X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,810
MOGADISHU
Wabunge nchini Somalia leo wamepiga kura kuidhinisha mapendekezo ya kuwepo kwa sheria za kiislam katika nchi hiyo ya pembe ya Afrika.
Wabunge hao wamesema kuwa wanamatumaini kupitishwa kwa mapendekezo hayo kutasaidia kupunguza mashambulizi kutoka kwa wanamgambo wa kiislam wenye imani kali dhidi ya serikali ya mpito ya nchi hiyo inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa, kwani hilo ni moja katika matakwa yao makuu.
Waziri wa Habari wa Somalia Farhan Ali Mohamed amesema kuwa wanazuoni na maimamu wataalikwa katika kuipitia upya katiba ya nchi hiyo na kutoa mapendekezo yao kuhusiana na vifungu wanavyoona kuwa viko kinyume na uislam.Mabadiliko hayo yanatakiwa kuidhinishwa na theluthi mbili ya wabunge hao.
Wabunge nchini Somalia leo wamepiga kura kuidhinisha mapendekezo ya kuwepo kwa sheria za kiislam katika nchi hiyo ya pembe ya Afrika.
Wabunge hao wamesema kuwa wanamatumaini kupitishwa kwa mapendekezo hayo kutasaidia kupunguza mashambulizi kutoka kwa wanamgambo wa kiislam wenye imani kali dhidi ya serikali ya mpito ya nchi hiyo inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa, kwani hilo ni moja katika matakwa yao makuu.
Waziri wa Habari wa Somalia Farhan Ali Mohamed amesema kuwa wanazuoni na maimamu wataalikwa katika kuipitia upya katiba ya nchi hiyo na kutoa mapendekezo yao kuhusiana na vifungu wanavyoona kuwa viko kinyume na uislam.Mabadiliko hayo yanatakiwa kuidhinishwa na theluthi mbili ya wabunge hao.