Bungeni - Highness Kiwia (Ilemela) atoa semina kwa Wabunge

Kwa hili la Tanesco sikubaliani na kiwia kuwa hawana walilofanya. Tanesco ya miaka iliyopita siyo hii ya leo nafikiri bado baadhi ya watu wamebaki na historia, Tanesco ya sasa inafanya kazi zake kwa mpangilio unaoeleweka, sikutarajia hata siku moja kuwa nitakuja kuwasha umeme wa Tanesco ila nataka nikuhakikishie kuwa nilipofanya mchakato wa ufuatiliaji nilishangaa jinsi Tanesco walivyokuwa wanafanya shughuli zao kwa uhakika kiasi cha mtu kama mimi kupata huduma hiyo bila kutoa chochote ndani ya week tatu toka nilipe kiasi cha pesa kilichohitajika, awali nilikuwa natumia jenereta, kwa siku tatu petrol ya sh.10,000/= sasa hivi hiyo elfu kumi napata uniti kama sikosei zaidi ya hamsini ambapo nazitumia kwa zaidi ya week tatu au mwezi kabisa, sasa jamani ni kweli hawajafikia hicho kiwango kinachotakiwa ila kwa sasa wanajitahidi tuwatie moyo matatizo mengine yako nje kabisa ya uwezo wa Tanesco.
wewe utakuwa mfanyakazi wa tanesco au ulitumia yale mambo ya undugunaizesheni
 
Huyu bwana nakumbuka nilikaa naye hapo nyuma kabla ya kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu uliopita pale Arusha aikiwa na muheshimiwa mwenzake ambaye sasa hivi ni mbunge wa Arusha mjini muheshimiwa GodBless Lema kwakweli alinipa hamasa kubwa sana wakati akiniambia anajikita katika kugombe jimbo la Ilemela Mwanza, amekomaa sana na anauchungu sana wa kuliletea jimbo lake maendeleo. Keep it Up Highness Kiwia kwa kutuonyesha vijana kua nasi tunaweza.

Highness-Kiwia-240x300.jpg

Kimtokacho mtu ndicho kimchafuacho twasoma hivyo kwenye misahafu ya maandiko matakatifu. Anachoongea mtu kinaonyesha fikra ndani ya moyo wake. Wabunge wengi wa kuchaguliwa ndani ya Chadema hawajavutwa na umaskini wa maisha yao, ingawa hawawezi kukosekana baadhi walioingia bungeni kwa mvuto huo. Utakuta wengi wanaopigania haki ni wali wajasirimali waliojitosha kuteteha haki za wananchi kutokana na kuporwa na viongozi jeuri. Naamini kila chenye mwanzo kina mwisho na dalili ya mwisho wa viongozi jeuri inakaribia kwani kila wanakogeukia wanashtukia kugonga ukuta na kurudi walikotoka, hataima watakasa pakutokea ndio itabaki historia na taifa jipya la kizazi kipya kujengeka.
 
Kwa hili la Tanesco sikubaliani na kiwia kuwa hawana walilofanya. Tanesco ya miaka iliyopita siyo hii ya leo nafikiri bado baadhi ya watu wamebaki na historia, Tanesco ya sasa inafanya kazi zake kwa mpangilio unaoeleweka, sikutarajia hata siku moja kuwa nitakuja kuwasha umeme wa Tanesco ila nataka nikuhakikishie kuwa nilipofanya mchakato wa ufuatiliaji nilishangaa jinsi Tanesco walivyokuwa wanafanya shughuli zao kwa uhakika kiasi cha mtu kama mimi kupata huduma hiyo bila kutoa chochote ndani ya week tatu toka nilipe kiasi cha pesa kilichohitajika, awali nilikuwa natumia jenereta, kwa siku tatu petrol ya sh.10,000/= sasa hivi hiyo elfu kumi napata uniti kama sikosei zaidi ya hamsini ambapo nazitumia kwa zaidi ya week tatu au mwezi kabisa, sasa jamani ni kweli hawajafikia hicho kiwango kinachotakiwa ila kwa sasa wanajitahidi tuwatie moyo matatizo mengine yako nje kabisa ya uwezo wa Tanesco.
Nadhani mkuu upo Dar, fikiri kiTanzania zaidi.
 
shoss acha udini na ukabila tukiamua tudili nawewe sijui utuambiaje usituletee siasa za maji taka highness kiwia ni mtoto wa mji wenye miamba kazaliwa na kukulia hapa sisi ndio wapiga kura wake tunayemfahamu na tulimchagua kwa kishindo
 
10lukuvi.jpg

Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Willium Lukuvi
akifuatilia mjadala wa Bajeti Bungeni mjini Dodoma jana

Mbunge wa Ilemela (Chadema) Highnes Kiwia ambaye aliiponda bajeti hiyo na kuipongeza bajeti iliyotolewa na wapinzani akisema ndiyo iliyopaswa kutekelezeka.

