Bunge kumalizika Ijumaa kisa JK atia kwapani Hotuba yake

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Habari za ndani toka hapa Kilimani zinasema wanachama wa jumba la baridi safari hii watakaa hapa Dodoma wiki 2 tu na kuondoka maana hawana la kufanya zaidi .Wengi wao walitegemea kwamba hotuba ya ndugu Rais itakuwa wazi iwape kamuda ka kukamua katika lile jumba na kula mbuzi Dodoma lakini sasa imethibitika rasmi kwamba , JK aliweka hotuba yake kwapani akalala nayo mbele na ndiyo maana Spika alisema haitaweza kujadiliwa maana hata kwenye hansard hakuna kitu .

Mimi najiuliza na nawauliza wadau wenzangu .Ni kawaida kwamba Mkulu anaingia Bungeni na kutema cheche baadaye anaweka ngoma kwapani anaondoka ? Ni kitu gani kimefichwa ambacho JK hakutaka kiwe katika records?
 
Samahani ndugu Lunyungu, naomba kuuliza...je kuna sheria yeyote inayohusu mhutubu kuacha hotuba yake kwa aliowahutubia baada kuhutubia?
 
Samahani ndugu Lunyungu, naomba kuuliza...je kuna sheria yeyote inayohusu mhutubu kuacha hotuba yake kwa aliowahutubia baada kuhutubia?


Kuna sheria inayotaka mambo ya bungeni yabaki kwenye kumbukumbu rasmi za bunge(hansard) unless spika aseme kitu fulani si rasmi kisiingie. Kwa hiyo jamani ile hotuba ya JK haikuwa rasmi? Its a national shame/scam!

Asha
 
Bunge la vikaragosi, kwani ni lini hili bunge lilishafanya maamuzi tofauti? I think hata hapo wamechelewa, wangefunga the second day walipofika chimwaga.
 
Kuna sheria inayotaka mambo ya bungeni yabaki kwenye kumbukumbu rasmi za bunge(hansard) unless spika aseme kitu fulani si rasmi kisiingie. Kwa hiyo jamani ile hotuba ya JK haikuwa rasmi? Its a national shame/scam!

Asha


Hao wabunge si walisikiliza? na bungeni kuna marapprteurs hawakupata chochote toka kwa hiyo hotuba? Huwa hawarekodi?
 
Kuna sheria inayotaka mambo ya bungeni yabaki kwenye kumbukumbu rasmi za bunge(hansard) unless spika aseme kitu fulani si rasmi kisiingie. Kwa hiyo jamani ile hotuba ya JK haikuwa rasmi? Its a national shame/scam!

Asha

Kwa hiyo tatizo la kutowepo rekodi za hotuna ya JK Bungeni ni la Bunge lenyewe. Ile hotuba waliirekodi yote, na watumishi wa hansard walisha-transcribe, lakini cha ajabu hadi leo si hotuba tu, bali hansard ya Agosti 21, 2001 haijawekwa kwenye tovuti ya Bunge
 
Hao wabunge si walisikiliza? na bungeni kuna marapprteurs hawakupata chochote toka kwa hiyo hotuba? Huwa hawarekodi?

Ni lazima kila jambo lisemwapo Bungeni kumbukumbu zipatikane huko na ndiyo maana waheshimiwa wanalia lia hovyo maana wanashangaa JK kuondoka na hotuba kwapani na wameshindwa kuijadili .Nia yake kwenda Bunge ilikuwa kuweka kumbu kumbu wazi na leo hakuna .Hii ni aibu kwa Mzee huyu .Tumekosa mwelekeo na hawataki kumsikiliza Warioba .

Je kuna mtu anaweza kuwa na undani wa kwa nini alichukua hotuba na kulala nayo mbele ?
 
Tumekosa mwelekeo na hawataki kumsikiliza Warioba. Je kuna mtu anaweza kuwa na undani wa kwa nini alichukua hotuba na kulala nayo mbele ?

Namsikitikia Warioba kwa sababu anakuwa kama sauti ya mtu aliaye nyikani, mzee wa watu anaandaliwa kutwishwa mizigo kuliko ya EPA.
Kuhusu hiyo hotuba Bunge wasitake kukwepa lolote, wanayo, kwa sauti na sofy copy, wasilikimbie hilo
 
Ni lazima kila jambo lisemwapo Bungeni kumbukumbu zipatikane huko na ndiyo maana waheshimiwa wanalia lia hovyo maana wanashangaa JK kuondoka na hotuba kwapani na wameshindwa kuijadili .Nia yake kwenda Bunge ilikuwa kuweka kumbu kumbu wazi na leo hakuna .Hii ni aibu kwa Mzee huyu .Tumekosa mwelekeo na hawataki kumsikiliza Warioba .

