda karagwe kuwatisha wananchi waliokuwa wanasubiri matokeo ya uchaguzi. Alisindikizwa na askari mpaka airport Bukoba na sasa hivi hawezi kukanyaga huko wananchi wana hasira naye. Sasa mtu kama huyu anatoa wapi moral authority ya kwenda kuwahoji watuhumiwa wakati yeye ni mtuhumiwa wa vote rigging?

Nawakilisha.

unqmteua mbunge asiye halali kuchungunza mambo yasiyo halali...huu ni upuuzi mpevu kabisa kuwahi kuushudia...hii ni team hewa na dhahiri itakuja na majibu hewa
 
SPIKA wa Bunge, Anne Makinda ameunda kamati ndogo ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuchunguza tuhuma za wabunge kuhongwa, huku Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, akitajwa kuwa mmoja wa watakaolazimika kwenda kutoa ushahidi.


Mbali na kuunda kamati hiyo, inayoongozwa na Mbunge wa Mlalo, Hassan Ngwilizi (CCM), pia ameipa Kamati hiyo hadidu za rejea na muda wa wiki mbili kukamilisha kazi hiyo.

“Baada ya kushauriana, imeonekana suala hili litafanyika vizuri kwa kuunda kamati ndogo ya wabunge watano ili ifanye haraka, kazi itafanyika kwa wiki mbili na taarifa itawasilishwa kwa Spika,” alisema Spika Makinda.

<<<<<HABARI KAMILI>>>>>


 
waziri wa zamani mh mungai na katibu wa zaman wa TFF ndg mwakalebela wanasakwa na TAKUKURU KWa tuhuma za rushwa kipind cha uchaguzi.
 
Jaman zengwe lao halijaisha hawa????na wanasakwa hawajulikan walipo,na je ni hao tuuuuuuu
 
Mbona Mwakalebela alishasafishwa na mahakama hizohizo za magamba!?
 
Naomba mwenye kuweza kutuwekea hansard ya bunge yenye kumbukumbu ya michango ya wabunge na kauli ya waziri siku anafanya majumuisho ya bajeti yake ya Nishati na Madini atuwekee ili kuweka kumbukumbu sawa!
 
Wanasakwa kwani wametoroka au wamefichama? Hebu turekebishe hiyo title.
 
Back
Top Bottom