"Bajeti mbadala ilipaswa kusomwa na positive mind kwani ikisomwa na negative mind sio tu msomaji ataona giza, bali atatumbukia gizani," alisema Kiwia na kuongeza:

"Sisi tunachofanya sio kubeza mafanikio, ila tunasema mafaniko yaliyopo hayaendani na wingi wa rasilimali tulizonazo, hatusemi hakuna kilichofanyika. Nyerere alisema, ili kuwa na maendeleo tunahitaji viti vitatu; watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora hakutaja fedha.

"Alisema (Nyerere) hatuwaondoi wakoloni kwa sababu tunachukia rangi zao, ni matendo yao. Sasa mkoloni wa leo ni ufisadi. hakuna namna Tanzania tukaondokana na umaskini kama hatuwezi kuondoa ufisadi."

Mbunge huyo ambaye ametishia kuikwamisha bajeti hiyo aligeukia sekta ya umeme akimtaka waziri Ngeleja kuongeza kasi ya utendaji wake ili huduma hiyo iwafikie watu wengi zaidi kuliko ilivyo sasa. "Namwambia ndugu yangu, Ngeleja, watu hawataki mahesabu ya Megawati, wanataka umeme," alisema.


Mwananchi

Well said, CDM hivyo vichwa mmetoa wapi? Halafu pia huwa wanapenda kutaja kilometers za barabara, watu wanataka barabara nzuri za lami sio unatajataja kilometers kila siku.
 
Viongozi wetu hawayaoni matatizo ya watanzania, wanafunzi wanakaa chini madarasani(kama yapo), wakati mawaziri wanatembelea magari ya bei mbaya, hata kama nchi ni masikini tungewaona wapo makini kama kidogo kilichopo tungegawana. AT LEAST MADAWATI SHULENI.
 
Mohamed Shossi said:
Ni mbunge wa Kibosho kwani si wa jimbo mojawapo pale rock city?

Mohamed,

..you should not engage na mambo ya ubaguzi-baguzi kama haya.

..wananchi wa Ilemela wameamua kumchagua what is the problem?

..hivi na wewe ukigombea Korogwe na kushinda halafu watu waanze kunung'unika kwamba una asili ya Kiarabu utajisikia namna gani?
 
  • Thanks
Reactions: LAT
Kwa hili la Tanesco sikubaliani na kiwia kuwa hawana walilofanya. Tanesco ya miaka iliyopita siyo hii ya leo nafikiri bado baadhi ya watu wamebaki na historia, Tanesco ya sasa inafanya kazi zake kwa mpangilio unaoeleweka, sikutarajia hata siku moja kuwa nitakuja kuwasha umeme wa Tanesco ila nataka nikuhakikishie kuwa nilipofanya mchakato wa ufuatiliaji nilishangaa jinsi Tanesco walivyokuwa wanafanya shughuli zao kwa uhakika kiasi cha mtu kama mimi kupata huduma hiyo bila kutoa chochote ndani ya week tatu toka nilipe kiasi cha pesa kilichohitajika, awali nilikuwa natumia jenereta, kwa siku tatu petrol ya sh.10,000/= sasa hivi hiyo elfu kumi napata uniti kama sikosei zaidi ya hamsini ambapo nazitumia kwa zaidi ya week tatu au mwezi kabisa, sasa jamani ni kweli hawajafikia hicho kiwango kinachotakiwa ila kwa sasa wanajitahidi tuwatie moyo matatizo mengine yako nje kabisa ya uwezo wa Tanesco.

Unauhakikika na unachosema mkuu
watu tumesota kupata umeme kama vile tunapewa bure.....tena ukiwa unatakiwa kuweka nguzo ndio utajua hii ni Tanzania zaidi ya uijuavyo
 
Hawa watoto wanafurahisha wamepikwa wakapikika,wanastahili kwa kweli pongezi kwa kutujuza mengi
 
Actions gani unataka Shossi? Wakiitisha maandamano wanaambiwa wanachochea fujo na kuhatarisha amani, wanatupwa lumande na kubambikwa kesi...wakisema fungeni milango bungeni tuchapane makofi ili watu wawe serious wanaambiwa 'wahuni'...wakisema bungeni sio sehemu ya kuuza sura wanaombewa miongozo ya spika eti wanatumia lugha za 'mtaani'...wakirudisha mpambano bungeni wanaambiwa longo longo 'actions speak louder! Wafanyaje sasa?

