Bunge Lijadili Hoja ya Dharura kuhusu Mgomo wa Madaktari

Kitila Mkumbo

JF-Expert Member
Feb 25, 2006
3,354
1,943
Nchi yetu ipo katika hali ya dharura kutokana na kutaabika kwa wagonjwa mahospitalini bila msaada kufuatia mgomo unaoendelea wa madaktari.

Itakuwa ni aibu kwa Bunge kuanza kikao chake leo kama vile mambo ni kama kawaida. Hata wabunge wenye hoja binafsi wangeziweka pembeni kwanza ili mojawao aombe kuwasilisha hoja ya dharura kuhusu hili la mgomo kama alivyofanya Wenje kuhusu umeme Mwanza katika kikao kilichopita. Tayari tunaonekana kituko, hili la mgomo wa madaktari litafanya baadhi ya binadamu wenzetu katika nchi zingine waanze kushuku ubinadamu wetu! Na huu utamaduni wa kuamini kwamba ubabe wa fukuzafukuza ni suluhisho la migogoro linazidi kutudhoofisha kifikra na kutufanya tuonekane ndondocha.

Na wabunge wanapojadili hili la mgomo, kama kweli watajadili, watambue kwamba kitendo chao cha kushinikiza na hatimaye kuidhinishiwa posho zisizo na tija, kimehalalisha na kuimarisha zaidi madai ya madaktari. Ujumbe wa posho za wabunge ni mmoja tu, nao ni kwamba kumbe serikali yetu ina uwezo wa kutekeleza madai yote ya madaktari. Kumbe basi tatizo sio uwezo, bali nia na mgomo ni njia mwafaka zaidi katika kushinikiza watawala kubadili nia.

Lakini je kuna mtu anasikiliza, na wakisikia wanajali?
 
Big up Kaka yangu Kitila Mkumbo! Kikao kinaanza saa tatu asubuhi hii...Mhe. Dr. Kigwangala, Mhe. Mnyika...pick it up!
 
Umesikika mkuu, nakuamini kwa ushauri. Nadhani mwenye akili atagundua ushauri wa busara na aufuate.
Lakini naini wa kusikiliza?

Mwenyewe yuko bize na Wizara ya Mambo ya Nje.
 
Wasiwasi wangu ni hata kama itatolewa hoja ya dharura kuhusu mgomo wa madaktari, ni waziri gani atakayetoa majibu ya kuaminika na yenye kuleta suluhu ya matatizo yaliyopo? Nani mwenye busara za kutatua mgogoro uliopo na wakati huu ambapo hata waziri mkuu ameshakuwa mtu wa jazba badala ya hoja?

Kwa mfano ikitokea mbunge akatoa hoja ya kutaka serikali ikashughulike na kutatua tatizo la madaktari kwanza na kusitisha shughuli za bunge, wabunge wako tayari kwa hilo au watajali posho?
 
Nimeona asbh wanajadili mkonge na pango, watashtuka kweli hawa jamaa wanotibiwa Apollo? Okey lets wait and see but I guess Dodoma inaweza kuwa biznes as usual.....
 
Kwa kuwa PM ameshatoa msimamo wake/maamuzi yake suala hili ni very likely likajadiliwa kiushabiki.....itakuwa vigumu kwa wabunge wa CCM "kumuangusha" waziri mkuu!

Hata hivyo sio wazo baya....wabunge wanaweza kujaribu......lakini linaweza kwenda vizuri zaidi bungeni kama hoja hiyo ya dharura italetwa na mbunge wa CCM.
 
Nimeona asbh wanajadili mkonge na pango, watashtuka kweli hawa jamaa wanotibiwa Apollo? Okey lets wait and see but I guess Dodoma inaweza kuwa biznes as usual.....

Hiyo imenipita, nani waliokuwa wanajadili?
 
Mkuu Kitila.Tuko pamoja.Umenena vema wabunge wetu wasikie kilio cha watanzania.Nadhani Tundu Lissu,Mnyika,Lema,Zitto na kiongozi wao Mbowe wamesikia
 
Umenene Dr..nategemea uzalendo na utaifa kwanza kwa hawa wawakilishi wetu,japo kwangu wamekwisha poteza mvuto muda mrefu.
 
Bunge linaendelea naona watu wanaendelea na maswali na majibu tu,sioni kama kuna dalili ya kuleta hoja kujadili jambo la dharura.lakini to be honest hili ni wazo zuri sana maana kwa taarifa nilizo nazo hali si nzuri huko mahospitalini tayari watu wanaendelea kupoteza maisha kila muda unavyokwenda.jamani hata wabunge wa CDM hamtaliona hili kama ni jambo la muhimu sana?
 