Je kuna mtu anaweza kuwa na undani wa kwa nini alichukua hotuba na kulala nayo mbele ?

Ni kawaida bali sio sheria. Hii ndio inayowafanya hao wabunge kusinzia na kulala bungeni! inawezekanaje washindwe kudiscuss yaliyosemwa na rais kwa vile tu rais kamaliza kuhutubia na kuondoka na hotuba yake?

Hao wanajua kila kitu, kama ada yao hawakosi kutafuta mchawi wakati mchawi ni wao wenyewe!
 
Kuna sheria inayotaka mambo ya bungeni yabaki kwenye kumbukumbu rasmi za bunge(hansard) unless spika aseme kitu fulani si rasmi kisiingie.

Wakuu hebu acheni utani huu, hivi ile iliyomnasa mzee wa vijisenti akinyunyizia si ipo, lakini tuliambwia alikuwa anatafuta kiti chake usiku wa manane, sasa mnafikiri kweli hawana majibu ya hii ya hotuba ya Muungwana?

Waulizeni tuone kama kweli hawana majibu! Sometimes tusiwe tunawa-underestimate sana as far as usanii is concerned!
 
Ni kawaida bali sio sheria. Hii ndio inayowafanya hao wabunge kusinzia na kulala bungeni! inawezekanaje washindwe kudiscuss yaliyosemwa na rais kwa vile tu rais kamaliza kuhutubia na kuondoka na hotuba yake?

Hao wanajua kila kitu, kama ada yao hawakosi kutafuta mchawi wakati mchawi ni wao wenyewe!

Mimi naona na wao wako katika mgomo kama Waalimu na Wazee wa EA maana na wao mshahara wao hawajapata .Labda wawe wamepata jana lakini wote nilio kutana nao pale Dar walikuwa wanashangaa kwamba Wanawezaje kukosa mishahara yao .Nika wauliza kama wao walikuwa na tofauti na watanzania wengine kama waalimu na wazee wa EA .Wakasema we Lunyungu acha hizo kijana .

Wanajua sana alicho kisema Rais ial hawawezi kujadili wakiwa hawana kitu maandiko .Maana Makinda kama kawaida atawaomba ushahidi wa mjadala wao kama alivyo muomba Mzee Ndesa wakati akichangia hoja .Kwa kifupi kuna magumashi hapa si bure .
 
Wakuu hebu acheni utani huu, hivi ile iliyomnasa mzee wa vijisenti akinyunyizia si ipo, lakini tuliambwia alikuwa anatafuta kiti chake usiku wa manane, sasa mnafikiri kweli hawana majibu ya hii ya hotuba ya Muungwana?

Waulizeni tuone kama kweli hawana majibu!

Tena wakati ule Ikulu walipoulizwa kwa nini hawaitoa hotuba walisema kuwa wameomba iliyorekodiwa Bungeni ili kurekebisha yale ambayo Mkuu aliyaongezea papo kwa papo-Kwa hiyo Bunge inayo hotuba hiyo, wasitake kutuzuga
 
Mimi naona na wao wako katika mgomo kama Waalimu na Wazee wa EA maana na wao mshahara wao hawajapata .Labda wawe wamepata jana lakini wote nilio kutana nao pale Dar walikuwa wanashangaa kwamba Wanawezaje kukosa mishahara yao .Nika wauliza kama wao walikuwa na tofauti na watanzania wengine kama waalimu na wazee wa EA .Wakasema we Lunyungu acha hizo kijana .

Wanajua sana alicho kisema Rais ial hawawezi kujadili wakiwa hawana kitu maandiko. Maana Makinda kama kawaida atawaomba ushahidi wa mjadala wao kama alivyo muomba Mzee Ndesa wakati akichangia hoja .Kwa kifupi kuna magumashi hapa si bure .


Hili ni la bunge kwa ujumla, hapa hakuna cha makinda sita ya kware wa mkwere. Bunge liwe responsible kwa kukosekana kwa hotuba hiyo kama sheria inalazimisha iwepo. Kama hakuna sheria ya kuacha muhutubu kuacha hotuba, inakuwaje kuna sheria ya wahutubiwa kudiscuss hotuba husika kwa kuwa na ushahidi wa hotuba hiyo? Pole Watanzania.
 
Kwa maoni yangu, sababu zote zinazotolewa sizo. Liko jambo!.
Kisingizio cha Mh.JK. Hakuicha hotuba sio kweli. Hotuba ile iko audio recorded na video recorded na bunge wenyewe. Tbc na Star Tv walirusha live huku wakirekodi off-air. Itv walijiunga na Star Tv na Channel ten walijiunga na Tbc na zote walirekodi. Hiyo habari ya kutojadiliwa kwa kisingizio cha hansard sio kweli.