The major impact, CCM are seeing opposition parties on negative for individual benefits
 
Kwa hili la Tanesco sikubaliani na kiwia kuwa hawana walilofanya. Tanesco ya miaka iliyopita siyo hii ya leo nafikiri bado baadhi ya watu wamebaki na historia, Tanesco ya sasa inafanya kazi zake kwa mpangilio unaoeleweka, sikutarajia hata siku moja kuwa nitakuja kuwasha umeme wa Tanesco ila nataka nikuhakikishie kuwa nilipofanya mchakato wa ufuatiliaji nilishangaa jinsi Tanesco walivyokuwa wanafanya shughuli zao kwa uhakika kiasi cha mtu kama mimi kupata huduma hiyo bila kutoa chochote ndani ya week tatu toka nilipe kiasi cha pesa kilichohitajika, awali nilikuwa natumia jenereta, kwa siku tatu petrol ya sh.10,000/= sasa hivi hiyo elfu kumi napata uniti kama sikosei zaidi ya hamsini ambapo nazitumia kwa zaidi ya week tatu au mwezi kabisa, sasa jamani ni kweli hawajafikia hicho kiwango kinachotakiwa ila kwa sasa wanajitahidi tuwatie moyo matatizo mengine yako nje kabisa ya uwezo wa Tanesco.

Huo umeme kwa wiki unao mara ngapi nyumbani kwako?!!!. Yawezekana umeajiriwa na mtu. Huku mjini bila Jenereta ofisi haiendeki. Wewe unashangilia. Ni bonus kiasi gani unapoteza kwa kulipia mafuta ya jenereta ofisini kwako. Kazi yako haiendani na matumizi ya umeme?? Funguka macho. Kuna watu wanauhitaji umeme na uwezo wa kulipia wanao lakini namna ya kuupata. Fikiria uko mbali na nguzo za umeme ulipo na nguzo moja si chini ya Tzs.900,000 x 5 = 4,500,000/=. Acha ushabiki. Inalazimu watu kuungana vikundi kama vya saccos ili kuomba umeme. Huu ni ujinga nambari one. Umeme uje ukukute sio uangaike kuutafuta has if ni bure.
 
Ubaguzi haujengi mkuu. Lakini kuwekeza kwenye elimu bora, miundo bora, sera makini na utawala bora zinaleta mabadiliko makubwa kwenye nchi husika.
 
Mohamed,

..you should not engage na mambo ya ubaguzi-baguzi kama haya.

..wananchi wa Ilemela wameamua kumchagua what is the problem?

..hivi na wewe ukigombea Korogwe na kushinda halafu watu waanze kunung'unika kwamba una asili ya Kiarabu utajisikia namna gani?

Aliyekuwa Gavana wa Califonia, Anold S. alizaliwa ulaya na kukulia marekani, wamarekani, Obama kazaliwa Hawaii baadaye kachaguliwa kuwa seneta wa Illnois (Chikago). Viongozi wengi tanzania wanafanya kazi nje ya mikoa waliyozaliwa. Tunaukataa huu ubaguzi wa mkoa, kanda na aina zote za kubaguana kwa nguvu zote. Sote ni watanzania wenye haki popote mradi sifa zinazotakiwa anazo.
 
Candid Scope said:
Aliyekuwa Gavana wa Califonia, Anold S. alizaliwa ulaya na kukulia marekani, wamarekani, Obama kazaliwa Hawaii baadaye kachaguliwa kuwa seneta wa Illnois (Chikago). Viongozi wengi tanzania wanafanya kazi nje ya mikoa waliyozaliwa. Tunaukataa huu ubaguzi wa mkoa, kanda na aina zote za kubaguana kwa nguvu zote. Sote ni watanzania wenye haki popote mradi sifa zinazotakiwa anazo.

Candid Scope,

..asante!!!

..Tanzania tunayoitaka ni ile ambayo Mtanzania atakuwa comfortable kuishi mahali popote pale ktk nchi yetu.

..ifike mahali Mtanzania awe judged kutokana na tabia na matendo yake siyo kabila lake,rangi, au dini.

..wananchi wa Ilemela wameonyesha mfano kwa kumchagua Ubunge Mtanzania mwenzao ambaye jina lake inaelekea halina asili na Ilemela.

..binafsi nadhani tu-encourage mwenendo huo badala ya kuupiga vita kama Ritz na Mohamed Shossi wanavyofanya hapa.
 
Back
Top Bottom