Bunge limejaa wala rushwa

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
Rushwa inalitafuna Bunge, Spika amebaki mtazamaji
Thursday, 21 July 2011 21:12
Mwananchi

JANA tulichapisha habari zilizoonyesha jinsi tuhuma za rushwa zinazowakabili baadhi ya wabunge zinavyoendelea kulitikisa Bunge. Tuhuma hizo siyo tu zinaonekana kulitia doa Bunge letu tukufu, bali pia zinatishia kuzisambaratisha baadhi ya kamati za kudumu za chombo hicho cha kutunga sheria. Wahanga wa tuhuma hizo katika siku za hivi karibuni ni Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) inayoongozwa na Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema na ya Nishati na Madini iliyo chini ya Mbunge wa Bumbuli, Januari Makamba.

Mpaka sasa hakuna anayejua lini mzimu huo wa rushwa ulianza kuzitafuna baadhi ya kamati hizo za kudumu hadi kuzifikisha hapo zilipo. Itakumbukwa kuwa, kamati hizo zilipoundwa baada ya Bunge la Kumi kuanza kazi mwishoni mwa mwaka jana, kamati nyeti za Bunge zinazoshughulikia hesabu za Serikali Kuu, Serikali za Mitaa na Mashirika ya umma zilianza kazi kwa kishindo kiasi cha kuwakuna wananchi kwa jinsi zilivyokuwa zinafanya kazi kwa ufanisi.

Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa, kwa mfano, ilijizolea sifa kemkemu kwa jinsi ilivyoanza kazi yake kwa mwendo wa kasi na kupambana na ufisadi katika halmashauri ilizokuwa imezikagua. Sote ni mashahidi wa jinsi kamati hiyo ilivyowashukia watendaji katika halmashauri mbalimbali nchini, kiasi cha baadhi yao kukatwa asilimia fulani ya mishahara yao baada ya kushindwa kutoa maelezo ya kuridhisha kuhusu matumizi ya fedha za halmashauri zao.

Lakini kamati hiyo sasa inaelekea kusambaratika kutokana na tuhuma za rushwa zinazowakabili wajumbe wengi wa kamati hiyo, kiasi kwamba imeshindwa kukutana licha ya Mwenyekiti Mrema kuitisha vikao mara tatu kwa nyakati tofauti. Mrema mwenyewe amekiri kwamba kutokana na hali hiyo ya wajumbe wengi kutofika kwenye vikao, anakusudia kuwasilisha taarifa hiyo kwa Spika wa Bunge ili kupata mwongozo wa nini la kufanya.

Gazeti hili limeona taarifa rasmi za Bunge (Hansard) zinazothibitisha kuwa, Mrema aliitisha vikao hivyo. Kitendawili ambacho sasa kimefumbuliwa ni kwamba, baada ya mjumbe wa kamati hiyo, David Kafulila kuwatuhumu bungeni wajumbe wawili wa kamati hiyo kwa kuomba rushwa kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, mkoani Tanga wakati kamati hiyo ilipokuwa inakagua miradi mbalimbali, wajumbe wengi walipata mfadhaiko na kukacha vikao ambavyo ajenda yake kuu ilikuwa kujadili tuhuma hizo za rushwa ambazo tayari zilikuwa zimemfikia Mrema na Spika mwenyewe.

Lakini kumbe mfadhaiko ndani ya kamati hiyo uliongezeka maradufu baada ya baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo waliokwenda mkoani Pwani kukagua miradi ya halmashauri za mkoa huo, pia kudaiwa kuomba rushwa kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiserawe ili wasiuchukulie hatua baada ya kugundua madudu katika mahesabu ya baadhi ya miradi iliyokuwa imetengewa fedha. Hiyo ndiyo siri ya kuwapo mshikemshike na mfadhaiko katika kamati hiyo na hakika, hiyo ndiyo sababu kuu inayowatia hofu wajumbe wengi wa kamati hiyo kiasi cha kuogopa kuhudhuria vikao vya kamati hiyo.

Kwa mwenendo huo wa wajumbe wengi wa kamati hiyo, hatuna sababu ya kutoamini kwamba halmashauri nyingine zilizokaguliwa na kamati hiyo ziliombwa rushwa lakini zilikosa ujasiri wa kutoa taarifa kwa mamlaka husika, tofauti na walivyofanya wakurugenzi wa halmashauri za wilaya za Kiserawe na Handeni.

