Bungeni: CCM kupitia Anne Makinda yaliumbua gazeti lake Jambo Leo. Yasema linaandika uongo!

Nikupateje

JF-Expert Member
Dec 22, 2009
1,334
988
Dakika tano zilizopita Mh. John Mnyika aliinuka kutoa hoja aungwe mkono na bunge zima. Hoja yenyewe ilikuwa ni kuhusu jambo linalohusu mamlaka ya bunge kwamba liweke ukomo kupewa taarifa ile ya David Jairo.

Mh. Mnyika aliuliza kwanza kutokana na swali lake Alhamis iliyopita kwa Waziri Mkuu aliyejibu kwamba taarifa ya suala lile ni kweli imechelewa kufika lakini itakuja bungeni wakati wowote kuanzia sasa.

Lakini Mnyika akiwa ameshika gazeti la JAMBO LEO la jana amelisoma likisema REPORT YA JAIRO IKO KWA SPIKA NA IMEOZEA PALE. BUNGE LACHAMBULIWA KAMA KARANGA.

Hivyo, Mnyika akataka kujua ukweli ni upi. Je, Pinda alikuwa muongo aliposemakuwa ripoti haijafika bungeni. Je, kama JAMBO LEO wako sahihi je, kwa nini uongozi wa bunge usichukuliwe hatua na bunge kwa si kwa kuitoa tu, bali kuiacha hadi iozee ofisini kwa spika? J,e huko kuozea kwa Spika ni kwa sababu bunge limechambuliwa kama karanga?


Hivyo, kutokana na mkanganyiko huo, Mnyika alitaka kuungwa mkono hoja ili bunge liweke deadline kuwa tipoti hiyo ifike siku fulani itakayotajwa kuliko kuwa na ambiguity kama inayojitokeza.

Anne Makinda aliinuka na kusema kwamba hoja hiyo haikubali kwa sababu Bunge halifanyi kazi na magazeti ambayo mara nyingi huandika habari za uongo.

MY TAKE:

Jibu hili la Spika, limenipa nguvu ya kuandika headline kwamba CCM yaliumbua JAMBO LEO. Ingekuwa umbuko hilo limetolewa na upinzani JAMBO LEO lisingejali sana, lakini kwa sababu limetolewa na kuumbuliwa na mwana-CCM yaani Anne Makinda na wengine weng mle walioko upande wa kulia wakashangilia basi alhamdulilah.
 
Najiuliza: hivi kwanini Mnyika alileta hoja hii kwa kutumia gazeti la JAMBO LEO kama source yake? Je ndiyo gazeti analoliamini? na inakuwaje hoja ianzishwe kwa kutegemea taarifa iliyoandikwa kwenye gazeti?
 
Najiuliza: hivi kwanini mnyika alileta hoja hii kwa kutumia gazeti la JAMBO LEO kama source yake? Je ndiyo gazeti analoliamini? na inakuwaje hoja ianzishwe kwa kutegemea taarifa iliyoandikwa kwenye gazeti?

Kama humuelewi Mnyika basi hii ilikuwa ni trick kubwa. Mimi naamini alijua itakataliwa. Lakini JAMBO LEO ni gzeti la CCM linaloongoza kuponda CHADEMA na linashabikiwa na kila mwana-CCM.

Hapa tayari karata tosha kwamba gazeti hili ni waongo wakubwa na wazushi na limethibitishwa na wao wenyewe CCM na hansard siku zote itaonyesha kwamba gazeti hili ni la uongo na hivyo lisiaminike tena habari zake.

Big up Mnyika, amewaumbua vya kutosha.
 
Ahahhahahahhaaaaaa!!

Kwa hiyo ndo kusema Bunge halitambua uwepo wa vyombo vya mawasiliano katika jamii na je kama bunge linavitambua kuwa vipo ni kwa nini lisijue kuwa vina timiza majukumu fulani kwa jamii. Je kama gazeti hilo hilo lingeandika Anne Makinda ahongwa ili aikalie ripoti ya Jairo na taarifa kemkem zikashushwa ingekuwa vipi hapo au Makinda angetoa jibu hilo hilo?????