Umesikika mkuu, nakuamini kwa ushauri. Nadhani mwenye akili atagundua ushauri wa busara na aufuate.
Lakini naini wa kusikiliza?

Mwenyewe yuko bize na Wizara ya Mambo ya Nje.
Mkuu, umenikumbusha jamaa yangu mmoja aliniambia kwamba waziri husika wa mambo ya nje hana kazi sasa hivi. kazi yake ni kufanya appointments na bookings za mkulu.

So, sad.
 
Kaka Kitila, Hoja yako ni ya msingi saana, hata mimi nilitarajia hasa vyama vya upinzani kulisimamia hili, maana ni kete nzuri saana kisiasa. Lakini nashangaa SI CHADEMA WALA TLP waliotamka neno in a very STRONG TERMS. Heri yao NCCR waliojitamkia on behalf of serikali kwa kuwaomba Madaktari kurudi kwanza kazini then madai yao ndio yajadiliwe. Hata hivyo kaka mkumbo nakutumia message binafsi uisome tafadhari!!!
 
Wazo zuri sana.Wabunge wa Chadema ambao ndio watetezi pekee wa watanzania wafanyie kazi hili swala
 
Nchi yetu ipo katika hali ya dharura kutokana na kutaabika kwa wagonjwa mahospitalini bila msaada kufuatia mgomo unaoendelea wa madaktari.


Lakini je kuna mtu anasikiliza, na wakisikia wanajali?
Dr, honestly, labda kama serikali itakuwa imegundua kwamba imechemka in the first place. Approach yake kwenye hili swala through katibu mkuu wa wizara husika and later PM Pinda was wrong in all aspects.

Otherwise, majibu ya serikali yanatolewa na waziri mkuu ambae ndiye aliyechemka zaidi, sasa tutatarajia majibu tofauti? Tukizingatia kwamba tayari Wabunge wa CCM wameshafanya kikao na kuonyesha kuchukizwa na mwenzao Kigwangala kwa ushiriki wake katika mgomo (I don't believe kwamba ameshiriki katika kiwango cha kuwashawishi madaktari anyway)
 
Nchi yetu ipo katika hali ya dharura kutokana na kutaabika kwa wagonjwa mahospitalini bila msaada kufuatia mgomo unaoendelea wa madaktari.

Itakuwa ni aibu kwa Bunge kuanza kikao chake leo kama vile mambo ni kama kawaida. Hata wabunge wenye hoja binafsi wangeziweka pembeni kwanza ili mojawao aombe kuwasilisha hoja ya dharura kuhusu hili la mgomo kama alivyofanya Wenje kuhusu umeme Mwanza katika kikao kilichopita. Tayari tunaonekana kituko, hili la mgomo wa madaktari litafanya baadhi ya binadamu wenzetu katika nchi zingine waanze kushuku ubinadamu wetu! Na huu utamaduni wa kuamini kwamba ubabe wa fukuzafukuza ni suluhisho la migogoro linazidi kutudhoofisha kifikra na kutufanya tuonekane ndondocha.

Na wabunge wanapojadili hili la mgomo, kama kweli watajadili, watambue kwamba kitendo chao cha kushinikiza na hatimaye kuidhinishiwa posho zisizo na tija, kimehalalisha na kuimarisha zaidi madai ya madaktari. Ujumbe wa posho za wabunge ni mmoja tu, nao ni kwamba kumbe serikali yetu ina uwezo wa kutekeleza madai yote ya madaktari. Kumbe basi tatizo sio uwezo, bali nia na mgomo ni njia mwafaka zaidi katika kushinikiza watawala kubadili nia.

Lakini je kuna mtu anasikiliza, na wakisikia wanajali?
Kweli Dr...this needs to be done ASAP......inauma sana....wish i had power in this country(bahati mbaya mi si mwanasiasa na wala sipendi siasa)....ningewaswaga hawa washenzi mithili ya Sokoine(na labda labda zaidi yake)....nchi gani hii inayoongozwa na manyang'au na mafisi!!.....TZ ni nchi tajiri sana na haikutakiwa iwe hapa ilipo....lakini tunaongozwa na manyang'au hawa......raia wa Tanzania ni wapole sana...they don't deceive this....hata dunia inalijua hili......only time will tell......
 
Nadhani ni kipimo kwa Wabunge wote leo. Ingawa nasikia Wabunge wa CCM wamekaa kama kamati ya chama na kuwatisha na hata kutaka kuwafukuza wengine uanachama, sasa hiyo ndiyo kawaida ya janja ya serikali na ccm, lakini kwa hili hawana ujanja, Suala hili la madaktari ni tete.
 
