Bunge la Kenya lamng'oa waziri wa Fedha -Kimunya

Walau hawa wanaonekana kuchukua hatua za kiutawala na kinidhamu za kuwajibishana ,hapa kwetu tatizo ni kuwa hakuna aliyetatayari kumona hatua zikichukuliwa .
 
Tatizo letu ni kuwa wakiona moshi unaanza kuwa mkubwa mawaziri wanaachia ngazi kisha wabunge wanarizika kuwa imetosha bila kuwachukulia hatua za kisheria na kinidhamu. It is like wakijiuzuru basi wamepata kinga ya sheria. Inaudhi hii kisha wanaanza kuwatetea mafisadi. Hawa mafisadi walitakiwa hata wasikaribia bunge kabisa, cha ajabu nao wanachangia mijadala bungeni.
 
siku sio nyingi huku kwetu nako kutakucha kwasni bado ni usiku na kuna giza ila kwa mbali nauona mwanga ukujitokeza .
 
Hawa ndio watu wanaojua kile wanachokifanya kwenye Bunge, angalia ufisadi wa 6 bln mtu anag'ooka lakini hapa kwetu Mramba kwenye Alex Stuwart alikatiza salama ,Mama Meghji naye akakatiza salama kwa kusema kuwa Kagoda ni national security .

sasa ni lazima wabunge wetu waweze kuiga jambo hili na kuhakikisha kuwa fisadi halikatizi kamwe.




....HAPA TANZANIA ULIONDOA WABUNGE WACHACHE WASIOFIKA 50....WALIOBAKI WOOOTE NI MBUZI ...AU KONDOO AMBAO KAZI YAO NI KUMFUATA MCHUNGAJI WAO[SPIKA NA KIKWETE ]....TU...YET WANATAKA WAFANANE MISHAHARA NA WABUNGE WA KENYA.,.....SWAIN....HAWAONI WENZAO WANAZALISHA..[WANAZUIA UFISADI]...HIZO BILIONI 133..ZA EPA...BILIONI 200 ZA IMPORT SUPPORT ...BILIONI 9 ZA IPL et al,MILIONI 150 KWA SIKU ZA DOWANS ,ets ets ....wangezizuia hizi hata wangetaka mshahara wa milioni 20 kwa mwezi ningeona sawa tu ...lakini kwa kazi ya kulala wengi wao wanayoifanya pale........hawastahili hata senti..zaidi ya box la condom kila mmoja anayelala....
 
mmhh nnaona wengi wanashindw a kuona kuwa bunge letu kuwa liko wazi zaidi na linajadili kwa uwazi na pa kuchukua hatua tunachukua

yako ya kujifunza toka kwa wenzetu lkn sio kuwa ss hatufanyi kazi sio kweli
 
Tanzania ni lazima tubadilike tuinge mfano wa kenya. Raisi aache kubebabeba mawaziri mafisadi. Director General wa PCCB TZ ajiuzulu alidanganya wananchi na Pia Mwanasheria Mkuu wa Serikali ajiuzulu kwa kuwa uwezo wake mdogo.

Wabunge wa TZ waache kulala Bungezi.

Mawaziri hawajibu maswali wanayoulizwa Bungeni.
 
Ni kweli wabunge wenyesifa na wanaofanya kazi inayotakiwa kwa mbunge hawafiki kumi to be honest. Waliobaki ni mambuzi na makondoo.
 
...Nitamshauri spika wa bunge letu Samuel Sitta andae ziara ya kutembelea bunge la kenya angalau wabunge wetu nao waende kubadirishana mawazo na wenzao kule kenya yawezekana wakirudi watakuwa moto zaidi kuliko ilivyo sasa...Sijui wao wabunge wa kenya walipotembelea bunge letu walijifunza lolote kweli toka kwa wabunge wetu au ni kuangalia tu ramani ya mjengo na mbwembwe nyingine?? Maana kama mbunge anasimama bungeni na kusema kiongozi asisemwe hata kama kafanya ufisadi kisa eti kawajengea jengo la kisasa la bunge napata mashaka na kiwango cha uwezo wa kufikiri cha baadhi ya waheshimiwa wetu..... Ni ujinga au ndio kubebana??
 
Bunge la Kenya jana lilimng'oa Waziri wa fedha kutokana na tuhuma za Rushwa na Ufisadi kwa kumpigia kura ya kukosa imani naye .

Waziri huyu Kivuitu nafikiri wengi mtamkumbuka jinsi ambavyo alikuwa na kiburi wakati wa kujibu maswali kuhusiana na uchaguzi mkuu akishirikiana na Amos Kimunya .

Nitawaletea taarifa zaidi hapa .

Wasiwasi wangu ni kuwa huenda huu ukawa ni muendelezo wa Mapamabano ya Raila vs Kibaki.

Hongereni wabunge wa Kenya. Hivi ndiyo linatakiwa liwe. Siyo Bunge la Tanzania wataanza kujibaraguza baraguza huyu ni 'mwenzetu' kaonewa, tuunde kamati ya kumchunguza, kamati yenyewe ikiundwa wataamua nini cha kuandika au kutoandika ili 'kulinda heshima ya serikali. Matokeo yake nchi inazidi kuangamia. Hongereni sana.
 
Hatimaye KIMUNYA amejiuzulu baada kutakiwa na Rais wake ili kupisha UCHUNGUZI.
 
Mbona alisema yuko tayari kufa kuliko kujiuzulu, imekuwaje amekubali kujiuzulu ama kifo ndo kitafuata?

Politics za Kenya ninazipenda sana, watu wakishupalia kitu lazima wahakikishe kinafika mwisho wake. Sasa ngoja Kimunya akakalie benchi kwanza huku akitafakari zile kauli za baada ya Uchaguzi.

Martha Karua anapiga mbinja tu maana njia sasa ni nyeupe na iko wazi ndani ya NARC-Kenya na Central Region kupitia chama chake. 2012 itawafanya mawaziri wawe na nidhamu!
 
Alisema pia kwamba anataka kuondoka na Waziri Mkuu Odinga na vigogo wengine!
Siasa ni hasa.
 
Mbona alisema yuko tayari kufa kuliko kujiuzulu, imekuwaje amekubali kujiuzulu ama kifo ndo kitafuata?

Politics za Kenya ninazipenda sana, watu wakishupalia kitu lazima wahakikishe kinafika mwisho wake. Sasa ngoja Kimunya akakalie benchi kwanza huku akitafakari zile kauli za baada ya Uchaguzi.

Martha Karua anapiga mbinja tu maana njia sasa ni nyeupe na iko wazi ndani ya NARC-Kenya na Central Region kupitia chama chake. 2012 itawafanya mawaziri wawe na nidhamu!

Alisema pia kwamba anataka kuondoka na Waziri Mkuu Odinga na vigogo wengine!
Siasa ni hasa.

Tusubiri labda atajinyonga jioni hii maana jinsi alivyo sisitiza ilinitisha
 
Wenzetu hapa hata hawajaunda tume lakini mwanaume amedondoka huku kwetu na tume juu ya tume result ni zap zero kulishana mapesa tu. wabunge wetu waamke na wajue kwamba kuna kazi watumwa wafanye sio kupokea mishahara mikubwa for nothing
 
Hapa mi ndo nashangaa jamani wabongo sijui tukoje? Just imagine sie na wakenya tuivo majirani.. lakini wenzetu wanafanyakweli, sie ndo kwaaanza tunashangilia na kulinda siri za mafisadi! duuu.. Mungu tunusuru
 
Back
Top Bottom