Kwa hiyo you-tube ni chombo cha polisi ndio maana wanafanyia kazi taarifa zake au kuna tofauti gani kati ya taarifa iliyoko kwenye gazeti na iliyoko you tube.

........................................................................................................................................................................

Anne Makinda aliinuka na kusema kwamba hoja hiyo haikubali kwa sababu Bunge halifanyi kazi na magazeti ambayo mara nyingi huandika habari za uongo.
 
Najiuliza: hivi kwanini mnyika alileta hoja hii kwa kutumia gazeti la JAMBO LEO kama source yake? Je ndiyo gazeti analoliamini? na inakuwaje hoja ianzishwe kwa kutegemea taarifa iliyoandikwa kwenye gazeti?

Hoja kubwa nayoiona mimi ni kuliwajibisha JAMBO LEO kwa kuandika habari ya uwongo na uchochezi! Kama spika amekanusha kuwepo ripoti mezani kwake, haoni ni jambo la msingi kuliwajibisha gazeti hilo na ikiwezekana kulifungia kabisa!!
 
No No hapo ni Mnyika amumbua Anne Makinda....maana yeye hajajibu swali la Mnyika badala yake kali-divert kwa magazeti, ni kweli source ya taarifa ni gazeti lakini Spika alitakiwa kutoa ufafanuzi wa hali ilivyo kwa sasa pengine hata kurudia tu maneno ya Pinda kuwa itafika wakati wowote na sio kutoa such a simple conclusion. Kumbuka waswahili husema WASWAHILI HUSEMA HIVI " M'MBEA HASEMI UONGO, JAPO HAJATUMWA' kwahio kwa sisi watu wazima tunahitimisha kuwa JAMBO LEO KASEMA UKWELI JAPO HAJATUMWA.....arguement ya ukweli wa hoja inabaki pale pale, asikwepe swali
 
Hoja kubwa nayoiona mimi ni kuliwajibisha JAMBO LEO kwa kuandika habari ya uwongo na uchochezi! Kama spika amekanusha kuwepo ripoti mezani kwake, haoni ni jambo la msingi kuliwajibisha gazeti hilo na ikiwezekana kulifungia kabisa!!
Huenda kuna kitu mnyika anakifahamu hata kabla ya habari hii kuandikwa ndani ya JAMBO LEO.Kama spika ataamua kukaa kimya bila kuwajibisha wahusika wa gazeti hili, then kutakuwa na ukweli ndani yake.
 
Je itakapobainika kuwa muongo ni Spika na sio gazeti itakuaje? Simaanishi kuwa iundwe tume
Hoja kubwa nayoiona mimi ni kuliwajibisha JAMBO LEO kwa kuandika habari ya uwongo na uchochezi! Kama spika amekanusha kuwepo ripoti mezani kwake, haoni ni jambo la msingi kuliwajibisha gazeti hilo na ikiwezekana kulifungia kabisa!!
 
Mbunge wangu Mnyika leo kaniangusha sana kwa kuomba mwongozo wa spika na kuleta gazeti la Jambo Leo kuwa wanasema ripoti ya Jairo iliishatoka na kuletwa kwa spika na kwamba ripoti imelichambua bunge kama karanga. Na spuka eti kakalia ripoti hiyo na Waziri Mkuu halusema ukweli kuwa ripoti bado. Akarudia mara nne kuhusu kuchambuliwa kama karanga kwa bunge! Sikuamini macho yangu na masikio kwamba mbunge makini kama Mnyika anakuja na copy ya gazeti la Jambo Leo kama ushahidi mkuu ndani ya bunge! Lets get serious, man. Anapoteza muda wetu kusikiliza upuuzi huu! Pia amezidisha kuomba miongozo utadhani only him knows it all!
 
Hoja kubwa nayoiona mimi ni kuliwajibisha JAMBO LEO kwa kuandika habari ya uwongo na uchochezi! Kama spika amekanusha kuwepo ripoti mezani kwake, haoni ni jambo la msingi kuliwajibisha gazeti hilo na ikiwezekana kulifungia kabisa!!

