mwankuga
JF-Expert Member
- Aug 30, 2010
- 334
- 120
Wakati Watanzania wengi wanasubiri kwa hamu bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 20111/2012,hali ya maisha inazidi kupanda.Hapa Dodoma wananchi wa kawaida wanaendelea kutafuta riziki zao,huku wengi wao wakiwa hawategemei jipya katika bajeti hiyo.Wananchi wengi wanasema bajeti haiwasadii kwa lolote zaidi ya kuwaumiza kwani wakubwa wamekuwa wakijijali wenyewe.Wakati hayo wakiendelea,kwa upande wa pili,serikali inategemea kusoma bajeti yake (mapato na matumizi) hapo tarehe 08/06/2011.
Pengine kinachosubiriwa ni takwimu za mapato na matumizi kwa upande wa miradi ya maendeleo na matumizi ya kawaida katika ofisi za umma.Bajeti hiyo imeandaliwa kwa kuzingatia Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025,Mpango wa Maendeleo kwa miaka 5 ambao unaanza kwa mwaka wa fedha 2011/2012,MKUKUTA 11,Ilani ya CCM ya uchaguzi ya 2010-2015 na itazingatia vipaumbele alivyovitaja rais katika hotuba ya kufungua bunge aliyoitoa tarehe 18/11/2011.
Aidha vipaumbele vya taifa kwa miaka 5 (2010-2015) ni kama ifuatavyo;
1) ELIMU.
" Kuboresha kiwango cha elimu kwa kuhakikisha vitabu vya kufundishia vinapatikana shuleni,kujenga maabara,upatikanaji wa madawati na kuweka mazingira bora ya kujifunzia kwa walemavu.
2) Kilimo,Mifugo na Uvuvi.
" Kujenga na kukarabati miundombinu ya umwagiliaji,kuwezesha kuwepo kwa pembejeo za kilimo,mifugo na uvuvi,kuendeleza tafiti,kuwezesha sekta binafsi ili kuwekeza katika kilimo,mifugo na uvuvi na kuhakikisha masoko kwa wakulima yanakuwepo
3) Nishati.
" Kuzalisha umeme kwa uwingi kwa kutumia vyanzo mbalimbali,kuimarisha miundombinu ya kuzalisha na kusambaza umeme,kuimarisha miundombinu ya kuzalisha na kusafirishia gesi asilia.
4) Miundombinu na Usafirishaji.
Kujenga na kukarabati barabara,madaraja na vivuko,kujenga na kuimarisha majengo ya serikali,kuimarisha miundombinu ya reli,viwanja vya ndege na bandari.
5) Maendeleo ya Viwanda.
6) Afya
7) Maji
8) Ardhi,Nyumba na Makazi
9) Huduma za Afya
10) Masuala Mtambuka
Lakini suala kubwa ni kuona serikali inaweka mikakati ya kupunguza matumizi yake na kukusanya mapato hasa kwa makampuni makubwa yakiwemo ya uchimbaji wa madini ambayo kwa muda mrefu yamekuwa yakisamehewa kodi,na mzigo wa kodi ukimwegemea zaidi mwananchi wa kawaida.Kawa kawaida kodi kwa vinywaji kama vile bia,sigara n.k vinategemewa kupanda,kwani serikali imekuwa ikifanya hivyo kwa miaka yote.Watumishi wa umma wasitegemme jipya katika mishahara .Tusubiri tuone
Pengine kinachosubiriwa ni takwimu za mapato na matumizi kwa upande wa miradi ya maendeleo na matumizi ya kawaida katika ofisi za umma.Bajeti hiyo imeandaliwa kwa kuzingatia Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025,Mpango wa Maendeleo kwa miaka 5 ambao unaanza kwa mwaka wa fedha 2011/2012,MKUKUTA 11,Ilani ya CCM ya uchaguzi ya 2010-2015 na itazingatia vipaumbele alivyovitaja rais katika hotuba ya kufungua bunge aliyoitoa tarehe 18/11/2011.
Aidha vipaumbele vya taifa kwa miaka 5 (2010-2015) ni kama ifuatavyo;
1) ELIMU.
" Kuboresha kiwango cha elimu kwa kuhakikisha vitabu vya kufundishia vinapatikana shuleni,kujenga maabara,upatikanaji wa madawati na kuweka mazingira bora ya kujifunzia kwa walemavu.
2) Kilimo,Mifugo na Uvuvi.
" Kujenga na kukarabati miundombinu ya umwagiliaji,kuwezesha kuwepo kwa pembejeo za kilimo,mifugo na uvuvi,kuendeleza tafiti,kuwezesha sekta binafsi ili kuwekeza katika kilimo,mifugo na uvuvi na kuhakikisha masoko kwa wakulima yanakuwepo
3) Nishati.
" Kuzalisha umeme kwa uwingi kwa kutumia vyanzo mbalimbali,kuimarisha miundombinu ya kuzalisha na kusambaza umeme,kuimarisha miundombinu ya kuzalisha na kusafirishia gesi asilia.
4) Miundombinu na Usafirishaji.
Kujenga na kukarabati barabara,madaraja na vivuko,kujenga na kuimarisha majengo ya serikali,kuimarisha miundombinu ya reli,viwanja vya ndege na bandari.
5) Maendeleo ya Viwanda.
6) Afya
7) Maji
8) Ardhi,Nyumba na Makazi
9) Huduma za Afya
10) Masuala Mtambuka
Lakini suala kubwa ni kuona serikali inaweka mikakati ya kupunguza matumizi yake na kukusanya mapato hasa kwa makampuni makubwa yakiwemo ya uchimbaji wa madini ambayo kwa muda mrefu yamekuwa yakisamehewa kodi,na mzigo wa kodi ukimwegemea zaidi mwananchi wa kawaida.Kawa kawaida kodi kwa vinywaji kama vile bia,sigara n.k vinategemewa kupanda,kwani serikali imekuwa ikifanya hivyo kwa miaka yote.Watumishi wa umma wasitegemme jipya katika mishahara .Tusubiri tuone