Bunge labuni njia mpya ya kujilipisha posho kwa kufanya vikao vya ziada

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
Spika Wa Bunge Akutana Na Ujumbe Wa Timu Ya Kujitathimini Katika Maswala Ya Utawara Bora Barani Afrika


3.jpg
6.jpg
5.jpg
7.jpg
4.jpg
1.jpg

Wajumbe wa timu ya kujitathimini katika maswala ya Utawara Bora barani Afrika (Africa Peer Review Mechanism –APRM)
wakiwa katika kikao cha pamoja na Spika wa Bunge na wenyeviti wa kamati za kudumu za Bunge
mara baada ya kukutana nao Ofisi za Bunge Dar es salaam.

Zile posho zilizokataliwa zimerudi kwa mlango mwingine, kwani wamebuni utaratibu wa vikao vya nje ya vikao vya kawaida vya bunge ili kujilipisha posho. Vikao vya wabunge vimeshamiri, na hata hawana muda wa kushughulikia mambo ya majimboni mwao. Misafara isiyoisha ya kutalii nje ya nchi kwa visingizio vya ukaguzi wa mashirika ya umma na majifunzo, utalii ni kama hata majukumu ya kushiriki vikao Dodoma hakuna umuhimu vile. Balozi zetu za nje zimenyang'anywa majukumu, sasa kazi hizo zinafanywa na wabunge wa bunge letu.

Hii tathmini ya utawala bora nini zaidi ya semina elekezi zilizofanywa na serikali ya Rais wetu Kikwete, matokeo yake ndio sawa na kutilia kibatari mafuta ya taa ili utambi uungue vizuri. Ninachoona mimi ni kuendelea kutumia pesa za walipa kodi bila manufaa na badala yake ujumbe wa watu wawili au watatu ungetosha na kisha kwenda kutoa lecture kwa wabunge wote.

Katika picha vikao vya kujitathmini vilipaswa kufanyika wakati wa vikao vya kawaida huko Dodoma, lakini vimepangiwa muda nje ya vikao vya kawaida ili kujenga mazingira ya kujilipisha posho. Kwa hali hii ni sawa na sikio la kufa kutosikia dawa. Wajumbe wote hao ilikuwa lazima wahudhurie au watatu au wawili wangetosha kupata ujumbe wa kuwafikishia wabunge wengine mjengoni?
 
Hili linchi ni kama lina laana. Sijui nani ametuloga. Hakuna hata wa kutuhurumia kwa hali tuliyo nayo kila mtu anajitahidi kula kwa nafasi aliyonayo. Tumekuwa kama mafisi.
 
Mkuu mbona naona heading haina direct link na thread? Labda kama sijaelewa.
Nilichokiona kwenye thread nadhani ni mambo ya muda mfupi, ukilinganisha na vikao vya bunge ambavyo vikianza vinakaa consecutively for certain period!
Anyway, it seems ni kama game linatafutiwa tactics za ushindi, ukizingatia bunge letu linaongozwa na vilaza wa ccm, siku zote wanawaza posho tu
 
Mkuu mbona naona heading haina direct link na thread? Labda kama sijaelewa.
Nilichokiona kwenye thread nadhani ni mambo ya muda mfupi, ukilinganisha na vikao vya bunge ambavyo vikianza vinakaa consecutively for certain period!
Anyway, it seems ni kama game linatafutiwa tactics za ushindi, ukizingatia bunge letu linaongozwa na vilaza wa ccm, siku zote wanawaza posho tu


Kwanza ilikuwa muhimu kamati zote za bunge wenye viti na makamu wote wahudhurie kikao hiki wakati ambapo wachache kama wawili au watatu wangehudhuria na kisha katika kikao kijacho kufikicha ujumbe kwa wabunge wengine ili kuokoa matumizi makubwa ya pesa na muda kwa baadhi ya wabunge kuwajibika majimboni mwao.

Kichwa cha habari maudhui yake nikile ambacho vikao vya kamati za bunge visivyoisha ambavyo ni endelevu, maana watokapo bungeni walio kwenye kamati wanaendelea na vikao na misfara bila kikomo hadi kukutanisha na vikao vinavyofuata. Kwa utaratibu huu wabunge wasio bahatika kuwa katika kamati za bunge hawatakoma kuomba kuongezewa posho kwa vile mapato yanatofautiana na walio kwenye kamati. Misafara ya wabunge nao kama kawa, ninavyoongea huenda kuna kamati za bunge ziko kutalii nchi za nje kwa kisingizio cha kukagua mashirika ya umma au kujifunza kutoka kwa wabunge wengine na wakirudi ni kudai ongezeko la posho za kupumzisha makalio kwa kasi mpya.
 
Hili linchi ni kama lina laana. Sijui nani ametuloga. Hakuna hata wa kutuhurumia kwa hali tuliyo nayo kila mtu anajitahidi kula kwa nafasi aliyonayo. Tumekuwa kama mafisi.

Yaani vituko haviishi kana kwamba wanashindana kula kama wako kwenye mbio za maratoni.
 
Yaani vituko haviishi kana kwamba wanashindana kula kama wako kwenye mbio za maratoni.

TANZANIA IMELAANIWA TANGIA TULIPOVUNJA UHUSIANO WA KIBALOZI NA ISRAEL NA KUANZA KUWACHUKIA BILA YA KOSA. Nitambariki yeyote atakaye kubaliki na kumtukuza yeyote atakaye kutukuza. Ona Kenya ilivyobarikiwa kiuchumi halafu ona sisi tulivyolaaniwa kiuchumi. ona kenya sasa inatutawala kiuchumi kama vile hatujawahi kupata uhuru wakati sisi tunawika kenya kwa kuuza mitumba tuu.

Leo hii wabunge wa kitanzania wamegeuka kuwa hatari sana kupita hata askari wa Al Shabab pale somalia. Mateso wanayoyapata wasomali kupitia uhuni wa Al Shabab na sisi tupatayo kupitia wabunge kujilimbikizi kila mapesa ya walala hoi, hayana tofauti kabisaa. Jamani wabunge wetu, wasaidieni watu walio athilika na siasa za ujamaa na kujitegemea kwanza halafu baadaye mje mjijue matumbo yenu.

watu ajulikanao kama wakulima ndio walioathilika sana na siasa za kuongopeana za ujamaa na kujitegemea. walikuwa wnakamtwa mjini halafu wanwekwa keko na baadaye hutupwa vijijini wkaishi kwa jina wakuloima huku ardhi ya kulimia hawana na wakiwa nayo haijai mkekani. mjini wanitwa wzurulaji halafu kijijini wanaitwa wakulima. sasa hawa wtu wanaihitaji msaada mkubwa sana ili waweze kuibuka katika bahari ya dhiki walilelewa na siasa za ujanja ujanja za ujamaa na kujitegemea. wabunge you need to grow up sometime!
 
Mimi nashindwa kuelewa, hivi INAKUWAJE MTU KULIPWA POSHO WAKATI ANATEKELEZA MOJA YA MAJUKUMU YAKE? Huu ni wizi na haupaswi kufumbiwa macho!
 
Siasa za Tanzania za kuganga njaa tu,tena kwenye mambo ya kutunyonya wananchi wote wanakuwa wamoja wala hamna upinzani tena!Haya bana hata msipolipwa hapa duniani lakini mjue mtalijibu kesho kwa mungu!Mfumo wa siasa wa Tz unamnyonya sana mlalahoi na ndiyo kikwazo kikubwa kwa ustawi wa Taifa letu!!Mungu yupo atatulipia tu!!
 
Back
Top Bottom