Umenipa wazo na mimi. Ni kweli JAMBO LEO linatakiwa lifungiwe kama MWANAHALISI kwa uzushi uliothibitishwa na Spika.
 
Je itakapobainika kuwa muongo ni Spika na sio gazeti itakuaje? Simaanishi kuwa iundwe tume

Huyo wa kubainisha kuwa spika ni muongo ndiyo sijamuona; unamaanisha awatie kikaangoni Pinda na Makinda, siyo Bongo!
 
Je itakapobainika kuwa muongo ni Spika na sio gazeti itakuaje? Simaanishi kuwa iundwe tume

ripoti ya awali iliwasilishwa na spika akaikataa kwa kutojitosheleza na kuitaka serikali ije na majibu kamili. inawezekana jambo leo wanainukuu hiyo ripoti ya awali.
 
Najiuliza: hivi kwanini Mnyika alileta hoja hii kwa kutumia gazeti la JAMBO LEO kama source yake? Je ndiyo gazeti analoliamini? na inakuwaje hoja ianzishwe kwa kutegemea taarifa iliyoandikwa kwenye gazeti?
Gazeti Jambo Leo ni gazeti la CCM unalingine la kuuliza?
 
Huu ni wakati mzuri wa serikali kuonyesha haina upendeleo kwa vyombo vya habari. Spika Anne Makinda leo bungeni akijibu swali la mbunge John Mnyika amesema gazeti hilo limeandika habari za uongo kuhusu bunge kwamba yeye kama Spika amekalia report ya Jairo.

SPika amekanusha na kusema huo ni uongo. Kama ni uongo basi huu ni uchochezi maana gazeti kwa namna moja lilikuwa linamfanya waziri mkuu aonekane muongo bungeni aliposema kuwa ripoti haijafika bungeni.

Hivyo, sasa tutarajie gazeti hili lifungiwe ili serikali isijitumbukize katika dimbwi la kuonekana hailiogopi MWANAHALISI lakini inaliogopa JAMBO LEO
 
Huu ni wakati mzuri wa serikali kuonyesha haina upendeleo kwa vyombo vya habari. Spika Anne Makinda leo bungeni akijibu swali la mbunge John Mnyika amesema gazeti hilo limeandika habari za uongo kuhusu bunge kwamba yeye kama Spika amekalia report ya Jairo.

SPika amekanusha na kusema huo ni uongo. Kama ni uongo basi huu ni uchochezi maana gazeti kwa namna moja lilikuwa linamfanya waziri mkuu aonekane muongo bungeni aliposema kuwa ripoti haijafika bungeni.

Hivyo, sasa tutarajie gazeti hili lifungiwe ili serikali isijitumbukize katika dimbwi la kuonekana hailiogopi MWANAHALISI lakini inaliogopa JAMBO LEO
Hilo gazeti mkubwa ni la kwao CCM! Kumbuka ule usemi usemao ukijua kudanganya sana pia usiwe msahaulifu!
 
Wewe sio ,muumini wa demokrasia, yawezekana umeajiliwa kufanya kazi hii, utakuwa si tofauti na ombaomba, hufai...hufai..hufai..tafuta ajira ufanye sio kazi hii!...mbafu..
 
Hoja kubwa nayoiona mimi ni kuliwajibisha JAMBO LEO kwa kuandika habari ya uwongo na uchochezi! Kama spika amekanusha kuwepo ripoti mezani kwake, haoni ni jambo la msingi kuliwajibisha gazeti hilo na ikiwezekana kulifungia kabisa!!
hivi mbona mnapindisha mambo kimbumbumbu????
MAKINDA ameongelea MAGAZETI kwa ujumla wake bila ku-categorize ni gazeti lipi.. sasa mnapotaka kumlisha maneno na kupindisha kauli yake kwa kutoa tafsiri tofauti na alivyomaanisha ni kwa maslahi gani???? grow up dirty kids!!!!!
 