Nchi yetu ipo katika hali ya dharura kutokana na kutaabika kwa wagonjwa mahospitalini bila msaada kufuatia mgomo unaoendelea wa madaktari.

Itakuwa ni aibu kwa Bunge kuanza kikao chake leo kama vile mambo ni kama kawaida. Hata wabunge wenye hoja binafsi wangeziweka pembeni kwanza ili mojawao aombe kuwasilisha hoja ya dharura kuhusu hili la mgomo kama alivyofanya Wenje kuhusu umeme Mwanza katika kikao kilichopita. Tayari tunaonekana kituko, hili la mgomo wa madaktari litafanya baadhi ya binadamu wenzetu katika nchi zingine waanze kushuku ubinadamu wetu! Na huu utamaduni wa kuamini kwamba ubabe wa fukuzafukuza ni suluhisho la migogoro linazidi kutudhoofisha kifikra na kutufanya tuonekane ndondocha.

Na wabunge wanapojadili hili la mgomo, kama kweli watajadili, watambue kwamba kitendo chao cha kushinikiza na hatimaye kuidhinishiwa posho zisizo na tija, kimehalalisha na kuimarisha zaidi madai ya madaktari. Ujumbe wa posho za wabunge ni mmoja tu, nao ni kwamba kumbe serikali yetu ina uwezo wa kutekeleza madai yote ya madaktari. Kumbe basi tatizo sio uwezo, bali nia na mgomo ni njia mwafaka zaidi katika kushinikiza watawala kubadili nia.

Lakini je kuna mtu anasikiliza, na wakisikia wanajali?

Dr kinachouna zaidi ni pale matatizo yanatokea mwenye nchi yuko huko kwenye vikao na mikutano ambayo siku zote amehudhuria na hakuna positive changes kwa taifa. Watu wanakufa, Pinda anasema hakuna pesa kwa madaktari at the same time anawaambia wabunge Rais kapitisha posho nao wanashangilia ujinga wakati watu wanakufa kwa kukosa tiba. Viongozi wamelewa madaraka na kusahau mambo ya muhimu kwa nchi. Ila nadhani Mungu anataka kuwaonesha kitu watanzania. Maana hata biblia inasema ukiona mambo yote hayo ujue mwisho umekaribia, ole wao watakaokata tamaa. Naamini mwisho wa ccm umefika
 
Nchi yetu ipo katika hali ya dharura kutokana na kutaabika kwa wagonjwa mahospitalini bila msaada kufuatia mgomo unaoendelea wa madaktari.

Itakuwa ni aibu kwa Bunge kuanza kikao chake leo kama vile mambo ni kama kawaida. Hata wabunge wenye hoja binafsi wangeziweka pembeni kwanza ili mojawao aombe kuwasilisha hoja ya dharura kuhusu hili la mgomo kama alivyofanya Wenje kuhusu umeme Mwanza katika kikao kilichopita. Tayari tunaonekana kituko, hili la mgomo wa madaktari litafanya baadhi ya binadamu wenzetu katika nchi zingine waanze kushuku ubinadamu wetu! Na huu utamaduni wa kuamini kwamba ubabe wa fukuzafukuza ni suluhisho la migogoro linazidi kutudhoofisha kifikra na kutufanya tuonekane ndondocha.

Na wabunge wanapojadili hili la mgomo, kama kweli watajadili, watambue kwamba kitendo chao cha kushinikiza na hatimaye kuidhinishiwa posho zisizo na tija, kimehalalisha na kuimarisha zaidi madai ya madaktari. Ujumbe wa posho za wabunge ni mmoja tu, nao ni kwamba kumbe serikali yetu ina uwezo wa kutekeleza madai yote ya madaktari. Kumbe basi tatizo sio uwezo, bali nia na mgomo ni njia mwafaka zaidi katika kushinikiza watawala kubadili nia.

Lakini je kuna mtu anasikiliza, na wakisikia wanajali?
Ndugu yangu DR. Kitila, wabunge wa CCM hawapo tayari kwa hilo. Kama umesoma gazeti la Mwananchi la tarehe 31/1/2012 utaona walivyomuweka kiti moto mbunge mwenzo Dr Kigwangala kwa kosa la kuwaunga mkono madaktari wanaogoma. Kwenye kamati yao ya wabunge wa CCM walimpongeza sana mh.sana mtoto wa mkulima wa sumbawanga kwa wa ganga wa jadi kwa hatua nzuri alizochukua dhidi ya 'madaktari watukutu' wanaogoma !
 
Back
Top Bottom