KUNA wanaodhani eti kuna kasoro na udhaifu mkubwa bungeni hivi leo. Siamini hivyo. Hili ninadhani linatokana na yale mazoea ya kuwa na bunge ambalo lilikuwa legelege na linalolala na kuuunga mkono hata kile wasichokijua wala wasichokielewa.Bunge hili lina vijana angavu wasiotaabika na maumivu ya uzee na kamba za kichama katika kujadili yalel ya msingi yatakalosaidia bunge la kesho na keshokutwa kuwa safi na lililoelimika na kutaalamika zaidi ili kuanza kushughulikia mambo ya kitaifa katika upana na kina zaidi demokrasia na haki za binadamu katika maendeleo yake na hususan kupata mahitaji yake ya msingi.Uovyo ovyo mnaouona barabarani, masokooni, vituo vya mabasi, maofisini, vyuoni, kwenye makazi ya watu ambako hakuna utawala wa kisheria-kwa sababu tu kuna watu wanaoamini kuwa wao, lao ndilo linalostahili kusikilizwa na kufuatwa na kwamba wanaweza kuwaburuza Watanzania watambue alama za nyakati kwenye ukuta.Aidha, wakati wa kuendelea kuwadanganya Watanzania kwa statistiki au takwimu zilizopikwa na kukaangwa na walaghai wakubwa wa wakati wetu umepita na hautarudi tena. Lazima taarifa zitawaliwe na ukweli na mantiki na sio vinginevyo. Sisi tuko ndani nyie mko nje na tunawaambia bunge sasa ni tamu, na msishangae mkiona hata wabunge wawili watatu wa CCM wakiungana nasi kuikosoa serikali yao hadharani.