BUNGE limechagua kiingereza...

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Kila aliyenyooosha kiingereza kwenye uchaguzi wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki jana alichaguliwa.Wabunge wakiongozwa na Spika walihama kwenye hoja na kuhamia kwenye kiingereza.Imedhihirika jana.Waliojikwaa kwenye lugha hii,wamejikwaa pia kwenye kura. Wamedhalilishwa.Ni kweli kigezo pekee ni kujua kiingereza? Wangapi walikuwa Bunge hilo wakijua kiingereza lakini hawakufanya chochote?

Ni muda wa kubadilika.Ni muda wa kusema hata Kiswahili chapaswa kutumiwa. Tukisimamie Kiswahili chetu popote.Tutaeleweka na kutetea maslahi yetu vyema.Kiingereza si lugha yetu jamani..

Mzee Tupatupa
 
Kilengesa ni hataree arifu ugonjwa wa taifa huu bora hata interview makazini ziwe za kiswahili.
 
Tupende tusipende kwa Tanzania Kiingereza kinaleta hadhi. Ukiongea Kiingereza kizuri basi utaonekana wewe ni "kichwa", utaonekana umesoma na kustaarabika, n.k.

Na ukiongea Kiingereza kibaya basi utaonekana hamnazo, hujasoma, hujastaarabika, na mambo mengine kama hayo.

Si sahihi kabisa ila hivyo ni ndivyo ilivyo.
 
Kila aliyenyooosha kiingereza kwenye uchaguzi wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki jana alichaguliwa.Wabunge wakiongozwa na Spika walihama kwenye hoja na kuhamia kwenye kiingereza.Imedhihirika jana.Waliojikwaa kwenye lugha hii,wamejikwaa pia kwenye kura. Wamedhalilishwa.Ni kweli kigezo pekee ni kujua kiingereza? Wangapi walikuwa Bunge hilo wakijua kiingereza lakini hawakufanya chochote?

Ni muda wa kubadilika.Ni muda wa kusema hata Kiswahili chapaswa kutumiwa. Tukisimamie Kiswahili chetu popote.Tutaeleweka na kutetea maslahi yetu vyema.Kiingereza si lugha yetu jamani..

Ni kweli tunapaswa kukipenda Kiswahili lakini tuna vikwazo vingi.Uchumi wetu bado mchanga,tunategemea bidhaa nyingi kutoka nje sababu viwanda vyetu vilishauzwa/kubinafsishwa siku nyingi.Mfano Mdogo simu/kompyuta uliyoitumia kuwafikishia watu hii habari maelekezo yake yapo kwa kiswahili?isitoshe Bunge la EA haliendeshwi kwa Kiswahili ktk jambo lolote.Mikataba inayoingiwa na viongozi wetu Wa kiserikali imeandaliwa kwa kiingereza sbb ya utegemezi(wawekezaji)tunaoutaka kutoka nje.Kiswahili tunakipenda lakini asilimia kubwa ya wananchi Wa Tanzania hawajui kuzungumza Kiswahili fasaha.
 
Mimi niliskia Kiswahili ndio lugha ya EA sasa hii habari ya kuwapima kwenye ki English ilitoka wapi?
 
Umesema kweli. Nguvi wa thiongo aliwahi kusema, "Si vizuri lugha moja ikakua katika kaburi la lugha nyingine," kwani lugha inapokufa kila kitu katika lugha ile kinakufa. Yaani namna ya kufikiri, ugunduzi, falsafa, mtazamo nk. Hapa kwetu Kiingereza kinataka kukua katika kaburi la Kiswahili. Kimsingi tunapoteza fedha na mda kujifunza Kiingereza. Nimewahi kufanya utafiti nikagundua kwamba tunahitaji 1% ya uwekezaji kama taifa katika lugha ya Kiingereza. Yaani kwa ajili ya watu watakaofanya kazi ya mipakani, uhamiaji, viwanja vya ndege na wageni wa ikulu. Mashuleni tufundishe Kiswahili kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu. Hii itasaidia sana kutengeneza utamaduni wetu pia tutakuwa na siri za taifa na namna ya kuwasiliana kama watu wa familia moja.
 
Mimi niliskia Kiswahili ndio lugha ya EA sasa hii habari ya kuwapima kwenye ki English ilitoka wapi?
Kiingereza ndio lugha rasmi ya Jumuiya. Kinachonishangaza ni kuwa kwa nini wawakilishi watu hadi leo hawajapambana kuhakikisha kuwa Kiswahili ndiyo inakuwa lugha rasmi ya jumuiya.
 
Mi nilifikiri kwamba kwa vile watz wengi tunaongea Kiswahili na wakati mwingine lugha za makabila.Nilijua kwamba wagombea wote watawapeleka kozi ya kuongea Kiingereza kwanza halafu waombe kura kwenye bunge baada ya kufuzu Inglishi kozi.Ningekuwa mimi ningeomba mwongozo kwa spika ili niongee kiswahili.
 
Back
Top Bottom