BUNGE LA KATIBA: Yanayojiri leo tarehe 27/02/2014

Acha udini kwani niyeye peke yake aliyeongelea kura za siri! Mbona wacangiaji wengi tu ameliona hilo kuna haja gani kumpa misifa yote isiyo na maana.

"Wacangiaji wengi tu ameliona". Kwa wataalamu wa lugha adhimu ya kiswahili wanisaidie mnyumbuliko wa hiyo quoted sentens kabla sijamjibu.
 
Ndie mwana CCM wa kwanza kuunga mkono hoja almost zote za kamati ya kanuni.....anapongezwa kupingana na chama chake kuwa si haki kupiga kura za wazi ilihali yeye anamchagua Mwenyekiti wake kwa kura siri. Anashangazwa leo tunataka kuvunja haki ya mwananchi.
 
Kilango siku za hivi karibuni baada ya kukatiwa kitu kidogo na mashefa ya EPA kapoteza dira kabisa.
 
Hoja ya kura ya siri ni ya msingi,waliokuwa wakitolewa kucha bila ganzi,ni kwa sababu ya kuwa mtazamo kinzani na serikali/utawala.
 
Ndie mwana CCM wa kwanza kuunga mkono hoja almost zote za kamati ya kanuni.....anapongezwa kupingana na chama chake kuwa si haki kupiga kura za wazi ilihali yeye anamchagua Mwenyekiti wake kwa kura siri. Anashangazwa leo tunataka kuvunja haki ya mwananchi.

Kura ya siri ni Kitanzi kwa CCM.
 
Natazama Bunge la Katiba kupitia startv Namuona Juma Duni Haji akizungumza kwa uchungu sana kuhusu kura;akiomba kura ziwe za siri na sio za wazi ;;kwa hii naliiunga mkono;
Kilango nae anapendekeza kura zipigwe kwa siri;adai Prof Lipumba kamshawishi sana
 
Nani atakubaliana nawe katika hoja yako? Wewe unaona ni vyema kuliteka Bunge Maalum la Katiba kwa siku ya pili sasa kujadili jambo la kura tu? Kwamba iwe ya siri au ya wazi? Iko wazi kabisa kuwa kura zote zinazotoa hatma ya jambo fulani hupigwa kwa siri. Inategemewa kuwa kura inayozungumzwa sasa katika Bunge Maalum la Katiba itatumika hasa katika kupitisha Ibara za Rasimu huko Dodoma. Yafaa iwe ya siri.

Waonaji wameshaona.Kuwa kura iwe ya siri. Na ndivyo ilivyo. Uwazi uwepo lakini usiwe katika kura ya kutoa mustakabali wa jambo fulani muhimu kama hili la Katiba mpya. Prof. Tibaijuka,nakuheshimu sana. Lakikini kaika hili uliteleza. Ni muda wako kuomba nafasi ya kuchangia na kujirudi.
Mkuu ccm waliweka maamuzi yawe kwa kura na mpango wao ulikuwa ni kura ya uwazi kwa malengo kuwa itawatisha wafuasi wao ama wale wenye kuteuliwa na raisi ili waendelee kupata upendeleo wa raisi lakini tunakoelekea ni mpango huo kushindikana maana naona tunaelekea kwenye kura ya siri... tusubiri plan b ya ccm
 
Back
Top Bottom