Najiuliza: hivi kwanini Mnyika alileta hoja hii kwa kutumia gazeti la JAMBO LEO kama source yake? Je ndiyo gazeti analoliamini? na inakuwaje hoja ianzishwe kwa kutegemea taarifa iliyoandikwa kwenye gazeti?

Maubero

Tafuta kitabu cha kanuni za bunge ujielimishe kadri ya uwezo wako. Kanuni za bunge zinamruhusu kufany alichofanya, kunukuu chombo cha habari.
 
Unajiangusha mwenyewe kwa kutokuelewa mantiki ya hoja yake.............!!
Lakini ni wapi J. Mnyika alisema huo ni ushahidi wake mkuu?? Je ni mara yako ya kwanza kuona habari za taarifa za gazeti zinajadiliwa bungeni??? Hata kujua tu kwamba gazeti lolote lile lipo kisheria kwa hiyo linatakiwa kuutumikia umma kwa kuwapa habari likikidhi matakwa ya kisheria haujui ndungu yangu?? ni kweli una haki ya kutokuamini macho na masikio yako kabisa kabisa tena nakushauri ikiwezekana uyan'goe na kuyakata yote.

Nikukumbushe kwamba hata mahakama inatambua uwepo wa vyombo hivi na huvitumia wakati mwingine kama rejea. Mch. Mtikila amewahi kushitakiwa kwa kusema Mwl. J.K. Nyerere alikufa kwa ukimwi, alipofikishwa mahakamani akamnukuu Rais mstaafu Benjamin W. Mkapa kwa kusoma kilichokuwa kimeandikwa kwenye gazeti la nipashe kama ujumbe wa Rais kwa umma kuhusu hali ya Mwl. na hapo ni mahakamani kwenye sheria sio bungeni tena.

Lakini hoja ya J. Mnyika ni zaidi ya kilichoandikwa na HABARI LEO sema tu ufinyu wa fikra ndo unawafanya wengi wakomee kwenye habari za kwenye magazeti bila kujitafakarisha kihoja na kimantiki juu ya swali la Mtanzania halisi J. Mnyika.

Duu! Nimejitahidi sana kukupa a, e, i, o, u.....n.k. kama sasa haujaelewa bado nakushauri uchukue nyundo ukitwange kichwa chako kipasuke tukakishone upya.

Mbunge wangu Mnyika leo kaniangusha sana kwa kuomba mwongozo wa spika na kuleta gazeti la Jambo Leo kuwa wanasema ripoti ya Jairo iliishatoka na kuletwa kwa spika na kwamba ripoti imelichambua bunge kama karanga. Na spuka eti kakalia ripoti hiyo na Waziri Mkuu halusema ukweli kuwa ripoti bado. Akarudia mara nne kuhusu kuchambuliwa kama karanga kwa bunge! Sikuamini macho yangu na masikio kwamba mbunge makini kama Mnyika anakuja na copy ya gazeti la Jambo Leo kama ushahidi mkuu ndani ya bunge! Lets get serious, man. Anapoteza muda wetu kusikiliza upuuzi huu! Pia amezidisha kuomba miongozo utadhani only him knows it all!
 
hivi mbona mnapindisha mambo kimbumbumbu????
MAKINDA ameongelea MAGAZETI kwa ujumla wake bila ku-categorize ni gazeti lipi.. sasa mnapotaka kumlisha maneno na kupindisha kauli yake kwa kutoa tafsiri tofauti na alivyomaanisha ni kwa maslahi gani???? grow up dirty kids!!!!!

Vipi, we ni Mhariri wa JAMBO LEO? Naona povu linakutoka! Kawaida yenu kupindisha maneno kama vilaza, habari ilikuwa quoted kwenye gazeti la JAMBO LEO, wewe unataka kusema Bi Mkubwa kwa kusema "Magazeti" kunaondosha ukweli wa kuwa alimaanisha JAMBO LEO! Mnyika hakuquote "MAGAZETI", aliquote "JAMBO LEO". Au ni kweli hiyo Ripoti anayo mezani?
 
Back
Top Bottom