Tunapoangalia uozo uliomo ndani ya kamati hiyo na kutathmini kiwango cha uozo katika Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini na Bunge zima kwa jumla ambalo wiki iliyopita lilikumbwa na tuhuma za wabunge wake wengi kupokea rushwa ili lipitishe bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini, hakika tunafadhaika na kupata mashaka juu ya mustakabali wa nchi yetu.

Kinachotufadhaisha zaidi ni pale Spika wa Bunge anapokaa kimya pasipo kuamuru kufanyika kwa uchunguzi huru wa Kibunge ili hatua zichukuliwe kwa wabunge waliodai au kupokea rushwa.



 
Hawa hapa

Minister-for-East-Africa-Cooperation-Samuel-Sitta.jpg
Pinda+in+tears.jpg
Waziri+Ngeleja.jpg


Mfuko wa posho, wizi na uhujumu wa taifa


Mustafa+Mkulo.jpg


Kiongozi wa wizi na ofisi ya wizi Tanzania inaongozwa na Huyu kikwete


tanzania_president.jpg
 
Hawa hapa

Minister-for-East-Africa-Cooperation-Samuel-Sitta.jpg
Pinda+in+tears.jpg
Waziri+Ngeleja.jpg


Mfuko wa posho, wizi na uhujumu wa taifa


Mustafa+Mkulo.jpg


Kiongozi wa wizi na ofisi ya wizi Tanzania inaongozwa na Huyu kikwete


tanzania_president.jpg

Bado wengi wanakosekana hapo akiwamo Mkapa.
 
to be honest, intergrity ya wabunge wengi na hasa wa CCM ni questionable

bado sijapata jibu bajeti ya wizara ya afya imepitaje

hakiyamungu
 
  • Thanks
Reactions: BAK
to be honest, intergrity ya wabunge wengi na hasa wa CCM ni questionablebado sijapata jibu bajeti ya wizara ya afya imepitajehakiyamungu[/nQUOTE] KWANINI NILIZALIWA TZ?ISIWE HATA MALAWI?
 
to be honest, intergrity ya wabunge wengi na hasa wa CCM ni questionable

bado sijapata jibu bajeti ya wizara ya afya imepitaje

hakiyamungu

Mkuu inadaiwa wakati wa bajeti kila Wizara "hutenga" shilingi milioni 900 zinazowekwa kwenye vibahasha na kukabidhiwa Wabunge ili kuhakikisha bajeti za Wizara hizo zinapitishwa kilaini. Hili Bunge lewtu halostahili kuitwa tena Bunge Tukufu limekosa kabisa utukufu ambao tulidhani ulikuwepo katika kuwawakilisha Watanzania wa majimbo mbali mbali yaliyowachagua Wabunge hawa.

Cha ajabu hadi sasa si Makinda wala Pinda aliyetamka kwamba kuna haja ya uchunguzi wa kina ili kujua ni Wabunge gani wanahusika na uozo huu na ulianza rasmi lini? awamu ya pili, ya tatu au ya nne, siamini kabisa uozo kama huu ulikuwepo wakati wa Mwalimu.
 
BAK.... hivi ina maana hii kashfa inawagusa hadi wabunge wa upinzani?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Kusema Bunge peke yake ni Understatement..
Rushwa Bongo imeshakuwa kama oil kwenye engine...
Bila Rushwa kazi haziendi
 
CCM imeoza kwa kuwa wanaingia bungeni kwa nguvu polisi na hongo ya wazi ya kanga ,kofia ,chumvi nk hawawezi kuwa na la maana kwa Taifa na serikali ni yao na wako juu ya sheria wanaendelea tu hawana wasi wasi .
 
BAK.... hivi ina maana hii kashfa inawagusa hadi wabunge wa upinzani?

Hili ndilo halifahamiki Mkuu, labda siku za usoni tutafahamu wahusika wote wa kashfa hii, na kwa maoni yangu Wabunge wote wapokeaji wa rushwa wanastahili kufukuzwa bungeni na kupandishwa kizimbani haraka sana bila kujali wanatoka chama kipi.
 
Back
Top Bottom