Rumishaeli
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 227
- 72
Wakuu wa JF kila wizara inapohitimisha bajeti yake bungeni, bunge hukaa kama kamati kupitisha bajeti ya wizara husika na wabunge huuliza maswali spesifiki kwa kila kipengele kwa wizara husika. Je nini kinachotoke pale waziri husika anapotoa majibu ambayo either ni general au hayajibu swali husika kutoka kwa mbunge. Maana mara nyingi nimeona yanapotokea hayo mwenyekiti huendelea kumwita mbunge mwingine kama vile waziri husika amejibu sawia. Wanajamii wenzangu nijuzeni maana majibu ya mawaziri wetu naona hayana mshiko kwa maswali hayo wakati wa bunge kukaa kama kamati.