Spika Six atuambie kweli,
 
Habari za ndani toka hapa Kilimani zinasema wanachama wa jumba la baridi safari hii watakaa hapa Dodoma wiki 2 tu na kuondoka maana hawana la kufanya zaidi .Wengi wao walitegemea kwamba hotuba ya ndugu Rais itakuwa wazi iwape kamuda ka kukamua katika lile jumba na kula mbuzi Dodoma lakini sasa imethibitika rasmi kwamba , JK aliweka hotuba yake kwapani akalala nayo mbele na ndiyo maana Spika alisema haitaweza kujadiliwa maana hata kwenye hansard hakuna kitu .

[B]Mimi najiuliza na nawauliza wadau wenzangu .Ni kawaida kwamba Mkulu anaingia Bungeni na kutema cheche baadaye anaweka ngoma kwapani anaondoka ? Ni kitu gani kimefichwa ambacho JK hakutaka kiwe katika records?
[/B]

hataki usemi wake wa "UKITAKA KULA KUBALI ULIWE" ujulikane kwenye hansard

macinkus
 
[/B][/I][/B]

hataki usemi wake wa "UKITAKA KULA KUBALI ULIWE" ujulikane kwenye hansard

macinkus

Sasa anaogopa huo usemi kukaa kwenye hansard wakati alipozungumza pale bungeni dunia yote ilikuwa inamsikiliza???!!!!
 
Sasa atakimbia kivuli chake hadi lini jamani .Maana kila kukicha kila afanyalo ama asemalo lazima linakuwa mwiba baada ya siku chache za watu kutafasiri .
 
Sasa atakimbia kivuli chake hadi lini jamani .Maana kila kukicha kila afanyalo ama asemalo lazima linakuwa mwiba baada ya siku chache za watu kutafasiri .

Nadhani sehemu iliyobaki inahitaji ujasiri wa wananchi kutenda zaidi ya kumweleza maana kama ni kuelezwa ameshaelezwa yote. Kama anajua kusoma alama za nyakati, atakuwa anafahamu kuwa hali si shwari hata kidogo. Lakini bado ana nafasi ya kutengana na mafisadi na nadhani wananchi wanaweza kumsamehe akiamua kuanza upya-lakini awe mweli, si mzugaji
 
Jamani nyie, Mnazugwa na mnazugika. Hotuba wanayo na imeshachapwa kama kitabu. Wanaichelewesha makusudi ili ipitwe na wakati ishindwe kujadilika. Sababu kuu ni kuwepo katika hotuba hiyo hoja ya Rais kuwasemehe mafisadi ambayo ni kuvunja katiba na kudharau sheria. Imehofiwa kuwa ikijadiliwa sasa kuna wabunge watatoa hoja ya kura ya kutokuwa na imani na rais. Kwa hiyo sasa wanasubiri kesi za wale ambao wajarudisha vijisenti zifunguliwe kinasanii mahakamani halafu hotuba itawawanywa. Wakati huo hakutakuwa tena na umuhimu wa kuijadili.

Lakini Kikwete na wajinga wenzie hawajui tu kwamba hili halimsaidii yeye wala wao.

Asha
 
Jamani nyie, Mnazugwa na mnazugika. Hotuba wanayo na imeshachapwa kama kitabu. Wanaichelewesha makusudi ili ipitwe na wakati ishindwe kujadilika. Sababu kuu ni kuwepo katika hotuba hiyo hoja ya Rais kuwasemehe mafisadi ambayo ni kuvunja katiba na kudharau sheria. Imehofiwa kuwa ikijadiliwa sasa kuna wabunge watatoa hoja ya kura ya kutokuwa na imani na rais. Kwa hiyo sasa wanasubiri kesi za wale ambao wajarudisha vijisenti zifunguliwe kinasanii mahakamani halafu hotuba itawawanywa. Wakati huo hakutakuwa tena na umuhimu wa kuijadili.

Lakini Kikwete na wajinga wenzie hawajui tu kwamba hili halimsaidii yeye wala wao.

Asha

Mzee wa siasa za majitaka mbona alikuwa wa kwanza kusema juu ya hotuba hii kutojadiliwa , alipata maelekezo ama ilikuwaje ?Kweli kwa CCM ya sasa hakuona Mbunge anaweza kusimama na kudai hana imani na JK maana wanaweza kumgombani kama mpira wa kona .Masikini JK alama hizi hata Msekwa alishindwa kuzisoma akasombwa na mafuriko .Sie yetu macho na muda ukifika tutawakumbusha wote haya yote.
 
Back
Top Bottom