Watanzania
JF-Expert Member
- Jul 7, 2009
- 727
- 42
Vifungu viwili vya bajeti ya wizara ya sheria na mambo ya katiba vimepangiwa shilingi milioni 900 kila kimoja kwa ajili ya mahakama ya kadhi. Wakipitia kifungu kwa kifungu, bunge wa la muungano wa Tanzania lipitisha vifungu hivyo vya bajeti vilivyoandaliwa na serikali ya CCM. Je serikali ya CCM sasa imekuwa ya kidini? Kama siyo ya kidini kwa nini iwe kwa dini moja tu wakati uanzishwaji wa mahakama za kimila za wamasai, wasukuma, wakatoliki, walutheri haukupata fungu la serikali?
Je sasa CCM ndio imedhamiria kumomonyoa misingi ya umoja wa kitaifa kwa kuleta udini? Je chama hiki kinastahili ridhaa ya watanzania tena? Kwangu mimi hapana na kodi yangu imetumika bila ridhaa yangu na imevunja katiba ya nchi kwa kuleta udini.
Je sasa CCM ndio imedhamiria kumomonyoa misingi ya umoja wa kitaifa kwa kuleta udini? Je chama hiki kinastahili ridhaa ya watanzania tena? Kwangu mimi hapana na kodi yangu imetumika bila ridhaa yangu na imevunja katiba ya nchi kwa kuleta udini.